Je, Tanzania haikujiandaa kuwa mwenyeji wa fainali za Chan, 2025?

Je, Tanzania haikujiandaa kuwa mwenyeji wa fainali za Chan, 2025?

Ad majorem

JF-Expert Member
Joined
Aug 11, 2018
Posts
1,101
Reaction score
1,650
Kwa Wananzengo wenzangu.
Kama mnavyofahamu kipenga cha kufungua Michuano ya Fainali za Afrika kwa wachezaji wa ndani maarufu kama CHAN kwa mwaka 2025, kinapulizwa leo kwenye ardhi ya Kambarage wa Butiama. Hii ni mara ya kwanza kwa Tanzania kuwa mwenyeji wa fainali hizi.

Lakini katika hali ya kushangaza, hakuna shamrashamra zozote kuelekea michuano hiyo. Ukiachana na Tamasha la Singeli, hakuna amsha amsha zile za kuhamasisha watu kuelekea fainali hizo. Hamasa ya National timu, inazidiwa na hamasa ya Ndondo Cup. Juzi nimesafiri kutoka Posta mpaka Mbezi, sikuona Billboard hata moja inayoonyesha Tangazo la fainali hizo. Ni kweli wizara imeshindwa kufanya organisation ya hamasa?

Simba na Yanga huwa wanafanikiwaje kuhamasisha mechi zao?
Au kila mmoja yuko busy na Maandalizi ya Uchaguzi?

Ukipita kwenye vijiwe vya kahawa mjini, hakuna anayezungumzia fainali hizo. Vyombo vya habari na influencers nao hawajafanya vizuri. Je, wamekosa mtu wa kuwaorganise au wamesusa? Je, watu wamekosa uzalendo kwa nchi kiasi hiki? Au ni hujuma kwa serikali ionekane haifanyi kazi yake vizuri?
Mbona watu wa Chama wameweza kuweka Mabango njia zote na mengi kweli. Tunashindwaje kwa jambo la nchi?
TUJISAHIHISHE.
 
Kuna watu watabeza hii
1. Wananchi wamekasirishwa na Maandalizi ya uchaguzi wa TFF ( Hawana pa kusemea zaidi ya kuwaachia wenyewe wajaze uwanja)
2. No reforms no election ya Lisu na chadema mshindo wake umefika mbali sana na huu ndiyo mwanzo wake tu.
TUSUBIRI TUONE lakini watz siyo WAMOJA TENA
 
Lugha ya kiingereza vyombo vya habari pia maofisa wa TFF, maofisa wa wizara Tanzania hii lugha ya kiEngl8sh inawaangusha vibaya sana .

Watawaambia nini watu wa kimataifa kuhusu michuano hiyo.

Wapo waandishi wachache Tanzania ingeweza kuwatunmia waliopo Tanzania wanaoongea Kiingereza na Kifaransa kuitangaza michuano hiyo kuhusu maandalizi, kinachoendelea, miundo mbinu na masuala mengine ya nje ya uwanja.

Michuano hii nchi za Uganda na Kenya ndiyo zitakuwa source ya habari zote kinachoendelea siyo TBC, Azam TV, ZBC, Wasafi, Manara TV, Global TV online, Ayo TV hawajawekeza kuwa na watangazaji waandishi wachambuzi wenye kuwezo wa kutumia lugha za kimataifa.

Kujazana kwa radio, TV na mitandao yote kutumia kiSwahili tu miaka yote madhara yake ndiyo yanaonekana leo hii 2025.

Tuwekeze kwenye waandishi, bloggers, wachambuzi, wataalamu wa michezo wenye uwezo wa kuongea KiEnglish.
 
Kwa Wananzengo wenzangu.
Kama mnavyofahamu kipenga cha kufungua Michuano ya Fainali za Afrika kwa wachezaji wa ndani maarufu kama CHAN kwa mwaka 2025, kinapulizwa leo kwenye ardhi ya Kambarage wa Butiama. Hii ni mara ya kwanza kwa Tanzania kuwa mwenyeji wa fainali hizi.

Lakini katika hali ya kushangaza, hakuna shamrashamra zozote kuelekea michuano hiyo. Ukiachana na Tamasha la Singeli, hakuna amsha amsha zile za kuhamasisha watu kuelekea fainali hizo. Hamasa ya National timu, inazidiwa na hamasa ya Ndondo Cup. Juzi nimesafiri kutoka Posta mpaka Mbezi, sikuona Billboard hata moja inayoonyesha Tangazo la fainali hizo. Ni kweli wizara imeshindwa kufanya organisation ya hamasa?

Simba na Yanga huwa wanafanikiwaje kuhamasisha mechi zao?
Au kila mmoja yuko busy na Maandalizi ya Uchaguzi?

