Je, sera ipi ya elimu inatumika kwa sasa nchini?

Je, sera ipi ya elimu inatumika kwa sasa nchini?

DullyJr

JF-Expert Member
Joined
Apr 10, 2011
Posts
13,993
Reaction score
11,878
Habari zenu wakuu?

Leo nimeamua kuja na swali ambalo kiukweli limekuwa likinitatiza ila kwa kuwa hapa tunakutana watu mbalimbali wenye upeo tofauti naweza kutoa sintofahamu iliyopo kichwani mwangu na kwa baadhi ya wadau........


SWALI: NI SERA IPI YA ELIMU INAYOTUMIKA NCHINI KWA SASA?

JE, NI HII ILIYOZINDULIWA NA MHE. JAKAYA MRISHO KIKWETE MWAKA 2014 AU KUNA NYINGINE?

Nakumbuka katika mwaka 2014 serikali ilifanya mabadiliko ya Sera na kuja na Sera mpya ya elimu na mafunzo ya mwaka 2014 ,Sera hiyo ilikuja na miongozo,matamko na mikakati ya utekelezaji wake.

Sera hiyo ilikuja na vitu kama

KUTILIA MKAZO KKK

ELIMU YA AWALI KUWA NI YA LAZIMA

ELIMUMSINGI ambayo iliweka wazi mfumo wa elimu mpya utakaotumika kuwa ni kufanya darasa LA kwanza mpaka kidato cha nne kuwa ni lazima ambapo walipendekeza mfumo wa 1-10-2-3+ na kuachana na ule wa 2-7-4-2-3+ ambapo kigezo kikubwa kilichotumika ilikuwa in kupunguza muda wa mwanafunzi kukaa shuleni ili kupata graduate wenye umri mdogo ili walitumikie Taifa kwa muda mrefu..........

Sasa Sera hiyo INA mambo mengi sana ambayo tukiorodhesha hapa tutakesha ila kwa uchache wake ni hivyo.

Sintofahamu imekuja baada ya serikali iliyoingia madarakani kuja na mambo mapya ambayo ni tofauti kabisa na Sera hiyo katika utekelezaji wake kwa mfano,

KURUDISHWA KWA MFUMO WA ZAMANI WA ELIMU NCHINI wa 2+7+4+2+3+ ambao unarudisha moja kwa moja ufanywaji wa mitihani ya darasa LA saba.

Kurudisha usimamiwaji na uendeshwaji wa mafunzo ya ualimu NECTA badala ya NACTE

Kurudisha grade a na stashahada ya uailimu wa sekondari na kufuta ODPE na ODECE zilizoletwa na Sera mpya.Matokeo yake wamewaweka katika sintofahamu kubwa hawa wahitimu wa ODPE na ODECE ambao kiuhalisia ndio matakwa ya Sera hiyo ambao walikuwa wanakuja kutekeleza mtaala mpya hasa wa awali wa mwaka 2016, ina maana kama mtaala huu haupo nini hatma ya hawa graduate?

Badala yake tunashuhudia kupelekwa kwa walimu wa sekondari katika shule za msingi kufanya utekelezaji wa mtaala ambao hatujausomea, ikiwa waliosomea mtaala huo wapo mitaani.....

Inamaana hili kundi kubwa LA watoto waliopo shule za msingi kwa sasa wakimaliza na kuanza kidato cha kwanza serikali itaturudisha tena maana lazma kutakuwa na uhaba wa walimu tu sasa hizi danadana mpaka lini??maana juzi naona TAMISEMI wameweka tangazo kuwa walimu 11000 was sekondari watapelekwa msingi mwaka huu....

AU NDIO WANAPELEKWA KULE WAZOEE MAZINGIRA MAPEMA YA KUFUNDISHA DARASA LA 8 - 10 YA ELIMU MSINGI,TUFAFANULIENI HILI FUMBO


Karibuni kwa michango......

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Write your reply...Viongozi Wa Wizara Ya Elimu Wengi Wana Jua Mfumo Wa Elimu Ni Kupandisha G.P.A Tu,
 
Write your reply...Viongozi Wa Wizara Ya Elimu Wengi Wana Jua Mfumo Wa Elimu Ni Kupandisha G.P.A Tu,
Kuna mambo mengi hayakaa sawa katika mfumo wetu wa elimu na serikali kwa ujumla hili linapelekea kila anayeingia kwenye system anaona ana jipya la kufanya....matokeo yake ndio yale huyu anaunganisha physics na chemistry huyu anafuta masomo ya biashara dah sijui mpaka lini hii

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pole mkuu najua wewe ni mwalimu was arts na hutaki kwenda primary usijali kikombe kitakuepuka
 
Habari zenu wakuu?

