Je, Rais Magufuli afuate ushauri wa Mzee Ibrahim Kaduma na kurudisha nyumba za Serikali alizouza? Je, aombe msamaha?

JokaKuu

Platinum Member
Jul 31, 2006
30,527
55,213
..Mzee Ibrahim Kaduma alitoa ushauri kwamba Jpm arudishe nyumba za serikali zilizouzwa na kuisabbaishia serikali hasara.

..Kufuatia Prof.Tibaijuka kurudisha fedha za Escrow, je ni wakati muafaka kwa Jpm naye kurudisha nyumba za serikali alizotwaa yeye mwenyewe, na zile alizouzia wengine?

Mwanasiasa mkongwe nchini, Ibrahim Kaduma amemshauri Rais John Magufuli kurejesha nyumba za Serikali zilizouzwa kwa watu binafsi wengi wao wakiwa waliokuwa watumishi wa umma, akisema ndiyo njia ya “kujisahihisha”.

Kaduma, ambaye amewahi kuwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Serikali ya Awamu ya Kwanza, aliyasema hayo wiki iliyopita katika mahojiano maalumu na gazeti hili kuhusu mambo kadhaa juu ya mwenendo wa CCM na Serikali yake katika kipindi ambacho chama hicho kimeadhimisha miaka 39 tangu kianzishwe.

“Kitu muhimu ambacho namshauri Rais, ni kuzirudisha nyumba za Serikali. Uuzaji wake haukuwafurahisha Watanzania walio wengi. Asimamie urudishaji huo ila afanye hivyo baada ya kutunga sheria ya maadili ya utumishi wa umma,” alisema.

Nyumba hizo za Serikali ziliuzwa wakati wa Serikali ya Awamu ya Tatu, chini ya Rais Benjamin Mkapa kwa usimamizi wa Dk Magufuli wakati huo akiwa Waziri wa Ujenzi.

Alimtaka Rais Magufuli kurejea kitabu kilichoandikwa na Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere cha ‘Tujisahihishe’ kwa yeye mwenyewe kuanza kujisahihisha kwa kurejesha nyumba ya Serikali aliyoinunua kwa utaratibu ule.

Alishauri kabla ya kufanya hivyo, Rais Magufuli atengeneze Sheria ya Maadili ya Taifa ambayo itamwambia kila mmoja amwogope Mungu na aseme ukweli wa mali wanazomiliki jinsi walivyozipata.
Advertisement

“Tujisahihishe maana yake kwa kiroho ni kutubu, Magufuli yeye mwenyewe angeanza kwa kutubu kwa wananchi, aeleze wazi kuwa CCM iliwakosea Watanzania (katika suala la uuzaji wa nyumba za Serikali).

Waziri huyo wa zamani wa mambo ya nje, alisema ili CCM iendelee kushika dola, haina budi kuirudia misingi iliyowekwa na waasisi wake ambayo imeachwa.

Alibainisha kuwa chama hicho kilirithi misingi ya vyama vya ukombozi vya Tanu na ASP, hivyo kinatakiwa kujitathmini kama kinatekeleza matakwa yaliyokusudiwa ya kuwakomboa Watanzania na kuwawezesha kupiga hatua ya maendeleo kwa wakati na kujikwamua kiuchumi.

“Taasisi yoyote yenye dhamira ya kuwaletea maendeleo wananchi wake ni lazima iwe na utamaduni wa kujitathmini. CCM ya sasa imepotoka na kusahau misingi yake. Endapo itarudi na kuisimamia, basi itatawala kwa muda mrefu ujao,” alisema.

Kaduma alisema kwa miaka kadhaa iliyopita, Taifa limesahau maadili ya uongozi na kujikuta likiyafumbia macho mambo yasiyofaa hasa yanapofanywa na viongozi wa Serikali.

Alitoa wito kwa wenye dhamana ya uongozi, kwa nafasi zao, kukubaliana juu ya maadili na misingi ya Taifa ili kwa pamoja, kusukuma gurudumu la maendeleo.

“Nchi hii tumeheshimu unafiki kuliko ukweli kwa kusahau maadili na misingi. Ni lazima tukae kama Taifa na tukubaliane juu ya namna tutakavyoiongoza nchi yetu,” alisema.

