mwehu ndama
JF-Expert Member
- Nov 12, 2019
- 543
- 1,875
Nimemfuatilia kwa umakini mkubwa winga huyu wa kikongo kwa msimu huu mpaka sasa, na baada ya kumtazama katika mechi ya Leo dhidi ya mtibwa ni wazi jesus moloko hana kitu kingine anachoweza kutoa kama msaada kwa timu yetu, ni winga wa kizamani mwenye uwezo mdogo wa kufanya maamuzi, na hata anapotakiwa kuisukuma timu mbele anashindwa, kwa kifupi muda wake ndani ya Yanga sc umefikia tamati na nitashangaa sana ikiwa mbabaishaji huyu ataendelea kuwa miongoni mwa wachezaji wetu baada ya DIRISHA hili dogo la usajili