Jerry Silaa atangaza kugombea Ubunge Ukonga

Jerry Silaa atangaza kugombea Ubunge Ukonga

Duh,msimu mwingine wa watanzania kudanganywa unakaribia! Ili wapewe ubunge wakifika bungeni wakitumikie chama badala ya umma..
 
Meya wa Ilala Jerry Silaa ametangaza nia ya kugombea Ubunge Jimbo la Ukonga Katika uchaguzi mkuu ujao.

Meya huyo ametangaza nia hiyo huku Jimbo la Ukonga likiwa jimbo linaloongoza kwa miundombinu mibovu ya barabara kiasi kwamba nauli ya daladala inafikia hadi 1000/-

Kwa sasa Jerry Silaa ni meya wa Ilala ambapo Jimbo la Ukonga liko chini yake na hatua mbalimbali za wananchi kulalamikia ubovu wa barabara hizo hazijafua dafu.

CCM imepoteza udhibiti wake katika maeneo mengi ya Ukonga kwa Chadema ambapo miaka ya nyuma ilikuwa ngome kuu ya chama hicho tawala.

Source:Mwananchi

Muulize yeye kama Meya ambaye ndiye msimamizi mkuu wa budget ya wilaya na miradi ikiwemo miundombinu amefanya nini kuondoa tatzo la miundombinu Ukonga...
 
Ni jambo la kuvutia na ukomavu wa kisiasa mfuasi wa Chadema kumpigia debe mfuasi wa CCM.
 
Afadhali mara dufu huyu aliyopo kuliko fisadi silaa amefilisi manispaa ya ilala iliyokuwa inaongoza kwa mapato na sasa ni ya mwisho. Mwaka jana ilitangazwa kuwa imefilisika hadi CAG akaleta wakaguzi. Na jerry slaa ana kesi ya mauaji aliyowekewa dhamana na mengi.
Kata yake ina miundombinu mbovu na uchafu umelundikana kila mahali. Hajawahi kuufanya mkutano wala kurudi kwa wananchi. Huyu fisadi hafai jamani
 
jery yupo fit anaweza kama atapitia CCM na sio CDM maana ukonga Wachaga si wengi na Wakurya waliopo hawana uwezo wa kumchagua Mbunge kupitia CDM maana kufanya hilo ni sawa na kulazimisha kivuli cha Mzungu kuwa cheupe.
 
Huyu aliyeshindwa kusimamia hata usafi tu ataweza nini? Kajamaa kachafu kuanzia nyumbani hadi ofisini!
 
jery yupo fit anaweza kama atapitia CCM na sio CDM maana ukonga Wachaga si wengi na Wakurya waliopo hawana uwezo wa kumchagua Mbunge kupitia CDM maana kufanya hilo ni sawa na kulazimisha kivuli cha Mzungu kuwa cheupe.
mkuu haka kajamaa hakafai, hata kupitia ccm, naamini ccm inao watu wazuri zaidi ya huyu anaye ishi na uchafu
 
jery yupo fit anaweza kama atapitia CCM na sio CDM maana ukonga Wachaga si wengi na Wakurya waliopo hawana uwezo wa kumchagua Mbunge kupitia CDM maana kufanya hilo ni sawa na kulazimisha kivuli cha Mzungu kuwa cheupe.

Wapumbavu utawajua kwa watakachoandika!
 
jery yupo fit anaweza kama atapitia CCM na sio CDM maana ukonga Wachaga si wengi na Wakurya waliopo hawana uwezo wa kumchagua Mbunge kupitia CDM maana kufanya hilo ni sawa na kulazimisha kivuli cha Mzungu kuwa cheupe.
teh teh, kwa hiyo ccm ni chama cha makabila yepi? Duh kazi ipo tanzania!
 
Back
Top Bottom