Ndugu zangu nimejiuliza: Hivi Shetani kuna kitabu chochote ambacho amejitetea?

Ndugu zangu nimejiuliza: Hivi Shetani kuna kitabu chochote ambacho amejitetea?

Ndugu zangu nimejiuliza hivi Shetani kuna kitabu chochote ambacho amejitetea kutokana na tuhuma lukuki zinazomkabili? Au yeye ndo hana cha kusema kashakubali kuangushiwa jumba bovu?😁
Shetani anafanya kazi kupitia binadamu hivyo utetezi wake huufanya kupitia kwa binadamu.
Na shetani yupo kila mahali,misikitini,makanisani,kwenye michezo,kwenye ufuska,kwenye mabenki na serikalini yupo
 
Shetani anafanya kazi kupitia binadamu hivyo utetezi wake huufanya kupitia kwa binadamu.
Kwa maana hiyo, shetani sio binadamu.
fimboyaukwaju said:
Na shetani yupo kila mahali,misikitini,makanisani,kwenye michezo,kwenye ufuska,kwenye mabenki na serikalini yupo
Unanichanganya ujue!
Kama kama anafanya kazi kupitia binadamu iweje tena awe msikitini, kanisani, kwenye bar, michezo na kila mahali???!!

Inamaana shetani ni watu!!???
 
Ndugu zangu nimejiuliza hivi Shetani kuna kitabu chochote ambacho amejitetea kutokana na tuhuma lukuki zinazomkabili? Au yeye ndo hana cha kusema kashakubali kuangushiwa jumba bovu?😁
Sijawahi kusikia wala kuona tuhuma dhidi ya shetani ambayo si ya kweli, na hivyo sioni kwa nini ajiteteee. Lakini nimeona na kusikia tuhuma nyingi dhidi ya Mungu ambazo si za kweli, na zaidi Mungu yeye mwenyewe kujitetea, anawataka wanadamu wamtetee, kama mashahidi wake.


Ezekiel 18:23: Je, mimi Bwana Mwenyezi-Mungu, nafurahia kufa kwake mtu mwovu? La hasha! Mimi napendelea aachane na njia zake mbaya apate kuishi.

Isaya 43:10; Mataifa yote na yakusanyike, watu wote na wakutane pamoja. Nani kati ya miungu yao awezaye kutangaza yatakayotukia? Nani awezaye kutuonesha yanayotukia sasa? Wawalete mashahidi wao kuthibitisha kwamba walifanya hivyo. Waache wasikilize na kusema, “Ilikuwa kweli". Nyinyi ni mashahidi wangu; niliwachagua muwe watumishi wangu, mpate kunijua na kuniamini, kwamba ndimi peke yangu Mungu. Kabla yangu hajapata kuwapo mungu mwingine, wala hatakuwapo mungu mwingine.
 
ahsante, mana yake shetani alikubali makosa na kuomba msamaha sio?
Kwamba unamuonea huruma 😂.

Ndomana kitabu cha Enoch kilifichwa mpaka siku za mwisho.

Sasa kama alikubali makosa mbona anaendelea kufanya maovu!

Ukitaka kujua character ya shetani angalia wafuasi wake, mfano:
wakana Mungu wanaozunguka na mabango kumkana Mungu na kumkashifu Mungu daily wanajiona wana akili na uwezo wote kama Mungu,
wauaji, wabakaji, wasio waaminifu kwa wenza wao, wanaotelekeza watoto wao etc. Shetani huyo hapo.

Satan is antigod. In a world of Free will he chose to Oppose God.

Miaka mitatu ya dhiki kuu (soon) kuelekea kurudi kwa Yesu mashetani yataachiwa na yatafanya uharibifu mkubwa, na wakati finally Yesu anakuja duniani watataka kupigana naye! !
Does this look like a repentant character!

Na adhabu yake ilitamkwa tangu siku aliyoasi. Hata moto wa maangamizi uliwekwa kwaajili yake, wanadamu wote wangemkubali Yesu hakuna hata mmoja angetupwa huko, huko wangeishia shetani na malaika waasi wenzake tu.

“Kisha atawaambia wale walio upande wake wa kushoto, ‘Ondokeni kwangu, ninyi mliolaaniwa, nendeni kwenye moto wa milele ulioandaliwa kwa ajili ya ibilisi na malaika wake."
Mathayo.25.41.NENO
 
Kwa maana hiyo, shetani sio binadamu.

Unanichanganya ujue!
Kama kama anafanya kazi kupitia binadamu iweje tena awe msikitini, kanisani, kwenye bar, michezo na kila mahali???!!

Inamaana shetani ni watu!!???
kwani huko misikitini na makanisani wapo kina nani? Si ni binadamu ndio wapo huko,kwani pasta,padri ai shehe anapozini,huwa wanafanyakazi kwa niana ya nani?
 
