Jeshi la polisi lajiweka njia panda

Jeshi la polisi lajiweka njia panda

KALOKAZA

Member
Joined
Jan 3, 2013
Posts
95
Reaction score
135
Jeshi la Polisi nchini, limejiweka njia panda, kufuatia taarifa yake kwa vyombo vya habari kukanusha habari iliyoandikwa na gazeti la Mtanzania toleo namba 7235 la Alhamisi 21.02.2013, yenye kichwa cha habri ‘WATUHUMIWA WA MAUAJI YA PADRE WAKAMATWA KENYA”. Kwa mujibu wa taarifa hiyo ni kuwa habari hiyo ni ya Uongo.
Maswali ya Msingi. [Habari zote zinahusu habari isiyo ya kweli dhidi ya polisi]

  1. Je Mwandishi wa habari hiyo wa Mtanzania atatafutwa na kupekuliwa chumba kama yule wa Tanzania Daima aliyeandika habari na baadaye kuomba radhi?

  1. Je Mhariri wa Mtanzania na Mwandishi wake watahojiwa kwa masaa zaidi ya sita, na kutolewa kwa dhamana Kama walivyohojiwa Mhariri na Mwandishi wa Tanzania Daima?

  1. Je Mhariri Mtendaji wa Mtanzania, na Mmiliki wa Gazeti hilo, na Mchapishaji watatafutwa kama wanavyotafutwa Mhariri Mtendaji wa Tanzania Daima, Mmiliki wa Gazeti na Mchapishaji ili wasaidie Polisi?

  1. Je Mtanzania litatishiwa kufungwa na Rais kama si huyu basi ni ajaye?

  1. Je Taaluma ya Mmiliki wa Gazeti la Mtanzania (Mfanyabiashara) itahojiwa kwanini anamiliki gazeti, kama walivyohoji Mmiliki wa Tanzania Daima kuwa Daktari lakini anamiliki gazeti?.
Mjadala ndugu wana JF.
 

Attachments

  • BARUA YA POLISI.jpg
    BARUA YA POLISI.jpg
    259 KB · Views: 313
Ungetusaidia zaidi wale ambao hatukupata kuisoma habari kutoka gazeti la Mtanzania kama ungeiweka hapa nasi tukaweza kuisoma ili kupata picha kwa mapana kuhusu maudhui ya habari yenyewe iliyopelekea polisi kukanusha na bila kuchukua hatua za kisheria.
 
Ungetusaidia zaidi wale ambao hatukupata kuisoma habari kutoka gazeti la Mtanzania kama ungeiweka hapa nasi tukaweza kuisoma ili kupata picha kwa mapana kuhusu maudhui ya habari yenyewe iliyopelekea polisi kukanusha na bila kuchukua hatua za kisheria.

Habari nzima ipo hapa JF kama ilivyoandikwa gazetini.
 
Ungetusaidia zaidi wale ambao hatukupata kuisoma habari kutoka gazeti la Mtanzania kama ungeiweka hapa nasi tukaweza kuisoma ili kupata picha kwa mapana kuhusu maudhui ya habari yenyewe iliyopelekea polisi kukanusha na bila kuchukua hatua za kisheria.
Kweli ukipenda chongo utaita mtoto wa jicho na pengo utasema mwanya. ina maana hujawahi kuisikiliza redio Imaan wewe?
 
Jeshi la Polisi lageuka kituo cha Sanaa.....hahahaaaaa natamani nije kuona Bango lao limeandikwa Kituo Cha Polisi-Sanaa - Central
 
Hakuna jeshi la polisi tz kwa maana halisi ya polisi,kuna genge la wahuni ambao hutumika kama mkono wa kulinda maslahi na matakwa ya wahuni nguli i.e. viongozi wa serikali kuu,si unajua mkono hauna akili za kwake,ndivyo walivyo hawa jamaa.
 
Pamoja na kadhia ya polisi,lakini ni vema tutakangalia pia utendaji au mtazamo wa waziri wa Habari na Michezo Dr Fenella Mukangala kwa tasnia nzima ya habari. Tangu ashike usukani, Mwanahalisi limefungiwa, Daudi Mwangisi kauliwa, na sasa Mhariri wa Tanzania Daima anapambana na polisi.

Kwenye hili la Tanzania Daima tunaambiwa ni kwasababu ya uchochezi, lakini inakuwaje gezeti kam Al-nuur lipo, au radio Imaan. Sijui waziri huyu msomi anatumia viwango gani kukagua vyombo vya habari?
 
