Obi
JF-Expert Member
- Jul 6, 2009
- 374
- 79
Kuna Story nimeipata kwa rafiki yangu naomba tuijadili kwa maslahi ya Taifa letu lenye rasilimali nyingi lakini ni masikini wa kutupwa.
Nikiwa kati ya WATU waliohudhuria mikutano ya kampeni hasa ya
urais,nimeona mengi,nimesikia mengi,ahadi kemkem,tam,nzuri na zenye
kuvutia na kama JK,SLAA au LIPUMBA mmoja wo akishinda na kutekeleza
ahadi zake basi TANZANIA itakuwa kama Boswana au kama sio kuifikia
Afica kusini. Sina sababu ya kuzitaja ahadi kwani wengi wenu mwazijua.
Ni saa 12:30 za jioni siku ya ijumaa,natoka ofisini kwangu JMOO
nakwenda posta ili kupanda gari la kuelekea mbezi nyumbani
kwangu(mbezi ya kimara).Abiria ni wengi kama kawaida,wezi wamo,ila
kuna magari ya kwenda mbezi ya buku(elfu moja) naingia na muda si
mrefu gari inajaa na kuondoka,wote tumekaa,foleni ni kama kawaida
kwani inaanzia faya na huku gari likiwa limefunguliwa radio moja ya chama
tawala.Watu tupo kimya na aliyesimama ni konda tu.
Mara hiyo radio ikaanza kutangaza sera za mgombea urais wa chama
tawala,ahadi nyingi,kile mara hiki najua mwazijua sina shida ya
kuzitaja ila ni moja tu ambayo nitaitaja ambayo imenipelekea kuandika
UJUMBE huu kwenu,ni ile ya KUNUNUA BAJAJI 40 KWA WAMAMA
WAJAWAZITO,hapo ni saa 1:30 za jioni na hatujavuka magomeni.
Mara baada ya huyo mgombea kutaja hiyo ahadi,nikasikia sauti kutoka
nyuma ya gari ikisema ZIMA RADIO YAKO AU BADILISHA STESHENIni sauti
ya kike tena mwanamama mjamzito.Dereva alizima radio,tukawa kimya kila
mtu nahisi alikuwa anajiuliza kwanini huyu mama kasema radio izimwe au
ibadilishwe stesheni,ukimya ulitawala ndani ya gari.Tukiwa tunaanza foleni
ya ubungo pale mahakama ya ndizi au bigbrother, na ikiwa ni saa 2:07
za usiku,nikasikia sauti ya mwanamama mwingine(sio mjamzito) ikisema
KAMA MIMBA ZINGEKUWA ZINABEBWA KWA ZAMU HUYU KIKWETE ASINGETAMKA
MANENO HAYO nikashtuka nikageuka nyuma nikakutana uso kwa uso na yule
mama mwenye mimba,mimba yake ilikuwa ni kama ya miezi nane tena
ilikuwa kubwa(namaanisha tumbo ni kubwa sana).
Tukiwa tupo stand ya mkoa na gari likiwa limesimama na ni saa 2:45
usiku kumbuka nimetoka posta saa 12:30 za jioni.Yule mama mjamzito
akasimama akaanza kusema MIMI SITOMPA KURA KIKWETE KWA JAMBO
HILI,NILIKUWA NIMPE ILA KWA JAMBO KAMA ILI SIWEZI KUMPA huku akilia na
kutokwa na machozi,yule mama mwingine aliyesema kama mimba zingekuwa
zinabebwa kwa zamu huyu kikwete asingetamka maneno hayo akaanza
kumbembeleza yule mama mjamzito akimsihi akae.Nilimtazama kila mtu
ndani ya gari sura zilibadilika zikawa sura za majonzi.
Nikatoka kwenye daladala(kimawazo) nikaleta taswira ya BAJAJI
nikamuweka yule mama nyuma na mimi nikawa dereva,nikafikiria umbali wa
kilometa 50 toka kijijini kwetu kule kanyigo kuja hospital,barabara
imejaa mashimo,nikawaza tumbo la yule mama akiwa yuma na uchungu na
babaji ikiwa inayumba kwenye mabonde ya barabara,NILILIA
nilishutushwa na honi nyingi za magari ambazo zilikuwa zikilipigia
daladala letu kwa kutotembea, kwani kila mtu alikuwa kwenye mawazo ya
yule mama(nahisi hivyo) na dereva alijisahau kwa kumuonea huruma yule
mama.Nilikuwa karibu na dereva nikamuuliza vp?,akajibu WE ACHA TUuku
akitoa leso na kufuta machozi na kuanza kuendesha gari.