Tupe somo kidogo mkuu, ni kwanini
Kitabu cha Enoch hakikuwekwa kwenye Biblia nyingi (kwenye nyingine kipo) mainly because Wayahudi hawakukichukulia kama sehemu ya Maandiko (Biblia ya Wayahudi / Agano la kale).

Kikawepo wepo kinasomwa kinanakiliwa lakini hakikupewa umuhimu.

Hadi wazee wa kanisa kwenye mabaraza yao walipoamua vitabu vipi ni maandiko matakatifu, vipi vimeibuka na wazushi ni vya kutupwa, na vingine kama cha Enoch kimewekwa kama kitabu chenye taarifa muhimu za ziada, lakini sio maandiko matakatifu.

What I find interesting ni
1) kwanza kimekutwa kati ya dead sea scrolls (vitabu vya wayahudi / agano la kale), so whoever alificha agano la kale aliona hicho kitabu ni cha muhimi au ni kitakatifu

2)Halafu ni wakati wa kuibuka kwake na kuwa public. 1947. Tunaofuatilia end time prophecies that is such an interesting time coz it's right about when Israel came back as a nation, ticking the end times clock. You know Yesu atashukia Yerusalemu kuwaokoa Wayahudi wakiwa wamezingirwa kila kona....

3)Halafu kitabu chenyewe kinaanza kwa kusema:

"Maneno ya baraka ya Henoko, ambayo kwa hayo aliwabariki wateule na wenye haki, watakaokuwa hai katika siku ya dhiki, wakati waovu wote na wasiomcha Mungu watakapoondolewa.

Naye akaanza mfano wake akisema:

‘Henoko, mtu mwenye haki, ambaye macho yake yalifunguliwa na Mungu, aliona maono ya Mtakatifu aliye mbinguni,

ambayo malaika walinionyesha, na kutoka kwao nilisikia kila kitu, na kutoka kwao nilielewa yale niliyoona; lakini si kwa ajili ya kizazi hiki, bali kwa ajili ya kizazi cha mbali kitakachokuja."


So ni kama kimeibuka kwa wakati sahihi uliowekwa, kwa ajili ya kusomwa na kizazi cha mwisho kitakachoshuhudia ujio wa Yesu. Kwa wanaopenda kupiga hesabu kuna muda na tarehe humo...
 
kwani huko misikitini na makanisani wapo kina nani? Si ni binadamu ndio wapo huko,kwani pasta,padri ai shehe anapozini,huwa wanafanyakazi kwa niaBa ya nani?
Me nachojua akizini, anakuwa anajiridhisha, baada ya tamaa ya kusex kumuingia. Sidhani kama anazini kwa niaba ya mtu au kitu. Kwa sababu anaridhika mwenyewe.
 
Kwanini Mungu hajawasamehe hadi leo wakati sisi tunaambiwa lazima tuwasamehe waliotukosea?
Kwasababu sisi ni watoto wa Mungu tutakaoishi kwenye Ufalme wa Mungu,
kwahiyo tunafundishwa kuwa kama Mungu, kama alivyotusamehe na sisi tunaseme, na inawezekana kwasababu ya kuamini Damu ya Yesu iliyomwagwa.

Guess nani aliimwaga damu ya Yesu? Tena wakati Yesu anarudi atataka kupigana naye!

Ni mtoto wa nani huyu sasa!
Ataishi wapi!
Nani anataka kuishi na huyu!

Hulka yake ni kutotii na kuharibu. Na hakukuwa na mpango wa kumuokoa. Kwanza sio mtoto ni baba.

"Ninyi ni watoto wa baba yenu, ibilisi, nanyi mnataka kutimiza matakwa ya baba yenu. Yeye alikuwa muuaji tangu mwanzo, wala hakushikana na kweli, maana hamna kweli ndani yake. Anaposema uongo, yeye husema lugha yake ya asili kwa maana yeye ni mwongo na baba wa huo uongo."
Yohana.8.44.NENO

Huyu unayetaka kumuonea huruma hana nafasi ya kuweka hiyo huruma unayompa.

Ndomanaa adhabu yake ilitamkwa on the spot baada ya uovu wake wa kwanza kabisa.

Na sisi wokovu na tumaini letu lilitajwa on the spot wakati tumeanguka kwa mara ya kwanza kabisa.
 
Shetani maana yake ni kiumbe (Jini au binadamu) muasi ambaye hupotosha viumbe (binadam na majini) wengine kuelekea katika njia ya sawasawa (iliyonyooka).

Mkuu wa mashaytwaan (mashetani) anaitwa Iblis. Huyu alilaaniwa mbinguni mara baada ya kukataa amri ya Mungu juu ya kumsujudia (kumpa heshima) Adam . Alikuwa na kiburi kwa kujiona yeye ni bora kutokana na kuumbwa kwa moto kuliko Adam aliyeumbwa kutokana na udongo.

