Jifunze kitu hapa

Jifunze kitu hapa

Author

JF-Expert Member
Joined
Jan 24, 2014
Posts
1,745
Reaction score
8,222
KUNA MWALIMU MMOJA ALIINGIA DARASANI AKAANDIKA UBAONI KAMA IFUATAVYO:

(1) 9+1=70
(2) 9+2=11
(3) 9+3=12
(4) 9+4=13
(5) 9+5=14
(6) 9+6=15
(7) 9+7=16
(8) 9+8=17
(9) 9+9=18
(10) 9+10=19

Alipo maliza kuandika tu, akaona wanafunzi wote walikua wanacheka, kwasababu alikua amekosea swali la kwanza.

Akawatazama wanafunzi, kisha akawaambia yafuatayo:
```"Nimejikosesha lile swali la kwanza makusudi, kwasababu nilihitaji mjifunze kitu kimoja muhimu sana.Mnapaswa kujua namna ambavyo dunia inaweza kuwachukulia. Unaona hapo, nimeandika kwa usahihi maswali tisa (9), lakini hakuna kati yenu aliyenipongeza kwa hilo; wote mmecheka na kunilaumu kwasababu ya kosa moja tu nililofanya."```

#HIVYO, HILO NI SOMO KWENU:

```"Dunia haijali mazuri unayofanya hata ukiyafanya mara milioni, lakini fanya baya moja uone jinsi watakavyo kulaumu..."```

"```Hata hivyo usikate tamaa, MARA ZOTE SIMAMA IMARA NA USHINDE VIKWAZO VYOTE." ```

*Huu Ndio Ujumbe wangu kwenu leo.......

#TIMIZA MALENGO YAKO
 
Tatizo la kichaa anafanya makosa mengi kuliko mazuri, kwa hiyo anapaswa kudharauliwa na kila mtu
 
Back
Top Bottom