Hili ni swali la changamoto kuhusu ndugu zetu hawa Wakristu wa Madhehebu ya Kipentekoste maarufu kama "Walokole". Ikumbukwe kuwa Ulokole kwa hapa Tanzania ulishika kasi sana miaka ya '80 na mwanzoni mwa '90.
Enzi hizo ulikua ukisikia Mlokole basi ni Mlokole kwelikweli na hata akiwepo mtaani kwenu Mlokole mmoja tu basi alikua akijulikana kwa utofauti wake hususani ukilinganisha na Wakristo wa Madhehebu mengine.
Baadhi ya tabia, vitu au mazoea mengine ambayo yalionekana kama ni kawaida kwa Wakristu Walokole(wale wa enzi hizo) hawakufanya.
NAORODHESHA hapa baadhi tu (mengine wadau wataongezea)
-Ilikua ni nadra sana kusikia Mlokole anaumwa hata Malaria tu.
-Ilikua ni nadra sana kusikia familia ya kilokole iwe Mke, Mume au Watoto kuumwa ugonjwa wowote.
-Ilikua nadra sana Mlokole kuimba nyimbo za asili/za makabila.
-Ilikua nadra sana kukuta Mlokole akijihusisha na mambo ya michezo kama mpira wa miguu, basketball au "draft".
-Ilikua nadra sana kusikia Mlokole ana boyfriend/girlfriend (Ilikua ni uchumba ukifuatia na ndoa tu).
-Baadhi ya Walokole walikua hawali "kitimoto".
-Baadhi walikua hawatumii baadhi ya vinywaji hata kama ni non alcoholic.
-Ilikua ni marufuku kumkuta Mlokole Bar au kwenye sehemu yoyote ya Starehe hata. kama sehemu hiyo ni ya waziwaziwaziwazi/au hata kama anakunywa soda
-Ilikua hairuhusiwi kufunga harusi wakati mke akiwa mjamzito au ameshazaa mtoto.
.......nyingine ongezea
SWALI KUU; Je Walokole kama wa enzi hizo bado wapo hadi kizazi hiki cha "kidigitali"? Nauliza hivi kwasababu juzikati nilihudhuria ibada ya harusi kwenye dhehebu moja la Walokole (lenye msimamo mkali kuhusu mambo ya ndoa) lakini cha kushangaza nikaona jamaa anamuoa mke ambaye ana mimba kubwa tayari inayoonekana.
Nakumbuka Walokole wa enzi zile walifundisha kuwa Madhehebu mengine yanayoruhusu kufungisha ndoa wakati mke ni mjamzito au ameshazaa tayari ni kinyume na Biblia. Walokole walisisitiza kuwa hadi siku ya kufungishwa harusi ndio inaruhusiwa "kupeana tunda" na si vinginevyo.
Ni nini kimetokea hadi nduguzetu hawa Walokole wamebadili gia angani kuhusiana na mafundisho na ubora wao kama ule wa enzi za '90.
Karibuni kutiririka
Enzi hizo ulikua ukisikia Mlokole basi ni Mlokole kwelikweli na hata akiwepo mtaani kwenu Mlokole mmoja tu basi alikua akijulikana kwa utofauti wake hususani ukilinganisha na Wakristo wa Madhehebu mengine.
Baadhi ya tabia, vitu au mazoea mengine ambayo yalionekana kama ni kawaida kwa Wakristu Walokole(wale wa enzi hizo) hawakufanya.
NAORODHESHA hapa baadhi tu (mengine wadau wataongezea)
-Ilikua ni nadra sana kusikia Mlokole anaumwa hata Malaria tu.
-Ilikua ni nadra sana kusikia familia ya kilokole iwe Mke, Mume au Watoto kuumwa ugonjwa wowote.
-Ilikua nadra sana Mlokole kuimba nyimbo za asili/za makabila.
-Ilikua nadra sana kukuta Mlokole akijihusisha na mambo ya michezo kama mpira wa miguu, basketball au "draft".
-Ilikua nadra sana kusikia Mlokole ana boyfriend/girlfriend (Ilikua ni uchumba ukifuatia na ndoa tu).
-Baadhi ya Walokole walikua hawali "kitimoto".
-Baadhi walikua hawatumii baadhi ya vinywaji hata kama ni non alcoholic.
-Ilikua ni marufuku kumkuta Mlokole Bar au kwenye sehemu yoyote ya Starehe hata. kama sehemu hiyo ni ya waziwaziwaziwazi/au hata kama anakunywa soda
-Ilikua hairuhusiwi kufunga harusi wakati mke akiwa mjamzito au ameshazaa mtoto.
.......nyingine ongezea
SWALI KUU; Je Walokole kama wa enzi hizo bado wapo hadi kizazi hiki cha "kidigitali"? Nauliza hivi kwasababu juzikati nilihudhuria ibada ya harusi kwenye dhehebu moja la Walokole (lenye msimamo mkali kuhusu mambo ya ndoa) lakini cha kushangaza nikaona jamaa anamuoa mke ambaye ana mimba kubwa tayari inayoonekana.
Nakumbuka Walokole wa enzi zile walifundisha kuwa Madhehebu mengine yanayoruhusu kufungisha ndoa wakati mke ni mjamzito au ameshazaa tayari ni kinyume na Biblia. Walokole walisisitiza kuwa hadi siku ya kufungishwa harusi ndio inaruhusiwa "kupeana tunda" na si vinginevyo.
Ni nini kimetokea hadi nduguzetu hawa Walokole wamebadili gia angani kuhusiana na mafundisho na ubora wao kama ule wa enzi za '90.
Karibuni kutiririka