Pole Kamanda mambo ya ujana achana nayo kabisa.....mimi nilisha wahi weka miadi na demu zamani, ikifika saa sita usiku nitupie jiwe juu ya nyumba yao, mamsap atakoka nje tumalizane kwenye kiambaza cha nyumba...nilirusha mawe kama matatu hivi kwenye ile nyumba ajabu akatoka baba mtoto akiwa na gobore.......ilinibidi nilale kwenye majani kwenye shamba la mahindi......huku nikuaibika sana. Demu tulipoonana kanisani akasema dingi ndo alikuwa amerudi toka ulevini.
Pole sana mheshimiwa, ila nimecheka mbavu sina. Jambo moja linalonishangaza, yaani ukakubali risk ya kuruka watu wote hao ukamfuate huyo Suzy pembezoni alikolala? What if watu wengine wangestuka in the process?
Hii imenikuta juzi hapa hapa nilipata kidosho toka Iringa nikapiga sound mtoto akaingia laini tukapeana promise siku tuonane siku ya siku ikafika mzee mzima nimeulamba nikakutana na kidosho basi nikawa natafuta kiwanja mulua cha kupoa nae mtoto wa kihehe nikapata kiota mulua naingia tu nakuta kiti akatokea mzee mmoja wa makamu sana akanishika mkono akaniuliza huyu kwako nani kabla sijajibu akashika mkono wa kidosho akamuuliza huyu nani wako akasema ndugu yangu mm nikawa mdogo pale pale yule mzee nikamwangalia ni babu yangu kumwangalia binti ni 21yrs dingi akaaanza kukoloma huyu ni mke wangu nimegaramia kutoka Iringa mpaka hapa wewe unajibebea kiulani ikabidi watu waingilie kati wakajua mm na uhusiano na mwanafunzi kuja kusikia maelezo ya babu yule akasema mke wake. Nilichoka nikaishiwa pumnzi pale pale.
Watu nao pale wakachoka ikabidi waanze kumzomea mzee yule ooof FATAKI huyoo.
Mhhh! angekuchoma mkuki!
Kumbe hivi visa huwakuta watu wengine pia ee? afadhali bwana kifo cha wengi harusi!
MwanajamiiOne, darasa la tatu unasome twisheni....au ndo mmesoma juzi juzi hapa hizi shule za akademi manake hazina dogo, unalijua azimio la arusha? LOL
Mbona sie tuition ilikuwa tangu std 2!! Si unajua tena shule za kapumua nani, mwalimu anataka ahemee hapo hapo. Ilikuwa tuition ya lazima ndugu yangu.
Na kweli ndugu yangu, ndio maana wanadai hiyo midadi ikichachamaa, kichwani kunakuwa kutupu kabisaaa...
hahaha Masanilo afadhali ulijificha maana duh sipati picha.
nakumbuka wakati nasoma darasa la tatu wakati huo nilikuwa mpole sana kiasi kwamba nlikuwa naambiwa maringa. Siku moja nikiwa naelekea tuition mchana nje kidogo tu ya nyumba yetu nikawakuta vijana majirani zetu wakiwa wamekaa kwenye kijiwe. Mmoja wao alikuwaga ananisumbua sana kunitaka kimapenzi nikawa naogopa kumkatalia (alikuwa mgomvi, mvuta bangi na mkubwa kiasi) nilijua atanipiga na pia sikuweza kumkubali nikaishia kumkimbia kila nikimwona ili asikumbushie ombi lake.
Basi siku hiyo aliponiona wacha anitolee uvivu kuwa naringa kitu gani kwanza naniliu yenyewe si mali kitu kwani hata nikibania italiwa na nyenyere nitakapokufa. Alipaka kwa nguvu tena bila tafsida. Sikuthubutu kumjibu kwani nilikuwa mwoga sana.
Fedheha ilinipata nilipogeuka nyuma na kumkuta Mdingi amesimama getini akinitizama!! Mpaka leo huwa sisahau.
Kuna siku nilikutana na yule mkaka ukubwani (akanambia yeye ni dereva tax - alikuwa na bonge la alama ya panga katika paji la uso- nilisikiaga aliingia kwenye ujambazi) duh
....Mjamii, inaelekea ulikuwa umejazia jazia hivi! yaani uko darasa la tatu na bado njemba zinakukomalia??
Hakuna lolote BabaDesi basi tu utundu wa wanyantuzu!
Hili linawakilisha wabongo nadhani, siyo wanyantuzu halisi ee?
Kwa maana halisi ya neno hilo Mzizi wa Mbuyu- nilikuwa nasoma kwa wanyantuzu kanda ya Ziwa!