Je, aachwe aseme tu, By "Taking The Bitter With The Sweet", Or Atumie Busara?

kama kulopoka ni tabia yake, hata wakimuandikia hatasoma hatasoma,maana atatamani kuendelea na tabia yake ileile.

kama unategemea ushauri kwa kua mwenzie ni mwalimu heti kasoma somo la saikokiji,basi pale ndio penyewe, maana wote ni walimu, na akijichanganya anachezea vitasa.

yaani hapo hatuna jinsi, tuvumilie tu pasco.
 
kama kulopoka ni tabia yake, hata wakimuandikia hatasoma hatasoma,maana atatamani kuendelea na tabia yake ileile.

kama unategemea ushauri kwa kua mwenzie ni mwalimu heti kasoma somo la saikokiji,basi pale ndio penyewe, maana wote ni walimu, na akijichanganya anachezea vitasa.

yaani hapo hatuna jinsi, tuvumilie tu pasco.
Story zingine mnatuvunja mbavu sana.
 
Asiyekuwa na 200 ya kuvukia pantoni na apige mbizi. By Unknown.

Mwaka 2020 kura za kishindo za ccm zitatokea kwa Wahaya, mark my word.
Ukiwa unaongea na wewe uatakiwa kuzingatia matumizi ya lugha sahihi kama huyu tunayemsema hapa. Katika maongezi muhimu ya namna hii usipende kutumia kauli za jumla kama huna huo uhakika wa unachokiongea. Kagera ni ethinical region, ni mchanganyiko wa watu wa rangi, dini na makabila tofauti kuliko unavyo narrow down eneo lile. Lakini pia ni uhakika gani unao kwamba ni wahaya tu na ni wote watakwenda kumpigia kura 2020?? Usitufanye tuhame mada bure kwa ajiri yako mkuu. Nadhani umeelewa.
 
"Ni mlevi tu huropika na kusema ukweli" E.Kezilahabi.
So watu wengine wanaweza kuropoka lakini vitu visivyo vya kweli bali kutafuta attention tu.
 
Mode naomba usaidizi wako kwenye heading iwe


Jee Aachwe Aropoke Tuu, By "Taking The Bitter With The Sweet", Or TuInject Busara Ndani Yake?!.

Paskali
Umekasirika! mie naona aachwe maana kigezo kwa wale wanaomtetea ni kuwa mbona akiropoka wananchi wanashangilia? Mwalimu mmoja alienifundisha uandishi wa wa habari alisema Watanzania wanapenda mambo ya hovyohovyo ndio maana magazeti ya udaku yanauza kuliko yenye mambo ya maana.
 
Wanabodi.
Hii ni thread ya swali "
Jee Aachwe Tuu Aendelee Kuropoka kwa sababu ndio "Taking The Bitter With The Sweet", au Tu Inject Busara Ndani ya Kichwa Chake ili achague maneno ya kuongea nini na wapi?!.

Declaration of interest. "Mimi Paskali ni mropokaji, ila kwa nafasi yangu ni ruksa kuwa mropokaji ila kuna positions huwezi kuwa mropokaji.
NB. Uropokakaji sio kutukana ni neno linalomaanisha kuongea maneno ya hovyo hovyo bila kujali the consequences of matamshi yako.
Angalizo.
Naomba kuanza na angalizo.
Simple Mind Discuss People.
Ordinary Mind Discuss Events
Great Mind Discuss Ideas.

Hii ni thread kuhusu ideas, naomba sana tusitaje jina la mtu yoyote kwa sababu hatujadili mtu bali tunahadili matumizi ya kutumia busara kuchagua kwa makini maneno ya kutumia katika kuongea, unaongea nini, wapi, na nani hivyo uchague maneno gani ya kuongea wapi ili kufikisha ujumbe husika.

Mropokaji ni Nani? .
Mtu anayeongea lolote popote, bila kujali anaongea nini na nani na huvyo atumie maneno gani, huyu ni mropokaji.

Jee ikitokea watu tukabahatika kumpata mtu safi mwenye uwezo wa kunyoosha kila palipopinda, na mwenye nía njema na dhamira safi lakini ni mropokaji, tumuache tuu aendelee kuropoka au tumsaidie ili apunguze uropokaji? .

