Ozzie
JF-Expert Member
- Oct 9, 2007
- 3,217
- 1,266
Nina jamaa yangu kanipigia simu dakika chache zilizopita. Alikuwa ananiazima 315,000/=. Kama mkopeshaji nimemuuliza kwa utani unataka madafu ya kunywea beer? Kumbe nikamfanya jamaa afunguke na kuanza kunipa story za watu wanaojitambulisha wanatoka mtandao wa Lowassa. Ati Lowassa kanunua pikipiki nyingi aina ya Boxer kwa ajili ya kuwapa vijana maeneo fulani, buuuuureee. Kuna list ya majina ya watu wanaotakiwa kupewa, lakini baada ya kuchangia kiasi cha sh. 315,000/= ili kufidia gharama mbalimbali kama Bima na usafiri. Ati wamejisikia kumpa deal jamaa yangu kwa kuwa huyu rafiki aliwapa huduma nzuri sana walipomtembelea ofisini kwao (yeye mtumishi wa afya), na hivyo wako radhi kuondoa jina la mtu mwingine na kupachika jina lake.
Nikasema kaka pamoja na shule yako yoooteee wataka uwe ----- kwa watoto wa mjini? Huyo kashtuka... Utadhani alikuwa usingizini...
Nikasema kaka pamoja na shule yako yoooteee wataka uwe ----- kwa watoto wa mjini? Huyo kashtuka... Utadhani alikuwa usingizini...