Allen Kilewella
JF-Expert Member
- Sep 30, 2011
- 25,138
- 48,364
CCM ni chama ambacho kimekuwa kinaua vipaji na ajira za watu kila uchwao na uchao.
Maelfu ya watanzania ajira zao au vipaji vyao vimeuawa na CCM ama kwa kuiunga mkono au kuipinga.
Nani anakumbuka zama zile za TMK wanaume na kundi la vichekesho la Zekomedi walipokuwa kama ndiyo alama ya sanaa Tanzania.
Hao jamaa waliposhiriki Kampeni za CCM mwaka 2010 ndiyo ukawa mwanzo wa kupoteza muelekeo. Hata msanii Marlaw aliwahi kusema kupotea kwake kimuziki kulitokana na yeye kuruhusu nyimbo zake kutumika na CCM kwenye Kampeni zao mwaka 2010.
Orodha ni ndefu lakini isemwe tu wasanii wengi wamepoteza wafuasi wao kisa walikubali kutumiwa na CCM kwa namna Moja ama nyingine.
Lakini vyombo vya habari Tanzania kwa Kasi ya ajabu vimepoteza watu wanaovifuatilia kwa kuwa watanzania wameamini hivyo vyombo vinatumiwa na CCM kama zana kuisadia kubaki madarakani.
Hizo ni ajira zinazouawa na CCM kisa yenyewe iendelee kubaki madarakani.
Maelfu ya watanzania ajira zao au vipaji vyao vimeuawa na CCM ama kwa kuiunga mkono au kuipinga.
Nani anakumbuka zama zile za TMK wanaume na kundi la vichekesho la Zekomedi walipokuwa kama ndiyo alama ya sanaa Tanzania.
Hao jamaa waliposhiriki Kampeni za CCM mwaka 2010 ndiyo ukawa mwanzo wa kupoteza muelekeo. Hata msanii Marlaw aliwahi kusema kupotea kwake kimuziki kulitokana na yeye kuruhusu nyimbo zake kutumika na CCM kwenye Kampeni zao mwaka 2010.
Orodha ni ndefu lakini isemwe tu wasanii wengi wamepoteza wafuasi wao kisa walikubali kutumiwa na CCM kwa namna Moja ama nyingine.
Lakini vyombo vya habari Tanzania kwa Kasi ya ajabu vimepoteza watu wanaovifuatilia kwa kuwa watanzania wameamini hivyo vyombo vinatumiwa na CCM kama zana kuisadia kubaki madarakani.
Hizo ni ajira zinazouawa na CCM kisa yenyewe iendelee kubaki madarakani.