Jinsi Michael Jackson alivyoilipua sony music

Jinsi Michael Jackson alivyoilipua sony music

el nino

JF-Expert Member
Joined
Nov 5, 2013
Posts
4,712
Reaction score
5,064
MUZIKI ni biashara kubwa sana katika karne hii ya 21 ambapo tumeshuhudia vijana wadogo wakitajirika kwa namna ya ajabu. MUZIKI umefanikiwa kukamata nyanja mbali mbali za uchumi, kupitia biashara ya muziki vitu kama vinywaji, nguo na bidhaa nyingine zimekuwa zikiuzwa sana kutokana na kuwa promoted na muziki.

Biashara ya Muziki imeambatana na uongo na ujanjaujanja mwingi ambao watu wengi hawaufahamu kutokana na namna biashara hii inapambwa kupitia video za muziki, mitandao pamoja na vyombo vya habari.

Mnamo mwaka 2002, mwanamuziki mkongwe na Mfalme wa muziki wa Pop (marehemu)"Michael Joseph Jackson" aliwalipua vibaya kampuni ya Sony Music, Kampuni inayomsimamia katika shughuli za muziki. MJ aliielezea jinsi siri za Sony Music na fitna walizomfanyia kwa makusudi kabisa walikataa kupromote album yake iliyojulikana kwa jina la "invincible" kwa kuwa MJ alikataa katukatu kuzunguka kuipromote album hiyo (kufanya music tour USA) kwa sababu kuwa Sony walifanya fitna kuhakikisha MJ anapata masilahi madogo kutoka kwenye mauzo ya kazi zake kwa kushirikiana na wakili wa MJ walihakikisha vipengele vya mikataba vinamkaba MJ kinyume na matakwa yake.

MJ alilipua kwa kuweka bayana kuwa wasanii wengi wakubwa nchini marekani hufariki wakiwa na stress kutokana na ujanja na fitna zinazofanywa na Music Labels zinazowasimamia kiasi cha kuwaacha wasanii hao wakiwa maskini na wamefulia, inafahamika kwamba utofauti wa MJ na wasanii wengine wengi ni kuwa licha ya ubora wake katika muziki alikuwa bora sana kwenye biashara ya muziki hii ilipekea MJ mwanamuziki aliyefanikiwa zaidi kwenye biashara ya muziki kwa kulamba mikataba minono na kumiliki haki zake kwenye mikataba.

SONY MUSIC na makampuni mengine makubwa nchini USA hawakupenda namna Michael Jackson alikuwa akiwapiga chenga kwenye mikataba yao ya kinyonyaji kwa kuwa alikuwa ananufaika kushinda kampuni husika tofauti na wasanii wengine ambao ukiwaangalia kwenye video zao wanavyotumia mahela , pombe, magari na wanawake utahisi wanaingiza kiasi kikubwa cha fedha kumbe kiasi kikubwa kinachukuliwa na makampuni makubwa ya muziki ambayo yamejificha nyuma ya wasanii hao......

Namna pekee iliyobakia ilikuwa ni kuhakikisha MJ anashushwa kimuziki kwa gharama yeyote ile, kwa maana kwamba MJ akishuka kimuziki hatakuwa na uwezo wa kubargain wenye mikataba vilevile SONY MUSIC walikuwa wakifukuzia catalog( ni kama hatimiliki) ya kazi zote za MICHAEL JACKSON (CATALOG YA MJ ina thamani zaidi ya mwanamuziki yeyote aliyewahi kuishi chini ya jua)hivyo basi kupitia kufinance kashfa za uongo kama kubaka watoto, kuacha kupromote album zake na kuwekeza zaidi kwa wasanii wachanga ambao ni replica ya MJ SONY MUSIC walikuwa wapo mbioni kufanikisha adhma yao ovu.

Mpaka kufikia mwaka 2002, dunia ilikuwa imefichwa kilichokuwa kinafanyika nyuma ya pazia, kumbe muziki sio tuu biashara ambayo tunaiona ipo fair na inafanyika based on talent, kuna mambo mengi sana yapo nyuma ya biashara ya muziki na wasanii wengi ni watumwa wa haya makampuni ya kinyonyaji, angalia msanii mwenye talent kama chriss brown au drake, kwa uwezo na soko la kazi zao kiasi wanachoingiza ni kidogo sana tofauti na kinachokwapuliwa na haya makampuni, unaweza ukawaona wanaendesha ferrari na magari mengine ya kifahari lakini ujue kuwa kiasi kikubwa kinachukuliwa na makampuni na wakati mwingine vitu hivyo wanakopeshwa kwa kusaini mikataba ya maisha kuyatumikia makampuni haya.

