JF diaries

"Tukikubaliana na haya yanayoendelea yanayopelekea kwenda kuharibu amani ya nchi yetu tutakuja kujuta watanzania, kwasababu tangu wazee wetu wametengeneza amani kwenye nchi hii na kuruhusu uwepo wa vyama vya siasa tulikuwa vizuri na amani tele ila hizi chaguzi tatu za 2015, 2020, 2025 kumekua na mambo ya hovyo yanayojitokeza ambayo hayaonyeshi Tanzania kubaki salama...

...tujiulize kwanini kila tunapokaribia kwenye uchaguzi mkuu haya hujitokeza, mfano tulipokaribia uchaguzi wa 2015 yalijitokeza mambo ya hovyo kabisa, uchaguzi wa 2020 yakatokea tena mambo hayo ya hovyo na safari hii tena yanajitokeza, je ni nani anafanya hayo! kila mtu aende akatafakari hilo tukijua muhimu ni usalama wa nchi" Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akizungumza wakati akiweka jiwe la msingi kwenye jengo la TBS Jijini Dodoma June 04, 2025.
 
Hii pia inafaa kuingia kwenye hansard za JF
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…