Jihadhari na wizi wa mtandao simu: 0658-051817

Jihadhari na wizi wa mtandao simu: 0658-051817

CHITENGAY

New Member
Joined
Dec 3, 2012
Posts
4
Reaction score
2
Napenda kutoa tahadhari kuhusu wizi wa mtandao unaoendelea hapa mjini. Mmiliki wa simu yenye namba. 0658-051817 kwa jina la CHRISOSTOM MWABULANGA simu yake inatumika kwa kazi hiyo na ipo hewani. Kinachafanyika ni kwamba anao uwezo wa kutumia namba ya simu yako kuandika sms kwenda mtu mwingine akielekeza hela kutumwa kwake bila ya wewe kujua. Mfano ni sms hii. 'Samahani nipo kwenye kikao.Naomba unisaidie kumtumia hela mwenye namba hii 0658051817 Mr mwabulanga Tsh 300,000 nitakupatia nikitoka! nimebanwa sana! Nadhani elimu hii ipo juu anaweza kupata msaada kwa wataalam wa kampuni ya TIGO. Naomba TIGO wafuatilie akaunti ya tigo-pesa na watu wa usalama kwani huenda watu wengi wameibiwa pesa kwa utapeli huu. Pia uingiliaji wa mtandao wa watu wengine ni kosa la jinai.
 
Sijui ni mimi peke yangu ama!?
Maana sijaelewa kitu.
 
Sijui ni mimi peke yangu ama!?
Maana sijaelewa kitu.
Kwa lugha rahisi ni hivii?
yaani mwenye namba tajwa anauwezo wa kukutumia meseji lakini ikaonekana imetoka kwa baba yako mzazi.
Definitely kama una uwezo utamtumia baba angalau 10,000/=.
Lakini ki ukweli ukituma haiendi kwa baba yako inaenda kwa huyo jamaa.
anavaa 'musk'...sura bandia ......ni aina ya ku 'hack' mamtandao....ila ...zoezi hili kufanikiwa lazima 'system admin' wa kampuni atahusika.
 
Mbulula wewe ndo maana ujaelewa.nini sasa usichoelewa?mbona kila kitu kipo clear.eti na ww ni great thinker.aya ndo matokeo ya div 5 shame on u
Mkuu kuwa mpole, binadamu hutofautiana namna ya kuelewa jambo.
 
Mbulula wewe ndo maana ujaelewa.nini sasa usichoelewa?mbona kila kitu kipo clear.eti na ww ni great thinker.aya ndo matokeo ya div 5 shame on u

Koma kutukana Members wenzako, kwa kujifanya umuelewa sana! Ilhali wewe mwenyewe Kiswahili chako mwenyewe hujui kukiandika!
Maneno uloyaandika hapa kama "ujaelewa" correct ni "hujaelewa"
Neno "aya" ni "haya" then unazodoa watu! Gaa.dem.shit !
 
Ni hatari sana hii.

Jamaa wangu wa karibu alishanieleza hili sikuamini.
 
Asante mkuu kwa tahadhari hiyo. Nadhani hii mitandao ya simu inabidi wawe makini sana kulinda 'system' zao maana kila ya leo watu wanakuja na mbinu Mpya za wizi.

Narudia tena, shukrani sana mtoa mada. Ubarikiwe.
 
Nimesikia kuna DEO mmoja katapeliwa kwa mtindo huu baada ya kupata sms kutoka SLO wake kuwa ana shida ampe kama 300000 jamaa katuma hela kumbe wala huyo mtu hajaomba hela yoyote.
 
Nimesikia kuna DEO mmoja katapeliwa kwa mtindo huu baada ya kupata sms kutoka SLO wake kuwa ana shida ampe kama 300000 jamaa katuma hela kumbe wala huyo mtu hajaomba hela yoyote.

What is DEO and SLO?
 
Mleta mada iyo kitu ni kweli kabisa kuna MTU kaibiwa hapa Dom kwa MTU kutumia namba ya mwenzie...ila tgo huu mchezo nadhan wanaulea
 
Back
Top Bottom