Kimsingi muziki wa sasa huko USA haujali sana kipaji , bali ni nani yupo nyuma yako (kampuni ipi ipo nyuma yako), nadhani wote ni mashahidi kwenye gramy za mwaka huu 2019) tumeona ajabu la mwaka kwa cardy b kushinda best rap album wakati kimsingi album ya rap iliyopeform zaidi mwaka 2018 ni album ya drake ambayo haikuwemo kabisa kwenye hiyo category!!

Ili uweze kuendelea kuwa juu ni lazima ukubali kulaliwa na makampuni haya, huku kwetu Tz biashara ya muziki inakuwa kwa kasi, soon and very soon tutaanza kusikia vilio kutoka kwa wasanii wetu, kutokana na ujanja wa makampuni haya ambayo yanahakikisha yanamiliki haki zote za mwanamuziki kwa njia yeyote ile.
 

Attachments

  • michael-jackson-sony (1).jpg
    michael-jackson-sony (1).jpg
    46.7 KB · Views: 67
Duhh....
Mkuu, nimekuja mbio nikidhani WakoJacko alijifunga bomu kama Al-Qaida na kuilipua kampuni ya Sony wallah....
 
Upuuzi umeandika...kwanini?hao ndio waliomfanya huyo MJ kuwa milionea na kupata kiburi alichokuwa nacho

Kuinua vipaji vingine siyo kosa, kila jambo lina wakati wake, muda ukipita umepita braza hatuwezi kukaa kusubiria mpaka MJ afe ndio vipaji viibuliwe tukiogopa kuwa mj kipaji chake kinakufa

Evidence ya kwamba hawa ndio walioratibu kesi za MJ ziko wapi?

Sony nao ni wafanyabiashara lengo lao siyo kutoa msaada msanii anufaike bali wote wanufaike...watu wamewekeza na wanakula hasara vile vile faida inapokuja as long as uli sign mkataba hutakiwi kulalamika

Fungua kampuni yako wewe uwe fair tuone itakupeka wapi
 
Kuna mahali niliwahi kusikia, kuna watu waovu ambao huharibu wasanii kwa njia ya madawa ya kulevya, tazama baadhi ya wasanii hapa waliokuwa kweny peak na namnna walivyopotezwa kwa matumizi ya madawa, biashara ya mziki kwa hapa nyumbani ipo hivyo.
 
Umeandika vyema Sana..na Tanzania Kuna vilio vya kunyonywa na Ruge mutahaba

Sent using Jamii Forums mobile app

Hivi inakuaje mtu unalia umenyonywa, hao wasanii wanasaidiwa wakiwa hawana kitu, wanabebwa, effort kubwa inafanyika kuwapromote wanafanikiwa afu unataka huyo mtu afe njaa ama?

Ruge kasaidia wengi sana sema wanapoona its not enough anymore ndipo wanapoanza kelele
 
Upuuzi umeandika...kwanini?hao ndio waliomfanya huyo MJ kuwa milionea na kupata kiburi alichokuwa nacho

Kuinua vipaji vingine siyo kosa, kila jambo lina wakati wake, muda ukipita umepita braza hatuwezi kukaa kusubiria mpaka MJ afe ndio vipaji viibuliwe tukiogopa kuwa mj kipaji chake kinakufa

Evidence ya kwamba hawa ndio walioratibu kesi za MJ ziko wapi?

Sony nao ni wafanyabiashara lengo lao siyo kutoa msaada msanii anufaike bali wote wanufaike...watu wamewekeza na wanakula hasara vile vile faida inapokuja as long as uli sign mkataba hutakiwi kulalamika

Fungua kampuni yako wewe uwe fair tuone itakupeka wapi
We mjinga kama haujaelewa usikimbilie kucomment kwa dhihaka...

Cha kwanza naomba uelewe waliomjengea Michael Jackson uwezo kifedha sio Sony ... Sony wamesaini dili na Michael akiwa ametoka Motown na Epic records mahala ambapo alishaiprove Dunia uwezo wake na tayari alikuwa ameshabargain kwenye mikataba akawa ndio msanii mwenye mikataba bora zaidi...



Kufanya biashara sio kosa ni kufitini nadhani hujui hata kifo cha MJ kilisababishwa na nini na kwanini Daktari Conrad Murray alikutwa na hatia kwenye kifo chake..