Jee tumuache tuu aendelee kuropoka simply because he is the best on what he does, au tumsaidie afundishwe namna ya kuchagua maneno gani azungumze wapi na nani ili kufikisha ujumbe sahihi na ndio maana taifa linagharimia watu mahirI kwa jina la speech writers ili wamuandikie nini cha kusema wapi, sasa hawa watu wanafanya nini?.

Au kwa vile dawa chungu ndio iponyeshayo ugonjwa, Tanzania kama taifa lazima tukiri tunaugonjwa, amepatikana daktari bingwa wa kutibu ugonjwa wetu ila dawa zake chungu kwa kudunga sindano zenye maumivu makali, kutoa vidonge vichungu kumesa na hata kutumbua majipu bila ganzi, tatizo pía ni mropokaji!, hivyo tuuchukulie huo uropokaji ndio tamu ya chungu ya dose yake, tuvumilie tuu, tumeze tupone? .

Sasa ili tupone, do we have to take the bitter with the sweet!, or to choose to take only the sweet na kumeza lakini the bitter tuteme? . Ule msemo wa wape wape vidonge vyao, una apply hapa, jee hivi ndio vidonge vyenyewe tunavyotakiwa kumeza au kutema ni shauri yetu au Tanzania ni yetu sote hivyo tunajukumu kusaidia? .

JF Has A Duty!.
JF we have a duty of care to help out this situation kwa kusema the right thing to do and how to go about it.

Atafutiwe Waalimu! .
Jee watafutiwe waalimu wa somo la busara kujaribu kuingiza busara japo kidogo ndani ya kichwa cha mtu huyu ili atumie kwenye matamshi yake, au tuendelee tuu kumuacha akiropoka huku anashangiliwa na umati wa watu ilihali anaidhalilisha taasisi ile takatifu?.

Nani wa Kumfundisha na kumsaidia?.
Mwanzo wa mwaka nilishauri humu, jf tukiona tatizo mahali tusiishie tuu kutaja tatizo ili tuu watu wajue kuna tatizo, bali tupendekeze na njia za utatuzi.

Kwa tatizo hili la uropokakaji tumpatie waalimu watatu.
1. Yule Mama Anayemmudu.
Huyu mama ni mwalimu na saikolojia ya Kufundishia anaijua, bahati nzuri imetokea she is so humble and down to earth. Katakana na majukumu mapya, ameacha ualimu. Tumuombe andelee na ualimu wake kwa kufungua darasa kwenye kile chumba na kila wakati muafaka baada ya majukumu muafaka ampige somo la yule mwanafunzi mkubwa anayemmudu. Japo huku mtaani anatajwa kuwa ni mbishi, lakini hakuna kiumbe chochote kinachoweza kuleta ubishi kwenye yale, hivyo somo la busara litamuingia.

2. Yule Mama Msaidizi.
Hapa ni kujifunza kwa mifano, mbona mama Msaidizi wake anazungumza kwa heshima, kwa busara na kwa unyenyekevu wa hali ya juu. Wewe Mama Msaidizi, haijalishi unamuogopa vipi bosi wako, kuliko kumuacha aidhalilishe hiyo taasisi aliyopo, kama hauwezi Kumsaidia bosi wako achague maneno ya kuzungumza wapi na nani, unakuwa huna msaada wowote kwake zaidi ya kutumwa kumwakilisha, ukiona kuna maeneo anakosea, mbishie hodi uzungumze nae nyinyi wawili tuu peke yenu, maana kuna watu wakiwekwa kwenye kona, pamba za masikio zinafumka na busara inawaingia.
3. Kwenye Vile Vikao Vyenu.
Kwa vile kila kinachozungumzwa kwenye vile vikao Vyenu ni siri, then ninaamini kuna mijitu mibold mule inaweza kumkabili na kumsaidia, msikubali mfalme aadhirike kwa kauli za uropokakaji, mna jukumu la kumstahi ili kumsaidia, hiyo taasisi ni tukufu, na hapo mahali patakatifu hivyo yampasa mmiliki kuwa mtakatifu na atoe matamshi ya kitakatifu yenye utukufu ndani yake. Mtakatifu hauwezi kuwa mropokaji.

Mungu Ibariki Tanzania.