Leo nimeamua kuja na swali ambalo kiukweli limekuwa likinitatiza ila kwa kuwa hapa tunakutana watu mbalimbali wenye upeo tofauti naweza kutoa sintofahamu iliyopo kichwani mwangu na kwa baadhi ya wadau........


SWALI: NI SERA IPI YA ELIMU INAYOTUMIKA NCHINI KWA SASA?

JE, NI HII ILIYOZINDULIWA NA MHE. JAKAYA MRISHO KIKWETE MWAKA 2014 AU KUNA NYINGINE?

Nakumbuka katika mwaka 2014 serikali ilifanya mabadiliko ya Sera na kuja na Sera mpya ya elimu na mafunzo ya mwaka 2014 ,Sera hiyo ilikuja na miongozo,matamko na mikakati ya utekelezaji wake.

Sera hiyo ilikuja na vitu kama

KUTILIA MKAZO KKK

ELIMU YA AWALI KUWA NI YA LAZIMA

ELIMUMSINGI ambayo iliweka wazi mfumo wa elimu mpya utakaotumika kuwa ni kufanya darasa LA kwanza mpaka kidato cha nne kuwa ni lazima ambapo walipendekeza mfumo wa 1-10-2-3+ na kuachana na ule wa 2-7-4-2-3+ ambapo kigezo kikubwa kilichotumika ilikuwa in kupunguza muda wa mwanafunzi kukaa shuleni ili kupata graduate wenye umri mdogo ili walitumikie Taifa kwa muda mrefu..........

Sasa Sera hiyo INA mambo mengi sana ambayo tukiorodhesha hapa tutakesha ila kwa uchache wake ni hivyo.

Sintofahamu imekuja baada ya serikali iliyoingia madarakani kuja na mambo mapya ambayo ni tofauti kabisa na Sera hiyo katika utekelezaji wake kwa mfano,

KURUDISHWA KWA MFUMO WA ZAMANI WA ELIMU NCHINI wa 2+7+4+2+3+ ambao unarudisha moja kwa moja ufanywaji wa mitihani ya darasa LA saba.

Kurudisha usimamiwaji na uendeshwaji wa mafunzo ya ualimu NECTA badala ya NACTE

Kurudisha grade a na stashahada ya uailimu wa sekondari na kufuta ODPE na ODECE zilizoletwa na Sera mpya.Matokeo yake wamewaweka katika sintofahamu kubwa hawa wahitimu wa ODPE na ODECE ambao kiuhalisia ndio matakwa ya Sera hiyo ambao walikuwa wanakuja kutekeleza mtaala mpya hasa wa awali wa mwaka 2016, ina maana kama mtaala huu haupo nini hatma ya hawa graduate?

Badala yake tunashuhudia kupelekwa kwa walimu wa sekondari katika shule za msingi kufanya utekelezaji wa mtaala ambao hatujausomea, ikiwa waliosomea mtaala huo wapo mitaani.....

Inamaana hili kundi kubwa LA watoto waliopo shule za msingi kwa sasa wakimaliza na kuanza kidato cha kwanza serikali itaturudisha tena maana lazma kutakuwa na uhaba wa walimu tu sasa hizi danadana mpaka lini??maana juzi naona TAMISEMI wameweka tangazo kuwa walimu 11000 was sekondari watapelekwa msingi mwaka huu....


Karibuni kwa michango......

Sent using Jamii Forums mobile app
Kama hao walimu wa awali ndio wamepoteza muda kabisa ,kifupi ule mfumo ulioletwa na Sera ya mjomba inaonekana dhahiri kuwa umepigwa chini na jpm
 
Kuna mambo mengi hayakaa sawa katika mfumo wetu wa elimu na serikali kwa ujumla hili linapelekea kila anayeingia kwenye system anaona ana jipya la kufanya....matokeo yake ndio yale huyu anaunganisha physics na chemistry huyu anafuta masomo ya biashara dah sijui mpaka lini hii

Sent using Jamii Forums mobile app
Well Said Mkuu,
 
Mie naona it’s clear wizara ya elimu ina lack skills lazima kulitakiwa kuwa na researchers kwenye hio wizara,wanaoiweza kuangalia jambo before kuli implement ,elimu ni swala senstive sio la kupigia dana dana au butua butua
 
Mie naona it’s clear wizara ya elimu ina lack skills lazima kulitakiwa kuwa na researchers kwenye hio wizara,wanaoiweza kuangalia jambo before kuli implement ,elimu ni swala senstive sio la kupigia dana dana au butua butua
Sahihi kabisa mkuu, lakini unaweza kuta hawa watu wapo ila hakuna wanalofanya au inawezekana kabisa mchanganyiko wa taaluma na siasa ndio ikawa inatucost maana kuchanganya taaluma na siasa no sawa na kuchanganya mlenda na pilau......

