JF vs FACEBOOK

Kwa kifupi FB haiwezi kulingana na JF hata kidogo mimi nina account kwenye fb lakini comment unazozikuta au post ni za kitoto zimekaakaa kingono ngono tu vijana watongozane yaani hamna cha maana nimeamua kutulia na JF yangu maana ninajaza maarifa ya kutosha na burudani pia mimi nainjoi kuwa JF kuliko FB. Nitarudi baadae kidogo
 
hapahapa jf nimepona ugonjwa ulionisumbua,kumbe ilikua ishu ya psychologia..viva jf siwezi kuwasaau wachangiaji nyote.mbarikiwe.
 
Kiukweli kwa upande wangu mimi facebook ni upuuzi mtupu na inapoteza mda sana... Nimekuwa facebook kwa miaka mingi sana lakini nilikuja kuona baadae kuwa nilikuwa napoteza mudawangu bila kunufaika na chochote lakini baada ya kuingia JF nimekutana na elimu na changamoto nyingi za kuelimisha ambazo zimenisaidia sana katika maisha hadi nikajiuliza nilikuwa wapi siku zote hizo nikipoteza mda Facebook.@!!!!
 
kwangu mimi naona hao rafiki zako wapo sahihi ila wewe upo sahihi zaidi yao, why? binadamu anatabia ya kuamini chake ni bora kuliko cha mwingune hata kama alichonacho yeye si bora kama cha mwenzake. Hata wewe naamini kabla hujajiunga na jf, fb uliona ni bora zaidi but now, cause you know what does jf mean, nadhani huna sababu ya kuwalaumu but take time to educate them nadhani watakuelewa.
 
Hapo ni sawa unashindanisha, New york (JF) vs Tandale (facebook)
 

Facebook hakuna 'ban' kutoka kwa mods, ila unaweza kuwa mod mwenyewe. Sasa ukikubali kuwa na marafiki wa 'ovyo' huko FB na ukashidwa kuwapiga ban usilalamike.

JF kuna kuheshimiana, ukikurupuka na hoja za ajabu ajabu tu huku unapata kibano cha JF members, ukilazimisha kuota mapembe Mods wanakutandika 'ban'.

Hivyo , JF > FB (katika maeneo mengi).
 
Ukitaka upate watu wa kucoment ktk statuz zako za facebook basi andika upuuzi wa kingono. But ukiandika ishu za msingi hakuna atakayechangia. Jamii Forum is the best. Imenifungua mengi hasa kisiasa
 

Hapo kwenye red sijaelewa vizuri, Ambilikile maana yake mshamba??!!, kama ndiyo hivyo waambie watuombe radhi wanyakyusa, neno ambilikile lina maana kubwa sana kwetu.......%&(#$%^ maanina zao.
 
nilijifuta fb lakini ilinibidi kujiunga tena kwa kuwa nilihitaji kampuni yangu kuwepo humo. Na huwezi kuwa na page fb bila kuwa memba
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…