Paskali.
Kumwambia mkubwa wako anaropoka ni matusi tena matusi sana...
Kumwambia Rais anaropoka ni kosa na ni matusi kabisa..
Sasa naona na wewe umeanza kutafuta kiki baada ya kusifiwa kule kwenye mkutano na waandishi wa habari sasa umeanza kuvuka mipaka....halafu unawaambia watu wasi jadili watu lakini wewe una mtukana Rais wa nchi kiasi hiki halafu unasema anaongea maneno ya hovyo hovyo....acha kutafuta umaatrufu kila mtu ana fahamu wewe ni muandishi wa habari sasa sijui unatafuta kiki za nini zaidi?
Huna adabu
 
Haka kajamaa hakana mpango wa kugombea 2020, kanataka kamalize miaka mitano.....kuna kipisi fulani cha video alisema "nikiwa raisi watanzania watalimia meno" alikuwa na maana kubwa sana ndio haya tuyaonayo sasa....lakini kumbuka huwezi kumfunza simba mzee njia mpya za kuwinda...ni ngumu sana kumbadili
 
Kumwambia mkubwa wako anaropoka ni matusi tena matusi sana...
Kumwambia Rais anaropoka ni kosa na ni matusi kabisa..
Sasa naona na wewe umeanza kutafuta kiki baada ya kusifiwa kule kwenye mkutano na waandishi wa habari sasa umeanza kuvuka mipaka....halafu unawaambia watu wasi jadili watu lakini wewe una mtukana Rais wa nchi kiasi hiki halafu unasema anaongea maneno ya hovyo hovyo....acha kutafuta umaatrufu kila mtu ana fahamu wewe ni muandishi wa habari sasa sijui unatafuta kiki za nini zaidi?
Huna adabu
Hakuna sehemu Paschal ametaja jina la mtu ama cheo mkuu
 
kama kulopoka ni tabia yake, hata wakimuandikia hatasoma hatasoma,maana atatamani kuendelea na tabia yake ileile.

kama unategemea ushauri kwa kua mwenzie ni mwalimu heti kasoma somo la saikokiji,basi pale ndio penyewe, maana wote ni walimu, na akijichanganya anachezea vitasa.

yaani hapo hatuna jinsi, tuvumilie tu pasco.
Trump si wamejaribu kumwandikia mara nyingi lakini wameshindwa. Amewaambia kabisa kuwa mihotuba ya kuandikiwa yeye hapendi na inamyima uhuru kwa sababu anataka kuwa real and authentic. Ndiyo shida (au tuseme uzuri) wa wanasiasa ambao siyo wanasiasa.

Huyu Mayalla si ana namba ya Mheshimiwa na angeomba tu wakutane waongee kilugha chao? "Hi Mayalla wang'wise, ulimhola ngosha? Enhaga mamihayo namhala..." Kuna kick anatafuta au ni kampango fulani wanakafanya (Sorry for mentioning people. Haizuiliki!)
 
Asiyekuwa na 200 ya kuvukia pantoni na apige mbizi. By Unknown.

Mwaka 2020 kura za kishindo za ccm zitatokea kwa Wahaya, mark my word.
Nyie watu wa biharamulo kunyeni mavi mbandike barabarani iwe rami!!
Mtu akileta fyoko atakiona, mimi sijaribiwi!!
 
Kumwambia mkubwa wako anaropoka ni matusi tena matusi sana...
Kumwambia Rais anaropoka ni kosa na ni matusi kabisa..
Sasa naona na wewe umeanza kutafuta kiki baada ya kusifiwa kule kwenye mkutano na waandishi wa habari sasa umeanza kuvuka mipaka....halafu unawaambia watu wasi jadili watu lakini wewe una mtukana Rais wa nchi kiasi hiki halafu unasema anaongea maneno ya hovyo hovyo....acha kutafuta umaatrufu kila mtu ana fahamu wewe ni muandishi wa habari sasa sijui unatafuta kiki za nini zaidi?
Huna adabu
Wewe ni Muhaya usiye na akili, si utamaduni wa wahaya kujipendekeza kama wewe bwegge kabisa, wahaya kiasili ni wajivuni.

Hivi ulitaka mtukanwe vipi ili huyo unayemtetea na kuona ametukanwa ndio ujuwe yeye ndio mwenye matusi tena ya rejareja na mkoa wa Kagera una Wazee wewe takataka funga domo lako huna adabu kutetea mambo ya hovyohovyo.
 
Back
Top Bottom