Je, niache Bsc. Busness Information Tech niende Education?

Je, niache Bsc. Busness Information Tech niende Education?

bunyua

Member
Joined
Dec 29, 2018
Posts
16
Reaction score
15
Mimi ni mhitimu wa kidato cha sita ila sina uelewa wowote kwenye kozi mana hatukupewa elimu yoyote kuhusu kozi, Sasa nimechaguliwa UDSM -Bsc.Busness information tech, ila sielewi hii kozi badae nakua mtu gani.

Hapa nafikiri nibadili kozi niende education, mana inaeleweka nitakuwa mwalimu labda badae, ila nikafikiri nipate ushauri wa kina nisije kuwa nimeacha kozi nzuri au mbaya pia na pia ningeomba utaratibu wa kubadili kozi mnisaidie.
 
Ila mimi hapo kwa uelewa wangu inawezekana ukawa mtu wa IT kwa upande wa biashara. Muhimu ni wewe kujua kujiongeza na kuweza kumudu vizuri inayofundishwa na pia kutafuta uko mtandaoni.
Jua sana kuichezea computer utatusua hata kwa kujiajiri.
 
Kama unapenda IT itakufaa, jiandae kusoma programming, databases, website design etc kama haupend kabisa technology Basi kasome education. Remember technology inahitaji Sana kujiongeza.

Na sio lazima ukimaliza uajiriwe. Unaweza kujiajiri pia. Kama mtu ambae anafanya na kutengeneza miradi mbalimbali ya kibiashara ya kisasa
 
Kwani wamekuchagua kozi ambayo hukuichagua wewe?
 
Chuo hawawez kukuchagua katika course flani kama wewe mwenyewe hukuchagua iyo course
 
Yani kama unaenda ualimu unajitafutia umaskini wa kudumu ndg
 
Aisee ukienda natanguliza pole kama utahama hiyo course
Mimi ni mhitimu wa kidato cha sita ila sina uelewa wowote kwenye kozi mana hatukupewa elimu yoyote kuhusu kozi, Sasa nimechaguliwa UDSM -Bsc.Busness information tech, ila sielewi hii kozi badae nakua mtu gani.

Hapa nafikiri nibadili kozi niende education, mana inaeleweka nitakuwa mwalimu labda badae, ila nikafikiri nipate ushauri wa kina nisije kuwa nimeacha kozi nzuri au mbaya pia na pia ningeomba utaratibu wa kubadili kozi mnisaidie.
 
Usibadili COURSE, stand with it utakua na future nzuri ukiendelea nayo, Education huwezi kufananisha na Buss Info.
 
Back
Top Bottom