PreGE2025 Jiandikishe Upate Haki ya Kupiga Kura

PreGE2025 Jiandikishe Upate Haki ya Kupiga Kura

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)

isaac shonga

New Member
Joined
Nov 1, 2015
Posts
2
Reaction score
0
WAJIBU WAKO, SAUTI YAKO, HAKI YAKO!

Ndugu wananchi, demokrasia imara hujengwa na watu wanaotambua haki zao na kuzitumia kikamilifu. Moja ya haki yako muhimu kama raia ni KUPIGA KURA!

Ili kuhakikisha unashiriki katika maamuzi ya taifa letu, hakikisha unajiandikisha kwenye Daftari la Kudumu la Mpiga Kura.

Usikubali wengine wakuchagulie viongozi bila sauti yako!

Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

Jiandikishe ili uwe na uwezo wa kuchagua viongozi bora na wenye maslahi ya wananchi!

Kura yako ni silaha yako ya mabadiliko!

Hakuna maendeleo bila ushiriki wako! Jiandikishe, shiriki, badilisha!

#JiandikisheSasa
#SautiYakoMaamuziYako
#DemokrasiaNiWajibu
 
Kujiandikisha na kupiga kura siyo big issue hata kidogo. Tunaweza kufanya hivyo. Ila ungetuambia baada ya kupiga kura, ni nani mwenye mamlaka ya kumtangaza mshindi halali aliyechaguliwa na wapiga kura?

1. Ni DED aliyeteuliwa na mgombea wa chama tawala, au ni kiongozi kutoka Tume Huru ya uchaguzi na ambaye mamlaka yake hayaingiliwi na chombo kingine?

2. Matokeo ya Urais yanatangazwa na nani? Mwenyekiti wa Tume inayoitwa Tume huru ya uchaguzi, na anayeteuliwa na mgombea wa chama tawala, au yatatangazwa na Mwenyekiti wa Tume huru kweli ya uchaguzi, na aliyepatikana kupitia mchakato wa wazi wa kuomba hiyo nafasi; na asiyeingiliwa majukumu yake na mgombea wa chama tawala?

3. Je, kama kutakuwa na dosari kwenye uchaguzi, wagombea wanaruhusiwa kuweka mapingamizi yao mahakamani ilo kuzuia mshindi kutanhazwa mpaka pale haki itakapo patikana?

4. Je, kwenye uchaguzi wa mwaka huu wagombea wa vyama vya upinzani hawataondolewa kwa hila na kwa sababu za rushwa, na zile za kipuuzi mfano kukosea kujaza fomu, nk, ili tu wagombea wa chama tawala wapite bila ya kupingwa?

Ukinijibu haya maswali yangu, nitajiandikisha mara moja ili kushiriki huo uchaguzi. Kinyume na hapo, utanisamehe kwa kweli. Maana siyo wananchi wote hatuna akili ya kufikiria.
 
WAJIBU WAKO, SAUTI YAKO, HAKI YAKO!

Ndugu wananchi, demokrasia imara hujengwa na watu wanaotambua haki zao na kuzitumia kikamilifu. Moja ya haki yako muhimu kama raia ni KUPIGA KURA!

Ili kuhakikisha unashiriki katika maamuzi ya taifa letu, hakikisha unajiandikisha kwenye Daftari la Kudumu la Mpiga Kura.

Usikubali wengine wakuchagulie viongozi bila sauti yako!

Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

Jiandikishe ili uwe na uwezo wa kuchagua viongozi bora na wenye maslahi ya wananchi!

Kura yako ni silaha yako ya mabadiliko!

Hakuna maendeleo bila ushiriki wako! Jiandikishe, shiriki, badilisha!

#JiandikisheSasa
#SautiYakoMaamuziYako
#DemokrasiaNiWajibu
Kwa sasa chaguzi za Tanzania sio zinazoamua kiongozi, bali genge la ccm ndio hupanga nani awe kiongozi.
 
Wengine wanajiandikisha wapate kitambulisho cha kuwasaidia kupata huduma za jamii wakati wanasubiri Kupata vitambulisho vya Taifa.
 
Jiandikishe kwa wingi ili upate kitambulisho tu.
 
Back
Top Bottom