Alimgomea Mungu katakata...na hata alipopewa nafasi ya kuomba msamaha (kutubia) kosa lake pia hakufanya hivyo ila alichagua kupewa umri mrefu wa kuishi duniani ili apate kuvipoteza vizazi vyote vya Adam.

Uadui wa Iblis kwa mwanadamu hauishi mpaka pale dunia itakapotamatika. Iblis ana majeshi yake ya wanaadamu na Majini...ambao nao pia huitwa mashetani kutokana na uasi wao na dhamira yao ya kupotosha vijmbe wengine wasieleke katika njia ya Mungu.

Jibu la swali lako ni kuwa Iblis ni ana jeuri ,kiburi na kujiona hivyo suala la kuomba msamaha kwake halipo moyoni mwake licha ya kujua hatma yake kuwa ni Motoni.

Mfano mzuri ni anko wake Mtume Muhammad (s.a.w) aliyeitwa Abu lahab...huyu alikuwa ni mpinzani mkubwa wa Mtume Muhammad enzi za uhai wake, Ufunuo uliteremshwa na Mungu kuja kwa Mtume kumuhusu Abu lahab na mkewe kuwa watakuwa ni kuni za motoni. Licha ya ujumbe huu mkali Abu Lahab na mkewe hawakufikiria suala la kusilimu na kuingia katika Uislam mpk kufa kwao. Moja kati ya muujiza mkubwa sana wa kitabu cha Quran kwani huyu mtu angesilimu basi Quran ingeonekana si ya kweli lwa kumuhukumu mtu Moto yungali hai na ameukubali Uislam.

Vivyohivyo Iblis (laana za Mungu ziwe juu yake) anajua maandiko yote ya Mungu katika vitabu vya Taurat,Zabur,Injil na Quran zikimuhukumu Moto ila hajawahi kutaka kuomba msamaha maishani mwake...Amechagua uasi badala ya uongofu.
 
Shetani hupoteza wanaadamu kupitia minong'ono inayoitwa waswas..ambapo huingiza mawazo maovu ndani ya akili ya mtu na kumpoteza kidogokidogo kupitia hatua zinazoitwa Khutuwaat Shaytwaan (footsteps of the devil).
 
Shetani maana yake ni kiumbe (Jini au binadamu) muasi ambaye hupotosha viumbe (binadam na majini) wengine kuelekea katika njia ya sawasawa (iliyonyooka).

Mkuu wa mashaytwaan (mashetani) anaitwa Iblis. Huyu alilaaniwa mbinguni mara baada ya kukataa amri ya Mungu juu ya kumsujudia (kumpa heshima) Adam . Alikuwa na kiburi kwa kujiona yeye ni bora kutokana na kuumbwa kwa moto kuliko Adam aliyeumbwa kutokana na udongo.

Alimgomea Mungu katakata...na hata alipopewa nafasi ya kuomba msamaha (kutubia) kosa lake pia hakufanya hivyo ila alichagua kupewa umri mrefu wa kuishi duniani ili apate kuvipoteza vizazi vyote vya Adam.

Uadui wa Iblis kwa mwanadamu hauishi mpaka pale dunia itakapotamatika. Iblis ana majeshi yake ya wanaadamu na Majini...ambao nao pia huitwa mashetani kutokana na uasi wao na dhamira yao ya kupotosha vijmbe wengine wasieleke katika njia ya Mungu.

Jibu la swali lako ni kuwa Iblis ni ana jeuri ,kiburi na kujiona hivyo suala la kuomba msamaha kwake halipo moyoni mwake licha ya kujua hatma yake kuwa ni Motoni.

Mfano mzuri ni anko wake Mtume Muhammad (s.a.w) aliyeitwa Abu lahab...huyu alikuwa ni mpinzani mkubwa wa Mtume Muhammad enzi za uhai wake, Ufunuo uliteremshwa na Mungu kuja kwa Mtume kumuhusu Abu lahab na mkewe kuwa watakuwa ni kuni za motoni. Licha ya ujumbe huu mkali Abu Lahab na mkewe hawakufikiria suala la kusilimu na kuingia katika Uislam mpk kufa kwao. Moja kati ya muujiza mkubwa sana wa kitabu cha Quran kwani huyu mtu angesilimu basi Quran ingeonekana si ya kweli lwa kumuhukumu mtu Moto yungali hai na ameukubali Uislam.

Vivyohivyo Iblis (laana za Mungu ziwe juu yake) anajua maandiko yote ya Mungu katika vitabu vya Taurat,Zabur,Injil na Quran zikimuhukumu Moto ila hajawahi kutaka kuomba msamaha maishani mwake...Amechagua uasi badala ya uongofu.
Been learning about Islam lately :2Head

Post in thread 'Mimi ni muislamu, nitakufa kwenye uislamu ila nakiri utume wa Muhammad unatia mashaka sana' Mimi ni muislamu, nitakufa kwenye uislamu ila nakiri utume wa Muhammad unatia mashaka sana
 
Back
Top Bottom