Wakati Rais Magufuli akikaribia kutimiza siku 100 tangu aingie madarakani, Mzee Kaduma aliwataka Watanzania kuendelea kumuunga mkono akisema tayari ameonyesha kuwajali na kuwafanyia kazi kama alivyoahidi.

Alisema amejitahidi kubana matumizi ya Serikali, kuongeza ukusanyaji wa mapato na kuboresha huduma za jamii jambo ambalo mbali na kurejesha heshima ya nchi, litasaidia kuwapunguzia Watanzania umaskini.

“Kufuta safari za nje kwa watendaji wa Serikali kumewaudhi wengi kwa sababu walikuwa wanalipana fedha nyingi sana. Lakini hivi ndivyo tulivyoishi enzi za Mwalimu. Magufuli hana makuu na anawatetea wanyonge, nawaomba sana Watanzania tumuunge mkono.”

Akizungumzia majukumu ya mkuu wa nchi katika utekelezaji wa utawala bora na demokrasia, Mzee Kaduma alisema ipo haja ya kufanya marekebisho katika baadhi ya sheria.

Alisema ni wakati muafaka sasa wa kuirekebisha Sheria ya Uchaguzi ili kutenganisha majukumu ya kiserikali na kichama kwa Rais.

“Tunahitaji Rais huru ambaye hatakuwa na minyororo ya chama chake ili atuongoze kwa umoja wetu. Yafaa matakwa ya mgombea kutokana na chama cha siasa yaondolewe ikiwa ni pamoja na kuzuia Rais kuwa mwenyekiti wa chama. Endapo Rais atakuwa huru, ataweza kuwaita wenyeviti wa vyama na kuzungumza nao bila upendeleo wowote,” alisema.

Pamoja na maoni hayo, alisema hana shaka na uongozi wa Rais Magufuli. “... Anafanana na Mwalimu Julius Nyerere. Wote wanawajali maskini na walifanya kila wawezalo ili kuwakomboa kutoka kwenye minyororo yote iliyofunga uhuru wao, iwe kiuchumi au kijamii, ili kuwafanya wafurahie rasilimali za Taifa lao.”

Kaduma aliungana na wadau wengine ambao wanapinga kurudiwa kwa uchaguzi wa Zanzibar kwa maelezo kuwa maridhiano baina ya pande zinazosigana yana nafasi nzuri ya kutatua mgogoro uliopo.

“Katika suala la Zanzibar nadhani CCM tungekubali kushindwa. Mimi ni mwanaCCM lakini nasema tungekubali kushindwa. Ningekuwa (Dk Ali Mohamed) Shein ningelinda heshima yangu maana hii ni hatari,” alisema.

Mzee Kaduma alisema kwa kuwa suala la Zanzibar ni baina ya vyama vya CCM na CUF, mtu pekee wa kutafuta ukweli ni mwenyekiti wa CCM.

“Rais mstaafu Jakaya Kikwete ndiye mwenye uwezo mkubwa wa kuweka mambo ya Zanzibar sawa maana yeye ndiye mwenyekiti wa CCM na suala lenyewe linakihusu CCM na CUF, ingawa kwa mbali sana Magufuli naye anaweza kufanya lolote kuondoa tatizo lililopo,” alisema.

Alisema anaamini CCM ingetenda haki kama ingepokea matokeo kama yalivyokuwa ambayo hata waangalizi wa ndani na nje wamesema hayakuwa na dosari.

“Ni vyema Rais Shein angekubali kushindwa. Chama pia kingefanya hivyo. Huko ndiko kujisahihisha. Kufanya hivyo Rais Shein angeondoka na heshima yake.”

Kuhusu hatua ya Serikali kuonekana kuminya uhuru wa vyombo vya habari kwa kufungia baadhi ya magazeti, Mzee Kaduma alisema: “Kama unataka kushinda ufisadi na rushwa, ni lazima vyombo vya habari viwe huru... ila waandike katika misingi iliyowekwa na inayokubalika kisheria.”

Akieleza jinsi vitendo vya rushwa na ufisadi vilivyotamalaki nchini kwa miaka ya hivi karibuni, alisema ili kufanikisha suala hilo ni lazima wadau wote washirikishwe.