Ni saa 3:07 usiku tupo kimara tunaanza foleni ya kimara stopover,watu
wote wapo kimya hakuna aliyeshuka mpaka sasa na konda kakaa kwenye
mlango ameinama,kila mtu kainama,huku wengine wakifuta mafua,na yule
mama mjamzito akionekana ana hasira na machozi yakimtoka
yenyewe.Nikajiuliza ina maana watu wote tunakwenda mbezi?,pia huyu
mama vp mbona kambadilisha kila mtu ndani ya daladala? Katumwa
nini?.Nikasikia sauti ya baba mmoja kutoka katikakti ya gari akisema
shusha konda hapo,konda akasema wapi?,baba akajibu hapo
hapo,Mmmmmmmmm?,Samahani konda nilikuwa nashuka bucha nimejisahau
alisikika yule baba akisema,Mmmmmmmmm?.Ndipo nilipoona kila mtu karudi
katika hali yake ya kawaida na wengine wakashuka hapo kama watu sita
hivi.Nikajiuliza je walikuwa wanawaza nini? Mpaka wapitishwe
kituoni?.Je walikuwa katika taswira kama yangu?,au uchovu wa kazi?
Kati ya wale walioshuka pale njiani(sio kituoni) baba mmoja akasema
akimwambia yule mama mjamzito POLE SANA MAMA NA MIMI NAKUAHIDI
SITOMPA KURA KIKWETEakateremaka.Tunavuka stopover na ni saa 3:30
usiku,kila mtu kaanza kusema lakeKIKWETE HANA AKILIalisikika baba
mmoja,KIKWETE NI MGONJWA alisikika dada mmoja,WANAIGEIZA NCHI YA
FAMILIA KWANI HAPA TUNATAWALIWA KIFALME alisikika kaka mmoja.Ni saa
3:45 nashuka kibanda cha mkaa na niliposimama nikawwambia abiria HUYO
NDIO RAIS WENU HATA AKIWA CHIZI SI MLIMCHAGU WENYEWE nikajibiwa na
konda SHUKA UKO NA NENDA ZAKO,Mmmmmmmm hata konda?
Nikiwa njiani nakwenda kwangu nikawa natafakari JE YALE MACHOZI YA
MAJI YALIYONDONDOKA NDANI YA DALADALA LEOje ni ya bure tu?,na je IPO
SIKU YATALIPWA?,na je IPO SIKU YATAGEUKA KUWA NI MACHOZI YA DAMU?
nisingependa tafakari yangu ya mwisho itokee.
Je wewe unatoa machozi gani au maneno gani?,je machozi ya furaha? Au
ya uzuni kama yule mama mjamzito?au maneno ya kumtukana rais wako kama
wale watu kwenye daladala.Kazi kwako. Nikipata nauli kabla ya UCHAGUZI
nitakwenda kanyigo nimuulize babu JE BABU UMESHAWAI KUONA KICHUGUU
CHA SENENE?.
Tusimpe Mbu kazi ya kutibu Malaria???????????????????
Nikiwa kati ya WATU waliohudhuria mikutano ya kampeni hasa ya
urais,nimeona mengi,nimesikia mengi,ahadi kemkem,tam,nzuri na zenye
kuvutia na kama JK,SLAA au LIPUMBA mmoja wo akishinda na kutekeleza
ahadi zake basi TANZANIA itakuwa kama Boswana au kama sio kuifikia
Afica kusini. Sina sababu ya kuzitaja ahadi kwani wengi wenu mwazijua.
Ni saa 12:30 za jioni siku ya ijumaa,natoka ofisini kwangu JMOO
nakwenda posta ili kupanda gari la kuelekea mbezi nyumbani
kwangu(mbezi ya kimara).Abiria ni wengi kama kawaida,wezi wamo,ila
kuna magari ya kwenda mbezi ya buku(elfu moja) naingia na muda si
mrefu gari inajaa na kuondoka,wote tumekaa,foleni ni kama kawaida
kwani inaanzia faya na huku gari likiwa limefunguliwa radio moja ya chama
tawala.Watu tupo kimya na aliyesimama ni konda tu.
Mara hiyo radio ikaanza kutangaza sera za mgombea urais wa chama
tawala,ahadi nyingi,kile mara hiki najua mwazijua sina shida ya
kuzitaja ila ni moja tu ambayo nitaitaja ambayo imenipelekea kuandika
UJUMBE huu kwenu,ni ile ya KUNUNUA BAJAJI 40 KWA WAMAMA
WAJAWAZITO,hapo ni saa 1:30 za jioni na hatujavuka magomeni.
Mara baada ya huyo mgombea kutaja hiyo ahadi,nikasikia sauti kutoka
nyuma ya gari ikisema ZIMA RADIO YAKO AU BADILISHA STESHENIni sauti
ya kike tena mwanamama mjamzito.Dereva alizima radio,tukawa kimya kila
mtu nahisi alikuwa anajiuliza kwanini huyu mama kasema radio izimwe au
ibadilishwe stesheni,ukimya ulitawala ndani ya gari.Tukiwa tunaanza foleni
ya ubungo pale mahakama ya ndizi au bigbrother, na ikiwa ni saa 2:07
za usiku,nikasikia sauti ya mwanamama mwingine(sio mjamzito) ikisema
KAMA MIMBA ZINGEKUWA ZINABEBWA KWA ZAMU HUYU KIKWETE ASINGETAMKA
MANENO HAYO nikashtuka nikageuka nyuma nikakutana uso kwa uso na yule
mama mwenye mimba,mimba yake ilikuwa ni kama ya miezi nane tena
ilikuwa kubwa(namaanisha tumbo ni kubwa sana).
Tukiwa tupo stand ya mkoa na gari likiwa limesimama na ni saa 2:45
usiku kumbuka nimetoka posta saa 12:30 za jioni.Yule mama mjamzito
akasimama akaanza kusema MIMI SITOMPA KURA KIKWETE KWA JAMBO
HILI,NILIKUWA NIMPE ILA KWA JAMBO KAMA ILI SIWEZI KUMPA huku akilia na
kutokwa na machozi,yule mama mwingine aliyesema kama mimba zingekuwa
zinabebwa kwa zamu huyu kikwete asingetamka maneno hayo akaanza
kumbembeleza yule mama mjamzito akimsihi akae.Nilimtazama kila mtu
ndani ya gari sura zilibadilika zikawa sura za majonzi.
Nikatoka kwenye daladala(kimawazo) nikaleta taswira ya BAJAJI
nikamuweka yule mama nyuma na mimi nikawa dereva,nikafikiria umbali wa
kilometa 50 toka kijijini kwetu kule kanyigo kuja hospital,barabara
imejaa mashimo,nikawaza tumbo la yule mama akiwa yuma na uchungu na
babaji ikiwa inayumba kwenye mabonde ya barabara,NILILIA
nilishutushwa na honi nyingi za magari ambazo zilikuwa zikilipigia
daladala letu kwa kutotembea, kwani kila mtu alikuwa kwenye mawazo ya
yule mama(nahisi hivyo) na dereva alijisahau kwa kumuonea huruma yule
mama.Nilikuwa karibu na dereva nikamuuliza vp?,akajibu WE ACHA TUuku
akitoa leso na kufuta machozi na kuanza kuendesha gari.
Ni saa 3:07 usiku tupo kimara tunaanza foleni ya kimara stopover,watu
wote wapo kimya hakuna aliyeshuka mpaka sasa na konda kakaa kwenye
mlango ameinama,kila mtu kainama,huku wengine wakifuta mafua,na yule
mama mjamzito akionekana ana hasira na machozi yakimtoka
yenyewe.Nikajiuliza ina maana watu wote tunakwenda mbezi?,pia huyu
mama vp mbona kambadilisha kila mtu ndani ya daladala? Katumwa
nini?.Nikasikia sauti ya baba mmoja kutoka katikakti ya gari akisema
shusha konda hapo,konda akasema wapi?,baba akajibu hapo
hapo,Mmmmmmmmm?,Samahani konda nilikuwa nashuka bucha nimejisahau
alisikika yule baba akisema,Mmmmmmmmm?.Ndipo nilipoona kila mtu karudi
katika hali yake ya kawaida na wengine wakashuka hapo kama watu sita
hivi.Nikajiuliza je walikuwa wanawaza nini? Mpaka wapitishwe
kituoni?.Je walikuwa katika taswira kama yangu?,au uchovu wa kazi?
Kati ya wale walioshuka pale njiani(sio kituoni) baba mmoja akasema
akimwambia yule mama mjamzito POLE SANA MAMA NA MIMI NAKUAHIDI
SITOMPA KURA KIKWETEakateremaka.Tunavuka stopover na ni saa 3:30
usiku,kila mtu kaanza kusema lakeKIKWETE HANA AKILIalisikika baba
mmoja,KIKWETE NI MGONJWA alisikika dada mmoja,WANAIGEIZA NCHI YA
FAMILIA KWANI HAPA TUNATAWALIWA KIFALME alisikika kaka mmoja.Ni saa
3:45 nashuka kibanda cha mkaa na niliposimama nikawwambia abiria HUYO
NDIO RAIS WENU HATA AKIWA CHIZI SI MLIMCHAGU WENYEWE nikajibiwa na
konda SHUKA UKO NA NENDA ZAKO,Mmmmmmmm hata konda?
Nikiwa njiani nakwenda kwangu nikawa natafakari JE YALE MACHOZI YA
MAJI YALIYONDONDOKA NDANI YA DALADALA LEOje ni ya bure tu?,na je IPO
SIKU YATALIPWA?,na je IPO SIKU YATAGEUKA KUWA NI MACHOZI YA DAMU?
nisingependa tafakari yangu ya mwisho itokee.
Je wewe unatoa machozi gani au maneno gani?,je machozi ya furaha? Au
ya uzuni kama yule mama mjamzito?au maneno ya kumtukana rais wako kama
wale watu kwenye daladala.Kazi kwako. Nikipata nauli kabla ya UCHAGUZI
nitakwenda kanyigo nimuulize babu JE BABU UMESHAWAI KUONA KICHUGUU
CHA SENENE?.
Tusimpe Mbu kazi ya kutibu Malaria???????????????????