Lukaku marata
JF-Expert Member
- Dec 4, 2019
- 448
- 752
Habari za humu wanaForum,
Kwanza kabisa nitoe pole kwa watanzania wote katika msiba huu mzito wa rais wetu mstaafu Benjamin WIlliama Mkapa. Niende moja kwa moja katika suala langu labda nitapata mawazo ya kunisaidia katika muktadha mzima wa maisha yangu kwani ninaamini humu kuna watu mbali mbali wenye uzoefu mbalimbali na wameshapitia mambo mengi magumu na makubwa tena zaidi yangu.
Kiumri nina miaka 26, ninaishi hapa Dar es Salaam nikijishughulisha na shughuli za hapa na pale. Katika maisha yangu kuanzia nilipokuwa chuo miaka 20 nilijiingiza katika mapenzi ya jinsia moja nikiwa ninafanya kama mfanyaji (yaani katika hii society anaitwa “Top”)
Katika kujiingiza kwangu katika huu mchezo sijui hata hiyo nguvu ilitoka wapi japo mwanzoni nilikuwa naogopa ila kutokana na mitandao hii ya kijamii imefanya nikutane na watu ambao tunafanya nao hayo mapenzi, kimsingi katika nchi yetu hata hapa Dar es Salaam watu wanaofanya ni vijana ages ya 20’s to 30’s ambao mimi nilikuwa ninakutana nao japo pia kuna watu wazima mimi hao nilikuwa sipendi kuwa nao.
Tena unakuta hawa vijana huwezi gundua kwamba wanajihusisha na haya mapenzi ya jinsia moja kwa sababu hana viashiria vyoyote vya kuonekana kike au la wengine nikiwemo mimi tuna mademu kabisa lakini bado hivi vitendo vinafanyika.Watu wanaweza dhani kwamba ni tamaa ya pesa lakini kwa watu niliokutana nao 70% hawafanyi sababu ya kusosa hela hiyo inadhihirisha kuwa tamaa ya pesa ndo chanzo,mpaka naandika uzi huu nimeshakutana na watu 20 ambao tumefanya nao haya mambo.
Lengo la kuanzisha huu uzi, kimsingi mimi nimechoka kufanya hivi vitendo kwani ninajua ninaikosea nafsi yangu,Mungu wangu,wazazi wangu na wale watu wote ambao wananiheshimu kwani hukiniona huwezi dhania kabisa kwamba ninafanya huu uchafu nina marafiki wengi tu lakini hakuna hata mmoja anayejua,wengi wanaonijua ni ambao nipo nao kwenye hii industry ambao nikiwa ninawaambia mimi nataka niache haya mambo wananiambia siwezi acha wakisema ninaweza kupunguza lakini sio kuacha.
Maana nimekutana na watu wengi sana kila nikijaribu kuwaambia nataka niache wanasema watu wamejaribu kuacha lakini inashindikana wakisema wengine wamesha wahi hata kwenda makanisani kuombewa lakini wapi,wengine washawahi mpaka kutoa kafara za wanyama lakini wapi.
Sasa nilichoamua naomba ushauri wenu mnisaidie labda ninaweza kupata mawazo tofauti kutoka kwenu because kwa kule nilipokuwa naomba ushauri wote tupo kwenye same boat labda ndo maana wanasema siwezi. Kati ya vitu nilivyokuwa ninafikiria kufanya:
1. Kwenda kwa watu wa psychology labda nikapate ushauri may be
2.Kujitoa uhai maana mateso ninayopata nafsini mwangu najua mimi na roho yangu
NOTE:
Huu uzi hauna lengo la kuvutia mtu yoyote katika hayo mambo,napia najua kuna watu watakuja hapa kunitukana na etc lakini niwaambie kitu kama wewe ni kijana unaweza kupata mtoto akawa anahiyo changamoto au hata pia mzazi wako yupo kwenye haya mambo au kama wewe ni mzazi na una mtoto wa kiume huwezi jua maana mimi hata wazazi wangu hakuna anayejua hata ndugu zangu so takecare
Kwanza kabisa nitoe pole kwa watanzania wote katika msiba huu mzito wa rais wetu mstaafu Benjamin WIlliama Mkapa. Niende moja kwa moja katika suala langu labda nitapata mawazo ya kunisaidia katika muktadha mzima wa maisha yangu kwani ninaamini humu kuna watu mbali mbali wenye uzoefu mbalimbali na wameshapitia mambo mengi magumu na makubwa tena zaidi yangu.