Ukipita kwenye vijiwe vya kahawa mjini, hakuna anayezungumzia fainali hizo. Vyombo vya habari na influencers nao hawajafanya vizuri. Je, wamekosa mtu wa kuwaorganise au wamesusa? Je, watu wamekosa uzalendo kwa nchi kiasi hiki? Au ni hujuma kwa serikali ionekane haifanyi kazi yake vizuri?
Mbona watu wa Chama wameweza kuweka Mabango njia zote na mengi kweli. Tunashindwaje kwa jambo la nchi?
TUJISAHIHISHE.
Mpunga wote upo kwenye uchaguzi isee hakuna mwenye habari na mpira wanasiasa sio watu.
 
Lugha ya kiingereza vyombo vya habari Tanzania inawaangusha.

Watawaambia nini watu wa kimataifa kuhusu michuano hiyo.

Wapo waandishi wachache Tanzania ingeweza kuwatunmia waliopo Tanzania wanaoongea Kiingereza na Kifaransa kuitangaza michuano hiyo kuhusu maandalizi, kinachoendelea, miundo mbinu na masuala mengine ya nje ya uwanja.

Michuano hii nchi za Uganda na Kenya ndiyo zitakuwa source ya habari zote kinachoendelea siyo TBC, Azam TV, ZBC, Wasafi, Manara TV, Global TV online, Ayo TV hawajawekeza kuwa na watangazaji waandishi wachambuzi wenye kuwezo wa kutumia lugha za kimataifa.

Kujazana kwa radio, TV na mitandao yote kutumia kiSwahili tu miaka yote madhara yake ndiyo yanaonekana leo hii.

Tuwekeze kwenye waandishi, bloggers, wachambuzi, wataalamu wa michezo wenye uwezo wa kuongea KiEnglish.
NI HUZUNI
 
Lugha ya kiingereza vyombo vya habari Tanzania inawaangusha.

Watawaambia nini watu wa kimataifa kuhusu michuano hiyo.

Wapo waandishi wachache Tanzania ingeweza kuwatunmia waliopo Tanzania wanaoongea Kiingereza na Kifaransa kuitangaza michuano hiyo kuhusu maandalizi, kinachoendelea, miundo mbinu na masuala mengine ya nje ya uwanja.

Michuano hii nchi za Uganda na Kenya ndiyo zitakuwa source ya habari zote kinachoendelea siyo TBC, Azam TV, ZBC, Wasafi, Manara TV, Global TV online, Ayo TV hawajawekeza kuwa na watangazaji waandishi wachambuzi wenye kuwezo wa kutumia lugha za kimataifa.

Kujazana kwa radio, TV na mitandao yote kutumia kiSwahili tu miaka yote madhara yake ndiyo yanaonekana leo hii.

Tuwekeze kwenye waandishi, bloggers, wachambuzi, wataalamu wa michezo wenye uwezo wa kuongea KiEnglish.
Nakubaliana na wewe, lugha ya Kimataifa imekua changamoto kubwa kwetu. Tunajificha sana kwenye kiswahili, lakini ukweli ni kwamba, Kiswahili sio lugha Rasmi kwenye majukwaa ya Kimataifa. Tuhimizane kujifunza kiingereza .
 
No body cares...

Cag alisema Kuna matumizi yasiyo na tija bilioni 600..wangetumia hizo kuwekeza kwenye marketing ..si pesa za kumwaga zipo..royal family waweke hela
 
Watanganyika mnapenda kudogosha sana vitu vyenu

Waziri Selemani Jaffo katazo la vyombo vya kigeni katika tasnia ya utangazaji vimepigwa marufuku.

Moja ya matokeo ya kutokuwekeza ktk mtazamo mpana wa kimataifa kuwepo vyombo vyenye base au vituo makao yao Tanzania kuweza kuitangaza nchi na matukio mbalimbali, ni katika eneo la michezo na burudani tumefeli sana utangazaji kimataifa.
 
Tanzania inachoweza ni Kuuza Rasilimali za Nchi ikiwemo Bandari na mwendokasi
 
Watanzania wengi hawana hamasa na timu yao ya taifa tofauti na vilabu hivi vya kariakoo, na pili shirikisho la mpira TFF na wizara haijatoa hamasa ya kutosha kuelekea fainali hizi
 
Kuna watu watabeza hii
1. Wananchi wamekasirishwa na Maandalizi ya uchaguzi wa TFF ( Hawana pa kusemea zaidi ya kuwaachia wenyewe wajaze uwanja)
2. No reforms no election ya Lisu na chadema mshindo wake umefika mbali sana na huu ndiyo mwanzo wake tu.
TUSUBIRI TUONE lakini watz siyo WAMOJA TENA
Labda wewe na mkeo au mmeo ndio sio wamoja. Wengine tangu mchana tumekusanyika sehemu tunaisubiri ufunguzi! Wewe eti Watanzania si wamoja! Si wa Moja wa nyoko!!!
 
Back
Top Bottom