Kweli ukipenda chongo utaita mtoto wa jicho na pengo utasema mwanya. ina maana hujawahi kuisikiliza redio Imaan wewe?

Mkuu,
Sijawahi kuisikiliza na haipatikani kwenye internet kwa sisi tusiokuwa nchini. Radio nyingi za Tanzania zinapatikana kwenye Tunein Radio ndani ya internet lakini kwa hii haipo
 
Kwa mwendo huu ambapo jeshi la Polisi limeshindwa wajibu wake no. 1 wa kuwalinda raia na mali zao, ambapo hivi sasa kila kukicha raia wasio na hatia wanauawa holela, itakuwa jambo la busara mno kama uongozi wa juu wa Polisi utaamua kujiuzuru wenyewe kwa hiari yao wenyewe!!
 
Huyu naye hujawahi kumskia? na hajawahi hata kuhojiwa na Polisi.





SHEIKH ILUNGA: Wauweni Maaskofu na Mapadre
www.youtube.comSheikh Ilunga Hassan akiwahamasisha Waislam kuwauwa Maaskofu na Mapadre.

Duh, hii falsafa yake ngumu kuielewa na kama alichokuwa anakisema ndivyo hivyo bila kuwa na maana nyingine zaidi ya hicho, basi huyu jamaa hata kwa nchi zilizo na wigo mpana katika demokrasia angekuwa yuko mikononi mwa dola.

Waingereza kwa kutaka kukabiliana na watu wenye mawazo kama ya huyu jamaa walikuja na act under section 4 of Terrorist Act na Offences against the Person Act 1861 ili kuiboresha zaidi.

This offence is created by section 4 of the Offences against the Person Act 1861 which reads:
. . . whosoever shall solicit, encourage, persuade, or endeavour to persuade, or shall propose to any person, to murder any other person, whether he be a subject of Her Majesty or not, and whether he be within the Queen’s dominions or not, shall be guilty of a misdemeanor, and being convicted thereof shall be liable . . . to [imprisonment for life] . . .

Kweli Tanzania kwa sasa uhuru wa kuongea umepata watu.
 
Pamoja na kadhia ya
polisi,lakini ni vema tutakangalia pia utendaji au mtazamo wa waziri wa
Habari na Michezo Dr Fenella Mukangala kwa tasnia nzima ya habari. Tangu
ashike usukani, Mwanahalisi limefungiwa, Daudi Mwangisi kauliwa, na
sasa Mhariri wa Tanzania Daima anapambana na polisi.

Kwenye hili la Tanzania Daima tunaambiwa ni kwasababu ya uchochezi,
lakini inakuwaje gezeti kam Al-nuur lipo, au radio Imaan. Sijui waziri
huyu msomi anatumia viwango gani kukagua vyombo vya habari?

Mkuu kwenye swala la 'usomi' la huyu waziri utakuwa unakosea kidogo. Inawezekana elimu yake ikiwa kama ya Nape. Namaanisha ya kuwa failure form 4 alafu baada ya miaka 5 au 6 unasikia ana Masters, kaipataje, anajua yeye na 'baba yake'....
Hivi kesho kutwa ukisikia nape ana PhD si utashaangaa.... Sasa, hiyo elimu ya Mukangala ni kama ya Nape.
Tunaongozwa na failure, waliopitia na kuzoea maisha ya short cut, ndio maana hawana uchungu na nchi hii....
 
Hapa KOSA kwa Jeshi la polisi ni KUKANUSHA TAARIFA ZA UONGO ZA GAZETI LA TANZANIA DAIMA? Wa kulaumu ni huyo MWANDISHI UCHWARA yeye kazipata hizo hbr wapi? POLISI WAPO RIGHT KUKANUSHA UONGO. "Hakuna NJIA PANDA hapa LABDA NJIA SHUKA!!!:bange:
 
Inawezekana hawa jamaa wamekamatwa lakini labda kuna makachero wa nchi za magharibi wanataka kuwahoji zaidi kwa kuwasafirisha kama walivyokuwa wanafanya kwa raia wa nchi za mashariki ya mbali (secret rendition) ili kupata habari zaidi za kijasusi. Kwa hiyo polisi wanataka kufunika kombe kwanza.

Anything is possible, kwa maana hiyo, hawataki kurumbana na gazeti la Mtanzania.
 
Mkuu,
Sijawahi kuisikiliza na haipatikani kwenye internet kwa sisi tusiokuwa nchini. Radio nyingi za Tanzania zinapatikana kwenye Tunein Radio ndani ya internet lakini kwa hii haipo

hawana utaalamu huo wa tunein
 
Back
Top Bottom