Analogia Malenga
JF-Expert Member
- Feb 24, 2012
- 5,011
- 9,876
JE WAJUA KUHUSU SERA NA SHERIA YA AFYA YA AKILI?
Sera ya afya inasema Afya ya akili ni sehemu muhimu ya huduma za afya ya jamii. Magonjwa na ulemavu wa akili vimekuwa vikiongezeka katika jamii kutokana na mabadiliko ya hali ya maisha. Huduma za afya ya akili nchini ni duni, kutokana na kutopewa umuhimu wake na upungufu wa wataalam wa magonjwa ya akili.
Sheria ya magonjwa ya akili ya mwaka 2008 imetafsiri kuwa magonjwa yatakayoainishwa na shirika la afya duniani(WHO) kuwa ni magonjwa ya akili na nchi itayaona magonjwa husika kama ni magonjwa ya akili.
WHO limetaja Sonona ‘depression’, Bipolar disorder, Schizophrenia (Uchizi), Dementia na Usonji ‘autism’ kuwa ni baadhi ya magonjwa ya akili. Magonjwa haya hasa sonona humfanya mtu kujitoa uhai kwa kuwa mtu huyachukia maisha.
Na sheria ya afya ya akili imetaka watu wenye magonjwa hayo kupelekwa kwa wataalamu wa afya ili kupatiwa matibabu. Sheria ilitaka kuanzishwa kwa National Health for mental health, na sera ilitaka uwepo wa bodi itakayoshughulikia afya ya akili.
Katika hali ya kustaajabisha Januari 2020, Kamanda wa Polisi mkoani Tabora, Barnabas Mwakalukwa alisema wangeanza msako kuwabaini wanaotaka kujinyonga na kisha kuwapeleka Mahakamani.
Kitu ambacho si sahihi kisheria kwa kuwa kwenye sheria ya afya ya akili imemtaka mtu yoyote polisi akiwemo kusaidia kuwabaini wagonjwa wa akili na kuripoti kwa Mental health facility na sio mahakamani
Sera ya afya inasema Afya ya akili ni sehemu muhimu ya huduma za afya ya jamii. Magonjwa na ulemavu wa akili vimekuwa vikiongezeka katika jamii kutokana na mabadiliko ya hali ya maisha. Huduma za afya ya akili nchini ni duni, kutokana na kutopewa umuhimu wake na upungufu wa wataalam wa magonjwa ya akili.
Sheria ya magonjwa ya akili ya mwaka 2008 imetafsiri kuwa magonjwa yatakayoainishwa na shirika la afya duniani(WHO) kuwa ni magonjwa ya akili na nchi itayaona magonjwa husika kama ni magonjwa ya akili.
WHO limetaja Sonona ‘depression’, Bipolar disorder, Schizophrenia (Uchizi), Dementia na Usonji ‘autism’ kuwa ni baadhi ya magonjwa ya akili. Magonjwa haya hasa sonona humfanya mtu kujitoa uhai kwa kuwa mtu huyachukia maisha.
Na sheria ya afya ya akili imetaka watu wenye magonjwa hayo kupelekwa kwa wataalamu wa afya ili kupatiwa matibabu. Sheria ilitaka kuanzishwa kwa National Health for mental health, na sera ilitaka uwepo wa bodi itakayoshughulikia afya ya akili.
Katika hali ya kustaajabisha Januari 2020, Kamanda wa Polisi mkoani Tabora, Barnabas Mwakalukwa alisema wangeanza msako kuwabaini wanaotaka kujinyonga na kisha kuwapeleka Mahakamani.
Kitu ambacho si sahihi kisheria kwa kuwa kwenye sheria ya afya ya akili imemtaka mtu yoyote polisi akiwemo kusaidia kuwabaini wagonjwa wa akili na kuripoti kwa Mental health facility na sio mahakamani