Juzi ktk mechi kati ya Chelsea vs Wolves,niliona Wolves nao wana mchezaji anaitwa Van Damme(yeye anaitwa Jelle Van Damme)
kuna Mcongo Zaire 1 alishaniongopea zamani eti Jean Claude Van Damme alizaliwa Kinshasa,mhh na mimi nikamuamini wakati ule nilipokuwa kwetu kihansi maana sikuwa na mtandao wa kuthibitisha wala sikuwa na ujanja wa kudai risiti enzi hizo,nikikumbuka yule mcongo uwa nachekesha mwenyewe maana alituongopea karibia wote mimi na wanakijiji wenzangu wa eneo hilo tulimuamini sana na tulikuwa tunamuona yeye ndie anajua vitu vingi hakosei.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.