Ukitaka kuelewa uliza kabla ya kuongea upumbavu wako
 
Hivi inakuaje mtu unalia umenyonywa, hao wasanii wanasaidiwa wakiwa hawana kitu, wanabebwa, effort kubwa inafanyika kuwapromote wanafanikiwa afu unataka huyo mtu afe njaa ama?

Ruge kasaidia wengi sana sema wanapoona its not enough anymore ndipo wanapoanza kelele

Mkuu hizi kampuni zinafanya zaidi ya kumsaidia , huwa zinaenda mbali kutaka kummiliki mtu na ukienda kinyume na mara kwa yao huwa zinakumaliza kabisa
 
[https://youtu.be/0mbpFqEkxG8/URL] ...nani alikuwa na the best deal at that time...
 
We mjinga kama haujaelewa usikimbilie kucomment kwa dhihaka...

Cha kwanza naomba uelewe waliomjengea Michael Jackson uwezo kifedha sio Sony ... Sony wamesaini dili na Michael akiwa ametoka Motown na Epic records mahala ambapo alishaiprove Dunia uwezo wake na tayari alikuwa ameshabargain kwenye mikataba akawa ndio msanii mwenye mikataba bora zaidi...



Kufanya biashara sio kosa ni kufitini nadhani hujui hata kifo cha MJ kilisababishwa na nini na kwanini Daktari Conrad Murray alikutwa na hatia kwenye kifo chake..

Ukitaka kuelewa uliza kabla ya kuongea upumbavu wako

We pimbi kweli, kama ame sign sony si aliona kuna maslahi?alishikiwa pistol akalazimishwa?

Usipende kuropoka based on hearsay, ukiulizwa ulete ushahidi utakimbilia kwenye article za za udaku za tmz, nia ya mfanyabiashara yeyote ni kupata faida na siyo kubembelezana usifanye mapenzi yako kwa MJ yakakupa upofu wa kuangalia upande wa pili

Uko biased sana...niambie wewe kifo cha MJ kilisababishwa na nini maana unaweza kuwa ndie daktari uliyemfanyia post mortem
 
Hivi. Akina Jay z na pdiddiy wamefanikiwaje kimziki maana wanaukaribia ubilionea

Sent using Jamii Forums mobile app

P diddy amefanikiwa kwa kuwa yeye hamilikiwi ila anamiliki wasanii kadhaa kupitia kampuni yake ya Bad Boys entertainment ..

Pia mafanikio ya Jay z yamewezekana kutokana na smart investments alizofanya nje ya muziki ... mfano kupitia kampuni yake ya Roc nation ameweza kumiliki wasanii wenye hits kama Rihanna n.k...

So wote hao ni smart investments walizofanya zinewabeba...

Tujiulize wasanii wenye hits na talented kama Chris brown, Rihanna na wengineo kwanini sio future billionaires kama kina Jay z
 
We pimbi kweli, kama ame sign sony si aliona kuna maslahi?alishikiwa pistol akalazimishwa?

Usipende kuropoka based on hearsay, ukiulizwa ulete ushahidi utakimbilia kwenye article za za udaku za tmz, nia ya mfanyabiashara yeyote ni kupata faida na siyo kubembelezana usifanye mapenzi yako kwa MJ yakakupa upofu wa kuangalia upande wa pili

Uko biased sana...niambie wewe kifo cha MJ kilisababishwa na nini maana unaweza kuwa ndie daktari uliyemfanyia post mortem


Cha kwanza... Akili yako ni ndogo sana kuweza kuelewa huu uzi.

Cha pili.... unajifanya mjuaji wakati huelewi chochote... akili ndogo sana kuendelea kutoa comment ukidhani unajua kumbe zero brain..



Cha tatu... source yangu ni maneno ya Mj mwenyewe ... kwa muda wako katafute speech yake kuhusu Sony akiielezea dunia ...

Cha nne.....Mj alikuwa akimiliki 50% ya Sony na issue sio kusaini mkataba kama wewe na upumbavu wako ulivyokurupuka hapa)

Issue ni misrepresentations kwenye mkataba wake na Sony iliyofanywa na attorney wake akishirikiana na Sony Music...


Cha tano... ukitaka ujue undani wa kifo cha MJ source ziko wazi kabisa zinaonyesha Uzembe uliofanya na D.k Conrad Murray mpaka akahukumiwa ...


Nenda kasome ushahidi uliotolewa na polisi ambapo ulichangia kumfunga Dk Murray utajua kabisa kuna watu walikuwa behind kifo chake...

Japo kichwa chako ni kigumu kama nazi utakuwa umeelewa kidogo... next time upunguze ujuaji
 
Back
Top Bottom