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mm mwenyewe nashindwa kuelewa hawa watu. Walisema kua upande wa Primary,, mwisho itakua darasa la sita,,kila baadae waziri wa elimu bungeni alikanusha. Na hawajatoa matamko kuhusiana na hili jambo,,kua mwisho ni la saba au la sita. Maana hata syllubus zilizopo inaonesha kuhitimu ni Darasa la sita. Mwenye ujuzi tafadhali anijuze.
 

Attachments

  • Screenshot_20190126-173301.png
    Screenshot_20190126-173301.png
    44.6 KB · Views: 33
Mm mwenyewe nashindwa kuelewa hawa watu. Walisema kua upande wa Primary,, mwisho itakua darasa la sita,,kila baadae waziri wa elimu bungeni alikanusha. Na hawajatoa matamko kuhusiana na hili jambo,,kua mwisho ni la saba au la sita. Maana hata syllubus zilizopo inaonesha kuhitimu ni Darasa la sita. Mwenye ujuzi tafadhali anijuze.
Yaani wizara ya elimu pale kuna maswali mengi kuliko majibu.....hasa hilo suala ndio linachanganya sana watu,Sera inatamka vingine waziri anatamka vingine........

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hii serikali bila ya kuwa na raia walio active kufuatilia mambo ya msingi ...utakuja kushangaa siku nchi IPO ktk shimo kubwa sana.....

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yaani wizara ya elimu pale kuna maswali mengi kuliko majibu.....hasa hilo suala ndio linachanganya sana watu,Sera inatamka vingine waziri anatamka vingine........

Sent using Jamii Forums mobile app
Watoto wanaotakiwa kuhitimu Shule ya msingi na sera mpya ambao ndo wanatumia syllubus ya hio sera wako darasa la 5 yaani mwakani wanahitimu la sita wakiuungana na wenzao wa darasa la 7. Kwa maana nyingine ni kwamba makundi mawili ya malaki ya wanafunzi watahitimu. Je serikali inatuambia nn wadau wa elimu?
 
Watoto wanaotakiwa kuhitimu Shule ya msingi na sera mpya ambao ndo wanatumia syllubus ya hio sera wako darasa la 5 yaani mwakani wanahitimu la sita wakiuungana na wenzao wa darasa la 7. Kwa maana nyingine ni kwamba makundi mawili ya malaki ya wanafunzi watahitimu. Je serikali inatuambia nn wadau wa elimu?
Ile Sera ipitie vizuri haitamki kuwa motto atamaliza darasa la 6 ila inaondoa mtihani wa darasa la 7 na mtoto ataendelea mpaka darasa la 10 yaani kwa kifupi Yale madarasa ya form1 mpaka form4 wameyaingiza humo ndani na kuiita ni ELIMUMSINGI ambayo ni ya lazima wakimaanisha asiwepo mtoto anayeishia 7 alafu akawa na option ya kuendelea au kutoendelea na masomo na elimu hii ni BURE.
so akimaliza hilo LA 10 ndio anasoma advance then university..........

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ila kwakuwa watoto kwa sasa wapo darasa LA 5 cha msingi tusubiri tuone mwaka wa keshokutwa watamaliza std 7 au ndio wataendelea std8 maana hili la serikali kupeleka walimu wa sekondari kule katika shule za msingi linanipa maswali..isije kuwa ndio wanapelekwa kufundisha darasa la 8 mpaka la 10.......kinachonishangaza ni kwanini iwe walimu wa sanaa tu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ile Sera ipitie vizuri haitamki kuwa motto atamaliza darasa la 6 ila inaondoa mtihani wa darasa la 7 na mtoto ataendelea mpaka darasa la 10 yaani kwa kifupi Yale madarasa ya form1 mpaka form4 wameyaingiza humo ndani na kuiita ni ELIMUMSINGI ambayo ni ya lazima wakimaanisha asiwepo mtoto anayeishia 7 alafu akawa na option ya kuendelea au kutoendelea na masomo na elimu hii ni BURE.
so akimaliza hilo LA 10 ndio anasoma advance then university..........

Sent using Jamii Forums mobile app
Ahaaaaa, sawa mkuu,, hapo nimekuelewa. Walimu na wazazi wamekua kwenye sintofahamu. Kingine chama kusikitisha,, wizara haijatunga vitabu vinavyoendana na hii sera.
 
Ahaaaaa, sawa mkuu,, hapo nimekuelewa. Walimu na wazazi wamekua kwenye sintofahamu. Kingine chama kusikitisha,, wizara haijatunga vitabu vinavyoendana na hii sera.
Yah walimu wenyewe hawaielewi hii kitu,ukienda primary school ukaelezea hili jambo wanakutolea mimacho tu,Mimi shahidi wa hilo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom