Setfree
JF-Expert Member
- Dec 25, 2024
- 5,527
- 7,121
Biblia ni kitabu cha kwanza kuandikwa kabla ya vitabu vingine vyote vya kidini duniani. Sehemu ya kwanza ya Biblia — yaani Agano la Kale — iliandikwa maelfu ya miaka kabla ya vitabu au maandiko mengine ya kidini. Hii inatufundisha kuwa Biblia ndiyo chanzo cha kwanza kabisa cha ufunuo wa Mungu kwa wanadamu.
Na hii ndiyo sababu, Biblia imekuwa msingi wa maadili na sheria nyingi duniani. Amri Kumi za Mungu, (Kutoka 20:1–17) ni "uti wa mgongo" wa sheria za mataifa mengi, zikikemea wizi, uongo, uzinzi, uuaji, na ibada ya sanamu. Hata watu wasio na dini wanakiri kwamba mafundisho ya Biblia yana busara na nguvu ya kuongoza maisha yenye haki.
Kwa hiyo, kwa kuwa Biblia ni ya kwanza, ina ukweli wa kwanza na wa mwisho. Kuiweka pembeni na kuamini vitabu vingine, ni sawa na kumweka Mungu pembeni.
Katika Yohana 12:48 tunaambiwa kwamba anayemkataa Yesu na kuyakataa maneno yake; maneno aliyoyasema Yesu yenyewe ndiyo yatamhukumu siku ya mwisho.
Moja kati ya maneno aliyosema Yesu - katika Biblia ni kwamba ,Yeye(Yesu) ndiye njia, kweli na uzima. Hakuna awezaye kwenda mbinguni kwa Baba, bila kupitia kwa Yesu (Yn 14:6).
Na tukumbuke kuwa Yesu Kristo ndiye atakayewahukumu wanadamu wote siku ya mwisho (Mdo 17:31). Siku ya mwisho imekaribia sana kwa jinsi dalili zinavyoonyesha. Shetani anaujua ukweli huu, ndiyo maana anahangaika mchana na usiku kuwashawishi watu wasisome Biblia. Anajua kwamba wakiisoma wataujua ukweli, na ukweli huo utawaweka huru na kuwaokoa kutoka dhambini, na kwa njia hiyo watapata tiketi ya kuingia mbinguni. Shetani anataka watu waangamie pamoja naye motoni.
Usimpe nafasi Shetani. Kataa uongo wake na maajenti wake wanaopindua ukweli wa Biblia. Soma Biblia, na uishi kulingana na yote aliyoyaagiza Yesu. Kumbuka tena: Biblia ndiyo itakayokuhukumu siku ile ya mwisho.
Yohana 12:48
"...yule anayenikataa mimi na kuyakataa maneno yangu; yale maneno niliyoyasema yenyewe yatamhukumu siku ya mwisho."
Na hii ndiyo sababu, Biblia imekuwa msingi wa maadili na sheria nyingi duniani. Amri Kumi za Mungu, (Kutoka 20:1–17) ni "uti wa mgongo" wa sheria za mataifa mengi, zikikemea wizi, uongo, uzinzi, uuaji, na ibada ya sanamu. Hata watu wasio na dini wanakiri kwamba mafundisho ya Biblia yana busara na nguvu ya kuongoza maisha yenye haki.
Kwa hiyo, kwa kuwa Biblia ni ya kwanza, ina ukweli wa kwanza na wa mwisho. Kuiweka pembeni na kuamini vitabu vingine, ni sawa na kumweka Mungu pembeni.
Katika Yohana 12:48 tunaambiwa kwamba anayemkataa Yesu na kuyakataa maneno yake; maneno aliyoyasema Yesu yenyewe ndiyo yatamhukumu siku ya mwisho.
Moja kati ya maneno aliyosema Yesu - katika Biblia ni kwamba ,Yeye(Yesu) ndiye njia, kweli na uzima. Hakuna awezaye kwenda mbinguni kwa Baba, bila kupitia kwa Yesu (Yn 14:6).
Na tukumbuke kuwa Yesu Kristo ndiye atakayewahukumu wanadamu wote siku ya mwisho (Mdo 17:31). Siku ya mwisho imekaribia sana kwa jinsi dalili zinavyoonyesha. Shetani anaujua ukweli huu, ndiyo maana anahangaika mchana na usiku kuwashawishi watu wasisome Biblia. Anajua kwamba wakiisoma wataujua ukweli, na ukweli huo utawaweka huru na kuwaokoa kutoka dhambini, na kwa njia hiyo watapata tiketi ya kuingia mbinguni. Shetani anataka watu waangamie pamoja naye motoni.
Usimpe nafasi Shetani. Kataa uongo wake na maajenti wake wanaopindua ukweli wa Biblia. Soma Biblia, na uishi kulingana na yote aliyoyaagiza Yesu. Kumbuka tena: Biblia ndiyo itakayokuhukumu siku ile ya mwisho.
Yohana 12:48
"...yule anayenikataa mimi na kuyakataa maneno yangu; yale maneno niliyoyasema yenyewe yatamhukumu siku ya mwisho."