Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 4,393
- 14,500
Wakuu!
Tuko kwenye joto la uchaguzi, lakini kuna wimbi la baadhi ya watu mashuhuri kujipendekeza — au kwa lugha nyepesi, uchawa. Tabia hii binafsi siipendi, kwa sababu ina madhara makubwa kwenye mfumo wa uongozi na mustakabali wa taifa letu.
Kilicho hatari zaidi ni kwamba hawa “machawa” wanaonekana kuwa na nguvu ya ushawishi na uwezo wa kuwaathiri wale walio nyuma yao, hasa kwenye maamuzi ya kwenye sanduku la kura.
Umaarufu wao, majina yao au nafasi walizonazo zinatumika kama chombo cha kusukuma ajenda fulani, hali inayowafanya wapiga kura wapoteze uhuru wa kuchagua kwa misingi ya sera na uwezo, na badala yake naona kama wanaingizwa kwenye mkumbo wa ushawishi wa kiitikadi au kihisia.
Tuko kwenye joto la uchaguzi, lakini kuna wimbi la baadhi ya watu mashuhuri kujipendekeza — au kwa lugha nyepesi, uchawa. Tabia hii binafsi siipendi, kwa sababu ina madhara makubwa kwenye mfumo wa uongozi na mustakabali wa taifa letu.
Kilicho hatari zaidi ni kwamba hawa “machawa” wanaonekana kuwa na nguvu ya ushawishi na uwezo wa kuwaathiri wale walio nyuma yao, hasa kwenye maamuzi ya kwenye sanduku la kura.
Umaarufu wao, majina yao au nafasi walizonazo zinatumika kama chombo cha kusukuma ajenda fulani, hali inayowafanya wapiga kura wapoteze uhuru wa kuchagua kwa misingi ya sera na uwezo, na badala yake naona kama wanaingizwa kwenye mkumbo wa ushawishi wa kiitikadi au kihisia.