Kiumri nina miaka 26, ninaishi hapa Dar es Salaam nikijishughulisha na shughuli za hapa na pale. Katika maisha yangu kuanzia nilipokuwa chuo miaka 20 nilijiingiza katika mapenzi ya jinsia moja nikiwa ninafanya kama mfanyaji (yaani katika hii society anaitwa “Top”)
Katika kujiingiza kwangu katika huu mchezo sijui hata hiyo nguvu ilitoka wapi japo mwanzoni nilikuwa naogopa ila kutokana na mitandao hii ya kijamii imefanya nikutane na watu ambao tunafanya nao hayo mapenzi, kimsingi katika nchi yetu hata hapa Dar es Salaam watu wanaofanya ni vijana ages ya 20’s to 30’s ambao mimi nilikuwa ninakutana nao japo pia kuna watu wazima mimi hao nilikuwa sipendi kuwa nao.
Tena unakuta hawa vijana huwezi gundua kwamba wanajihusisha na haya mapenzi ya jinsia moja kwa sababu hana viashiria vyoyote vya kuonekana kike au la wengine nikiwemo mimi tuna mademu kabisa lakini bado hivi vitendo vinafanyika.Watu wanaweza dhani kwamba ni tamaa ya pesa lakini kwa watu niliokutana nao 70% hawafanyi sababu ya kusosa hela hiyo inadhihirisha kuwa tamaa ya pesa ndo chanzo,mpaka naandika uzi huu nimeshakutana na watu 20 ambao tumefanya nao haya mambo.
Lengo la kuanzisha huu uzi, kimsingi mimi nimechoka kufanya hivi vitendo kwani ninajua ninaikosea nafsi yangu,Mungu wangu,wazazi wangu na wale watu wote ambao wananiheshimu kwani hukiniona huwezi dhania kabisa kwamba ninafanya huu uchafu nina marafiki wengi tu lakini hakuna hata mmoja anayejua,wengi wanaonijua ni ambao nipo nao kwenye hii industry ambao nikiwa ninawaambia mimi nataka niache haya mambo wananiambia siwezi acha wakisema ninaweza kupunguza lakini sio kuacha.
Maana nimekutana na watu wengi sana kila nikijaribu kuwaambia nataka niache wanasema watu wamejaribu kuacha lakini inashindikana wakisema wengine wamesha wahi hata kwenda makanisani kuombewa lakini wapi,wengine washawahi mpaka kutoa kafara za wanyama lakini wapi.
Sasa nilichoamua naomba ushauri wenu mnisaidie labda ninaweza kupata mawazo tofauti kutoka kwenu because kwa kule nilipokuwa naomba ushauri wote tupo kwenye same boat labda ndo maana wanasema siwezi. Kati ya vitu nilivyokuwa ninafikiria kufanya:
1. Kwenda kwa watu wa psychology labda nikapate ushauri may be
2.Kujitoa uhai maana mateso ninayopata nafsini mwangu najua mimi na roho yangu
NOTE:
Huu uzi hauna lengo la kuvutia mtu yoyote katika hayo mambo,napia najua kuna watu watakuja hapa kunitukana na etc lakini niwaambie kitu kama wewe ni kijana unaweza kupata mtoto akawa anahiyo changamoto au hata pia mzazi wako yupo kwenye haya mambo au kama wewe ni mzazi na una mtoto wa kiume huwezi jua maana mimi hata wazazi wangu hakuna anayejua hata ndugu zangu so takecare
