Jinsi nilivyonusurika kupata HIV

Jinsi nilivyonusurika kupata HIV

Nzi Chuma

JF-Expert Member
Joined
Jun 21, 2015
Posts
475
Reaction score
1,176
Wakuu nawasalimu.

Ni mambo ya mitandaoni tu, nimekutana nae. Mrembo sana. Kwakua familia iko mbali kidogo, nikaona nitume nauli aje mkoani tuponde raha. Professionally ni nurse, na nliwasiliana nae kwa miezi zaidi ya mitatu nikajiridhisha kuwa ni mtu mzuri ameshika dini hana shida. Siku ikafika, nauli nkatuma, basi likapandwa. Katika kujihakikishia usalama wa afya zetu, alinambia atakuja na vipimo vya "HIV rapid test". Nikasema sawa.

Alipofika, kabla hatujaanza mambo yetu akatoa vipimo..akanitoboa akatoa damu akaweka kwenye kipimo akaweka vile vimaji akaweka chini kusubiri matokeo. Muda huo nikatoboa kidole chake tukaweka damu kwenye kipimo kingine. Majibu yangu yakatoka negative na yeye akaona dalili za kutoka positive.. akaanza kuzuga anashika kipimo.. nikampokonya nikaweka pale.. goma likasoma vistari viwili vya HIV-1, ambayo ndiyo HIV common kwa huku kwetu. Pozi likaniishia. Hamu ikakata. Nikamwambia lala mpaka asubuhi, nitakupa nauli uondoke kwa amani. Kulipokucha tu nikampandisha gari za kwao.

Tukirudi nyuma kidogo, najiuliza, ingekuaje kama asingekuja na vipimo na mimi nisivyoweza kutumia kondom? Ningefanyaje?! Si ningeikwaa ngoma kirahisi sana. Nimejifunza kuwa makini!. Vijana tuwe makini tutunze afya zetu na tuzidi kumuomba Mungu, ana kawaida ya kutuepusha na majanga tusiyoyatarajia.

Siku njema wakuu!
 
Ivo Vipimo bado havina Accurancy ya 100%, Umefeli kula nyama bure boya wewe
Bro, siku ya pili baada ya kufika safari akanambia kaenda hsptal akapima tena wakamwambia ni kweli anayo maambukizi.
 
Kuna tatizo mahala. Atakuwa ni mjinga kiasi cha kuja kufanya vipimo hapo kwako bila kujipima mwenyewe kwanza na vipimo ni vyake? Au isije ikawa mlichanganya vipimo. Embu pima tena.
Bro, sijachanganya vipimo, cha kwangu nlikua nacho na kilitoa majibu kabla ya chake
 
Bro, sijachanganya vipimo, cha kwangu nlikua nacho na kilitoa majibu kabla ya chake
Ookey mkuu. Basi hajielewi. Kwa mazingira hayo mtu hujipima kwanza kabla ya kujimwambafy. Halafu vile wanasema havionyeshagi + kama ni miezi mitatu kurudi nyuma na vinakuwa aggresive kweli.

Huu ugonjwa umekaa kitapeli tapeli sana. Wazungu si wa kuamini 100%
 
Ookey mkuu. Basi hajielewi. Kwa mazingira hayo mtu hujipima kwanza kabla ya kujimwambafy. Halafu vile wanasema havionyeshagi + kama ni miezi mitatu kurudi nyuma na vinakuwa aggresive kweli.

Huu ugonjwa umekaa kitapeli tapeli sana. Wazungu si wa kuamini 100%
Ni kweli. Huu ugonjwa unaweza kuishi kwa wasiwasi kumbe upo fresh tu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom