Jinsi nilivyofilisika

Jinsi nilivyofilisika

siyumwe

Senior Member
Joined
Apr 10, 2017
Posts
152
Reaction score
134
Wahenga walisema mbuzi wa masikini hazai hata akizaa anazaa dume, ni msemo wa muda mrefu ila naamini unaishi,

Mwaka 2016 nilifanikiwa kumaliza kidato cha 6 ila matokeo yalivyotoka sikufanikiwa kuwa na pass mark za kunifanya niendelee mbele katika kipindi hiko nilihisi kuchanganyikiwa kwasababu nyumbani mimi ndio mkubwa na wazazi walikuwa wameweka mategemeo makubwa kwangu na kwakuwa nyumbani hata msosi ulikua wa kuunga unga hivyo sikuwa na option ya kuendele tena mbele kuhusu maswala ya elimu.

Kipindi bado niko shule nilipokuwa nikirud likizo kuna rafiki yangu alikua chuo kuna bidhaa X alikua anauza so baada ya yeye kuona sina ishu ya kufanya na kipindi hiko alikua yuko mwaka wa 3 aliniambia nikimbize ile biashara yeye kwa kipindi hiko alikua na mambo mengi ya kufanya akiwa chuoni hivyo asingeweza kuwafikia wateja kwa urahisi

Japo haikuwa rahisi ila nilikimbiza ile biashara kiasi cha kwamba ilikua kwa haraka na pale nyumbani mchango wangu ukawa unaonekana kwa 70% badae nikaja kupata wazo badala ya kwenda kununua hizo bidhaa X kwanini nisifanye production mwenyewe nikajaribu kufanya utafiti wa vifaa na kuanza kununua mdogo mdogo basic tools zote.

Wateja wangu kwa 97% nilikua nawapata online kipindi nawatafuta wateja nilipata kufahamiina na jamaa mmoja yeye alikua anatoka mkoa Y ambapo aliniambia yeye anaweza kuzitengeneza hizo bidhaa hivyo wakati nafikiria kuzalisha mwenyewe nilijua kuna mtu nitaungana nae mwisho wa siku alifanikiwa kuja Dar tukafanya kazi pamoja

Kazi ya uzalishaji haikuwa rahisi kama nilivyotarajia maana ilikua na changamoto nyingi na inabidi uwe smart sana kuweza kui manage upande wa production kuja usimamizi wa kazi mpaka unapokuja kuuza na mwisho wa siku uione faida yako baada ya kutoa matumizi yote, mtaji na kuweka faida pembeni nashukuru niliweza kumudu vizuri kwa muda wa miaka 2 biashara ikawa imekuwa kubwa pia nilikua nmeshaanza kupata wateja nje ya nchi kama INDIA, BRAZILI, USA, OMAN NK kwa nchi za Afrika nchi zote za SOUTHEN AFRICA(SA,BOTSWANA,NAMIBIA,ZIMBABWE,ZAMBIA) na nchi nyingine za hapa jirani

Mikosi ilipoanza

W
akati biashara ipo kwenye peak nilipata mteja mmoja aliyekua nchi Z alikua ni mtz ila makazi yake pamoja na biashara yake yalikua huko tulianza biashara vizuri na alikua mteja wangu wa nguvu sana kabla ya kuwa ananunua kwangu alikua anatoa Kenya hizo bidhaa ila alipoanza kwangu wateja wake walizipenda sana so speed ya jamaa kuagiza mzigo kwangu ilikua kubwa mpaka nikaamini huko kuna fursa kubwa ya kutoboa zaidi kwa biashara yangu ikabidi niongee na jamaa akakubali kuwa atanipokea

Kabla sijatoka huku kulikuwa na jamaa yangu ambae nilikuwa nafanya nae kazi nikampanga yeye abaki mimi nikifika kule nitacheki mazingira yakiwa mazuri mimi nirudi yeye aende ili tuwe tunakimbiza huku na kule jamaa alikubali ila kwakuwa hakuna anayejua kesho kumbe nilikua najichimbia shimo kubwa mbele yangu

Safari ikaanza ya kwenda kule miaka miwili iliyopita nikafika salama na nikapokelewa vizuri nilienda na bidhaa kidogo ili kuangalia mazingira yapoje, baada ya kufika nikaona kwa nature ya biashara ilivyo ili kujitofautisha na wengine siwezi kuuzia chini maana ntapunguza value ya bidhaa pia nikacheki nikaona kuna uwezekano wa kupata fremu bei ilikua 200USD kwa mwezi almost 460000 ya kitanzania na sio kubwa sana kulinganisha na huku kwetu za street ambapo huku unapata kwa 70K ambayo haipo center ila kwa kule ya ukubwa huo utapata kwa 500USD kwa mwezi na kwa nature ya biashara yangu kutoa 200USD sikuwaza maana nilijua nikiuza bidhaa 20 tu nmepata hela ya kodi na hizo naweza uza hata kwa mtu mmoja

Changamoto ilianza kuja baada ya jamaa niliyemuacha huku alikua anashindwa ku manage vizuri pia tulianza process ya kumtafutia passport huku ila mchakato ulikua mrefu sana hivyo mpaka muda wa mimi kurudi huku baada ya miez mi 3 ya kukaa kule ilikua bado hajapata, nilifanikiwa kurudi japo kwa njia za panya maana nilizidisha siku za kukaa kule hivyo ningerudi kihalali ingejua shida kwangu so nilipofika huku ikabi nirudishe ofisi kama mwanzo huku nikisubiri jamaa apate passport aende kule na kipindi chote hiko frem ilikua imefungwa na kodi ilikua inahesabiwa kama kawaida.

Mpaka mwaka unakaribia kuisha jamaa alikuwa hajapata passport na mimi kadri muda ulivyokua unazidi kwenda nilijua jamaa muda wa kupata passport unakaribia hivyo sikuwaza na kwakuwa sikukuu zilikua zinakaribia nika target soko la kule pia nili target ku clear makosa ya mwanzo maana soko la online hata ukiwa na bidhaa mbili unauza ila kwenye frem inahitaji uwe na mzigo mkubwa na upangilie vizuri ili mteja akipita mzigo umuite na umvutie kwa mpangilio wake

Nikaingiza 90% ya mtaji wangu wote nikiamini naenda kuuaga umasikini maana nchi niliyokua naenda ilikua ni center ya nchi nyingine za ukanda wa kusini na wengi wao walikua wanakauja kuchukua mizigo hapo baada ya kila kitu kukamilika nikatuma mzigo na mm nikafika nkapanga mzigo vizuri ila safari hii ofisi ya Dar niliifunga kwa muda ili jamaa akija kule nirudi kuifungua, nilivyofika ikabidi nilipe miezi niliyokuwa nadaiwa baada ya hapo nikaanza kuuza mwaka jana mwanzoni, jamaa kapata passport so ikabdi mi nirudi yeye aje huku ila hata nilipofika huku mambo hayakuwa kama nilivyotarajia maana jamaa alisema hatoweza kwenda daah ilinikata sana nikiwaza 90% ya mtaji upo kule nikiwaza niende kule maana nakuwa naua ofisi ya huku na nikisema nibaki huku pia naua ofisi ya kule

Kila option niliyofikiria ili niweze ku maintain ofisi zote mbili ilifeli ikabidi niongee na jamaa aliye nipokea mwanzo nikamuomba anitolee mzigo wote anitumie huku na nikamtumia hela ya usafirishaji ila mwisho wa siku mzigo haukutumwa na kipindi hiko corona ilikuwa ishaanza kuingia Tanzania na mipaka yote ikafungwa so option ya kutuma mzigo ikashindikana na huku biashara ikaanza kudorola ikafikia stage nikawa nakosa hata hela ya pango nikiongea na jamaa kuhusu mzigo ananipiga chenga nikamwambia uza nitumie hela anadai biashara hakuna ila badae kwenye uchunguzi wangu nikaja kugundua jamaa aliuza inshort ameniingiza kwenye mataa na huo ndo ukawa mwisho wa biashara yangu

Kipindi biashara inafanya vzuri nilikua naona fursa nyingi za kibiashara nilikua nashaangaa kuona kijana anashindwa vipi kupanga mtu anakosaje hela ya vocha n.k ila saiv maisha yamebadilika ss ndo nimejua mtu anashindaje njaa na anakosaje kazi ya kufanya maana imefikia hatua kula yang tu ya shida fursa zote sizioni naishi kwa mshikaji tu nayy anakaribia kunichoka yani kila nikiwaza hatma ya maisha yangu siion

Nipo hapa wakuu kama mtu anafursa ya kazi iwe kibarua au parmanent sichagui kazi pia ninauzoefu wa mambo ya online marketing kama mtu ana bidhaa zake na anahitaji kuongeza sales naweza kufanya kazi hiyo pia, nipo dar, umri miaka 25 jinsia ya kiume na nipo tayar kwenda kufanya kazi mkoa wowote ule
 
Hiyo bidhaa x ungeitaja tu,
Ndiyo itakuwa tahisizaidi kusaidika
Kwasababu tayari unauzoefu nayo
Nimeficha bidhaa na location kwasabab ya identity ila unaweza tafuta nyuzi zangu za nyuma niliitaja boss
 
yaaani mkuu mimi nitoke kwenye kujiajiri then niajiriwe ooooh shit camooon meen...mimi hiyo nerv aise
hata kama nimefilisika nilichoo gundua umejua kosaa jipange upyaaa chakata akiliiii kuna mahali tu kunatobo im sure
Kuna mda inabidi ukimbie vita ili ukajipange upya kesho urudi kupambana, sijakata tamaa ila kwanza nataka ni solve tatizo hata la kupata basic needs tu
 
Pole sana mpambanaji, haya ni maisha ambayo Watu Wengi wamekutana nayo, ila kama ni kweli uko karibu na mafanikio, usikate tamaa, tengeneza mtaji upia, na angalia biashara nyingine au hio hio ya kufanya, kwa ujuzi wako wa online marketing unaweza tengeneza pesa, pitia kwa Watu wenye maduka ya nguo na bizaa ambazo wanaweza uza online na jieleze jinsi unavyoweza wasaidia, pia kuna online company kama swahili media nk wanaweza kukupa kazi, wao wanaangalia ujuzi sio vyeti . ukipata hata sehemu ya kujitolea fanya, usinyamaze ongea na watu tembelea sehemu zenye watu wanaojishughulisha.
 
Mkuu pole sana ...ila nikushauri kitu njia bora ya kusaidiwa ni wewe kutoficha mambo muhimu .Mfano umesema kuna bidhaa ulikua unatengeneza hujataja jina la hiyo bidhaa kumbuka pengine kuna mtu anazo hizo bidhaa ila labda hana pa kuuzia au hajui kutengeneza ungeitaja ingekuja njia moja wapo ya kusaidiwa....

Kisa chako hakiko mbali mimi nilitapeliwa mwaka 2018 na jamaa nilimtrust ile mbaya kwa kushirikiana na mshikaji wangu, nilipoteza kila kitu almanusura nipoteze na nafasi ya elimu yangu..lakini M/Mungu alinitoa kule na leo alhamdulillah rizki napata nashukuru japo binadamu hariziki tunataka zaidi.
 
Mwanzo 3:18 -19 Michongoma na miiba itakuzalia, nawe utakula mboga za kondeni;
kwa jasho la uso wako utakula chakula, hata utakapoirudia ardhi, ambayo katika hiyo ulitwaliwa; kwa maana u mavumbi wewe, nawe mavumbini utarudi.

Ni kupambana mpak unashuka kaburini , no mecy ....inuka pambana , fight to death
 
Mkuu wewe ni MWANAUME! Hela ina formula Moja, NJIA YAKE NI ILEILE! Kama mto wa msimu vile, unaweza kukauka ila siku mvua ikinyesha maji yatapita njia ile ile tu!

Nakuombea mvua inyeshe tena kwako Mkuu.

Bad times don't last forever. There is always another door, keep fighting mdogo wangu.
 
Pole sana mpambanaji, haya ni maisha ambayo Watu Wengi wamekutana nayo, ila kama ni kweli uko karibu na mafanikio, usikate tamaa, tengeneza mtaji upia, na angalia biashara nyingine au hio hio ya kufanya, kwa ujuzi wako wa online marketing unaweza tengeneza pesa, pitia kwa Watu wenye maduka ya nguo na bizaa ambazo wanaweza uza online na jieleze jinsi unavyoweza wasaidia, pia kuna online company kama swahili media nk wanaweza kukupa kazi, wao wanaangalia ujuzi sio vyeti . ukipata hata sehemu ya kujitolea fanya, usinyamaze ongea na watu tembelea sehemu zenye watu wanaojishughulisha.
Shukran sana mkuu kwa mawazo yako chanya ngoja nifatilie hilo la swahili media,niliwaza kupita madukani lakin sio kila mtu anaweza akakaa chini asikilize historia yako ndo mana nmeisi pia kupitia platform hii naweza nikapata watu nitakao weza kufanya nao biashara
 
Back
Top Bottom