Alisema suala hilo linahitaji ushiriki wa mihimili yote ya dola bila kusahau umuhimu wa vyombo vya habari. “Vita ya rushwa na ufisadi itapiganwa vyema endapo kutakuwa na uhuru wa habari na vyombo vyake. Kitu muhimu ni uwapo wa sheria makini ambayo itazingatiwa na kila mmoja. Naishauri Serikali itekeleze suala hili ili kila Mtanzania atoe mchango wake,” alisema.
 
Hakuna ufisadi na uhujumu uchumi mkubwa kama zoezi la uuzwaji Wa nyumba za serikali atakuja kiongozi ipo siku atazirejesha zote.Wameuziana nyumba za umma zenye maeneo potential kwa thamani ya nyumba za nyasi za kijijini tena unalipa kwa installment.Ingekuwa kweli dhamira ya kupambana na uhujumu uchumi na ufisadi ni ya dhati wangeanzia hapa.
 
Naamini Magufuli hakuuza nyumba, lilikua wazo la serikali na yeye alizinunua.

Kama ni tutaenda kwa busara, ushauri ni kwa Magufuli kuzinunua hizo nyumba kwa bei ile ile. Kwa maana kama ulinunua nyumba kwa shilingi milioni 50, serikali inakirudishia pesa zako unarudisha nyumba kwa NHC kama nyumba ilikua ya NHC. Kea kifupi nyumba irudi kuwa mali ya serikali.
 
..Mzee Ibrahim Kaduma alitoa ushauri kwamba Jpm arudishe nyumba za serikali zilizouzwa na kuisabbaishia serikali hasara.

..Kufuatia Prof.Tibaijuka kurudisha fedha za Escrow, je ni wakati muafaka kwa Jpm naye kurudisha nyumba za serikali alizotwaa yeye mwenyewe, na zile alizouzia wengine?
Uamuzi wa kutwaa nyumba za serikali, sio uamuzi wa Magufuli, ni uamuzi wa serikali, yeye alikuwa ni mtekelezaji tuu.
Japo naunga mkono ushauri wa Mzee Kaduma, mmoja wa wana CCM wachache waliokuwa na uadilifu wa Nyerere, lakini pia nafahamu uwezo wa serikali yetu, hauna the capacity ya kuzitwaa tena, kufuatia development iliyofanywa kwenye nyingi ya nyumba hizo, kwa vile waliogawiwa waligawiwa kihalali, kuzitwaa tena itapaswa walipwe fidia, fedha ambazo serikali yetu hauwezi kuwa nazo hata baada ya miaka 100!.

P
 
Uamuzi wa kutwaa nyumba za serikali, sio uamuzi wa Magufuli, ni uamuzi wa serikali, yeye alikuwa ni mtekelezaji tuu.
P
Hata uamuzi kuwa pesa za Escrow hazikuwa uhujumu uchumi wala pesa za serekali haukuwa wa Rugemalira ulikuwa uamuzi wa serekali na Rais Kikwete alitamka hivyo siku anaongea na wazee wa Dar e salaam.

Amini usiamini siku moja atakuja 'kichaa' mwingine atatumbua waliouza nyumba za serekali
 
..ulikuwa ni uamuzi wa KIFISADI.

..sasa hivi anauwezo na mamlaka ya kurudisha nyumba za serikali kama kweli alikuwa hakubaliani na uamuzi ule.

cc misasa
Una ushahidi ambao hauna mashaka juu ya ufisadi uliofanyika mkuu?

Cc jokakuu
 
..Mzee Ibrahim Kaduma alitoa ushauri kwamba Jpm arudishe nyumba za serikali zilizouzwa na kuisabbaishia serikali hasara.

..Kufuatia Prof.Tibaijuka kurudisha fedha za Escrow, je ni wakati muafaka kwa Jpm naye kurudisha nyumba za serikali alizotwaa yeye mwenyewe, na zile alizouzia wengine?
Huyu mzee kama yuko hai haifiki asubuhi lazima Atekwe
 
Hata uamuzi kuwa pesa za Escrow hazikuwa uhujumu uchumi wala pesa za serekali haukuwa wa Rugemalira ulikuwa uamuzi wa serekali na Rais Kikwete alitamka hivyo siku anaongea na wazee wa Dar e salaam.

Amini usiamini siku moja atakuja 'kichaa' mwingine atatumbua waliouza nyumba za serekali
Ndio maana CCM itatawala milele ili kuzuia vichaa wasije kuishika ikulu yetu, halafu wakaleta ukichaa kama huo.
P
 
Back
Top Bottom