Je waijua Korea Kaskazini?

Je waijua Korea Kaskazini?

eden kimario

JF-Expert Member
Joined
Jun 13, 2015
Posts
10,356
Reaction score
16,400
Jiji kuu ni pyongyang
Serikali - kiongozi mkuu
Ufalme - gojoseon
Nchi hii ilijitangazia uhuru ikiwa bado chini ya utawala wa Japani 1/4/1919
Ukombozi kutoka utawala wa Japani ilikuwa ni 15/8/1945
Jamhuri kamili ilikuwa ni kati ya 15/8/1948 na 9/9/1948
Kwa mujibu wa sensa ya 2013 korea ya kaskazini ina watu milioni 24 na laki 8
Imepakana na korea kusini, china, na urusi
Fedha wanayotumia ni won ya korea kaskazini

Korea ya kaskazini ni matokeo ya ugawaji wa korea baada ya vita kuu ya pili ya dunia
Korea ilikuwa koloni la Japani tangu mwaka 1910 hadi 1945

Kwenye mwaka wa mwisho wa vita kuu ya pili ya dunia
Jeshi la Urusi liliwafuata Wajapani kaskazini mwa ras ya korea huku Wamarekani wakiingilia kusini mwa ras ya korea

Mazungumzo ya kuiunganisha tena korea baada ya uvamizi wa Wajapani yalikufa baada ya vita baridi kuibuka kati ya kaskazini iliyokuwa imekombolewa na Urusi na ile ya kusini iliyokuwa imekombolewa na marekani

Mwisho wa siku kila mmoja alianzisha serikali yake kulingana na itikadi itikadi za waliowasaidia kuikomboa mikononi mwa wajapani ambao ni Urusi na Marekani

Warusi walitaifisha tasnia na ardhi wakaacha serikali ya kikomunisti kazkazini
Huku Marekani ikiacha uchumi wa kibepari katika serikali ya kusini

Katika vita ya korea iliyofuatia korea ya kaskazini ilidumu kwa sababu ya msaada wa kijeshi kutoka china

Mpaka leo serikali ya korea kaskazini inamiliki viwanda karibu vyote nchini humo huku asilimia kubwa ya pato la taifa ikipelekwa katika jeshi ambalo ni jeshi kubwa duniani

Nchi hiyo inakamata nafasi ya 9 katika nchi zilizo na teknolojia kubwa ya kijeshi duniani

Lakini hali ya wananchi wa vijijini ni mbaya kutokana na upungufu wa chakula

Korea kaskazini hutoa misaada ya vyakula na makazi kwa raia wake kwa bei nafuu kwa msaada wa serikali huku elimu na huduma za afya zikitolewa bure

Raia wa korea kaskazini haruhusiwi kutoka nje ya nchi hiyo bila kibali maalum cha serikali au kuingia nchini humo bila kibali maalum

Kodi ya mapato ilifutwa rasmi nchini humo mwaka 1974

Jeshi la korea kaskazini lina jumla ya askari milioni 1 laki 1 na elfu sita

Kwa hiyo ni moja kati ya nchi tano duniani zilizo na jeshi la kudumu lenye askari zaidi ya milioni huku wao wakiongoza

Nchi hiyo ililipua bomu la kwanza la nyuklia mwaka 2006 na inasemekana mpaka sasa wamepiga hatua kubwa kijeshi duniani kwa sababu pato la taifa karibu asilimia 80 huelekezwa jeshini

Unaweza kuongezea na wewe jinsi uijuavyo korea kaskazini
 
f04ffc17c2cfe28013d22d228b74a9dd.jpg
2b68632422a6ae1d7e4d2bb3ef328fe2.jpg
336cbe3323f55d232a0213c6faf5b38d.jpg
0047399b8df05f9e64728f64fbd4c7e5.jpg
 
Umesahau pia kwamba korea ni nchi inayoongoza kwa propaganda za vitisho,na pia ni nchi yenye silaha nying za kizamani tukianzia na ndege za kivita,bunduk,meli,na vifaru,wanatumia silaha zilizotoswa na russia baada ya vita ya pil ya dunia,ndege zao za kivita hazina tofaut na za bongo,wamejitahid sana ku develope continental missilez za kubeba nuclear ndio,ila kwenye silaha zungne,ni kama bongo tuu ingawa wao wanazo nyingi..MIM NI HATER
 
Back
Top Bottom