Mayu
JF-Expert Member
- May 11, 2010
- 8,402
- 13,764
Wakuu wiki iliopita wajanja walikata wavu wakakwapua kimeo cha shemeji yenu iphone 4, na kwa msaada wa apps za cydia nikafanikiwa kuipata iphone tena
Kwanza hatukukimbilia kuiweka kwenye lost mode icloud maana uwezekana wa kuipata ungekuwa mdogo
Iphone ipo jailbrake na nika install apps mbili kutoka cydia iLostfinder na inner
Kazi ya iLostFinder ni mtu akikikosea mara kadhaa kuingiza password basi itaonyesha ujumbe wa maandishi madogo kwa kadri utakavyokuwa unataka ujumbe gani (mfano unaweza kuandika usomeke " Simu imepotea tafadhali wasiliana na mwenyewe kwa no 086777 nk).
Na wakati anasoma hayo maandishi kwakuwa madogo hivyo atasogeza uso basi app hii itampiga picha na kutuma kwenye email ulioset
Pia inazuia mtu kuzima simu, simu haizimiki hadi iishe chaji
Kazi inner ni akibadili tu line inatuma sms kwa namba utakazo set hivyo utajua namba mpya inayotumia simu yako
Pia ina track sms, call log na pic kwenye camera roll, uki login kwenye web unaona kila anachofanya
Walipokwapua tu jumla ya sura 16 zikatumwa kwenye email . Zikiwemo za wezi na mafundi kadhaa wa simu hadi wa kariakoo
Wakafanikiwa kutoa screen lock, inner ikaanza kutuma kila simcard inayowekwa
Na pia ikaanza kutrack mawasiliano yote ya iphone ikiwemo. Sms, call log na picha
Kazi ikawa rahisi kama kumsukuma mlevi vile
Sura za wezi hatukuzutambua lakini tukatambua sura ya fundi simu wa tunapoishi, tukampiga biti na picha yake na muda tukamuonyesha, akamtaja teja aliyemtea aitoe lock ikamshinda akamrudishia, tukadaka teja tukaweka ndani, teka likasema limempa mshkaji wake akampa elf10 sababu simu hizi hazifunguki, huyo mshkaji wa teja alipopata taarifa akakimbia mji
Simu ikawa kinya kama wiki mbili haitumi chochote, mara ghafla zikaanza sms, tukajua imetolewa screen lock, ikabadilishwa line kama mara 4 hivi ya tano ikawa kimya, siku alipiingia online tu tukaanza kupata watu wote anao sms na anaopigiana nao simu na picha zake kibao anajipiga
Kulingana na sms tukajua hadi anapofanyia kazi tukaenda na polisi tukamdaka kama kuku wa kisasa
Akakiri kauziwa na mtu
Hatukutaka tabu tukachukua simu yetu tukasepa
Kwanza hatukukimbilia kuiweka kwenye lost mode icloud maana uwezekana wa kuipata ungekuwa mdogo
Iphone ipo jailbrake na nika install apps mbili kutoka cydia iLostfinder na inner
Kazi ya iLostFinder ni mtu akikikosea mara kadhaa kuingiza password basi itaonyesha ujumbe wa maandishi madogo kwa kadri utakavyokuwa unataka ujumbe gani (mfano unaweza kuandika usomeke " Simu imepotea tafadhali wasiliana na mwenyewe kwa no 086777 nk).
Na wakati anasoma hayo maandishi kwakuwa madogo hivyo atasogeza uso basi app hii itampiga picha na kutuma kwenye email ulioset
Pia inazuia mtu kuzima simu, simu haizimiki hadi iishe chaji
Kazi inner ni akibadili tu line inatuma sms kwa namba utakazo set hivyo utajua namba mpya inayotumia simu yako
Pia ina track sms, call log na pic kwenye camera roll, uki login kwenye web unaona kila anachofanya
Walipokwapua tu jumla ya sura 16 zikatumwa kwenye email . Zikiwemo za wezi na mafundi kadhaa wa simu hadi wa kariakoo
Wakafanikiwa kutoa screen lock, inner ikaanza kutuma kila simcard inayowekwa
Na pia ikaanza kutrack mawasiliano yote ya iphone ikiwemo. Sms, call log na picha
Kazi ikawa rahisi kama kumsukuma mlevi vile
Sura za wezi hatukuzutambua lakini tukatambua sura ya fundi simu wa tunapoishi, tukampiga biti na picha yake na muda tukamuonyesha, akamtaja teja aliyemtea aitoe lock ikamshinda akamrudishia, tukadaka teja tukaweka ndani, teka likasema limempa mshkaji wake akampa elf10 sababu simu hizi hazifunguki, huyo mshkaji wa teja alipopata taarifa akakimbia mji
Simu ikawa kinya kama wiki mbili haitumi chochote, mara ghafla zikaanza sms, tukajua imetolewa screen lock, ikabadilishwa line kama mara 4 hivi ya tano ikawa kimya, siku alipiingia online tu tukaanza kupata watu wote anao sms na anaopigiana nao simu na picha zake kibao anajipiga
Kulingana na sms tukajua hadi anapofanyia kazi tukaenda na polisi tukamdaka kama kuku wa kisasa
Akakiri kauziwa na mtu
Hatukutaka tabu tukachukua simu yetu tukasepa