Je ni Shule gani nzuri ya boarding ya Shule ya msingi ?

Je ni Shule gani nzuri ya boarding ya Shule ya msingi ?

Akilinjema

JF-Expert Member
Joined
Aug 9, 2016
Posts
11,428
Reaction score
11,846
Nina mtoto wa ndugu yangu ana umri wa takriban miaka 10 ni wa kiume, tumemtoa kijijini alikokuwa anaishi na baby Na Bibi Yake mzaa mama yake, lengo la kumchukua ni kutaka asome na kuondokana mazingira ambayo yangempekea hata kujifunza Wizi n.k !

Sasa tumeishi naye sasa Kwa miaka miwili tumeshambadilisha Shule mbili anatosoma Kwa sasa ni ya tatu ambazo zote ni Shule za kutwa, lakini pamoja na umri wake kuwa mkubwa lakini maendeleo Yake ya darasani ni madogo sana tena ya kukatisha tamaa, amewekewa hadi twisheni lakini haijaweza kusaidia hadi sasa,

Mtoto ni mtukutu kupita kiasi , anapiga watoto wa Watu shuleni, ni muongo, hapendi kusoma, hesabu rahisi hajui, yani tunafikiria kumrudisha kijijini tumeshamjulisha babu Yake na mama Yake kuwa Temu hii iliyobaki asipobadilika namrudisha yani ukitaka asikukere usifuatilie mambo Yake ya Shule nyumbani penyewe acheni tu jamani!

Sasa ningependa Kama kuna Shule ya boarding ya watoto watukutu tumpeleke huko Mimi niko radhi kwenda kukopa ada yake aende tu wakagangaike nae hadi aelewe na kujitambua!
 
Kwa sasa yuko darasa la kwanza ktk Shule ya kawaida tu baada ya kuona Shule ya English medium hela ilikuwa inapotea bure! Yani ktk umri huo akiwa darasa la kwanza lakini bado anashindwa kuelewa masomo jamani
 
Nilishawahi kumpiga mara tatu lakini Kwa sasa nilishaacha mtoto ni nunda sijawahi kuona aisee!
 
Labda kama unataka kumpeleka boarding ili kukwepa kero zake. Ila mtoto wa umri huo si sahihi kumpeleka boarding, na kwa tabia hizo atazidi kuwa worse huko boarding na kujifunza matabia mengine, anahitaji malezi ya ukaribu.
 
Boarding anaenda kukutana makundi..
utundu ndo utazid..mnyooshe mwenyewe ...fimbo inahusika apo...
 
Labda kama unataka kumpeleka boarding ili kukwepa kero zake. Ila mtoto wa umri huo si sahihi kumpeleka boarding, na kwa tabia hizo atazidi kuwa worse huko boarding na kujifunza matabia mengine, anahitaji malezi ya ukaribu.

Nakubaliana na Wewe kabisa Ila palipofikia nikipata nafasi ya boarding naona bora aende ili kuondokana na kero zake!
 
Nakubaliana na Wewe kabisa Ila palipofikia nikipata nafasi ya boarding naona bora aende ili kuondokana na kero zake!
Ni afadhali ujaribu kufix kero zake akiwa bado mdogo kuliko aendelee na hizo tabia na huko boarding ataongeza tabia nyingine. Trust me akibalehe na hujamrekebisha itakuwa balaa, mtamsusa kabisa. Mrekebishe sasa hivi na uwe nae karibu
 
Ni afadhali ujaribu kufix kero zake akiwa bado mdogo kuliko aendelee na hizo tabia na huko boarding ataongeza tabia nyingine. Trust me akibalehe na hujamrekebisha itakuwa balaa, mtamsusa kabisa. Mrekebishe sasa hivi na uwe nae karibu

Sawa ila Ndiyo maana Mimi naona bora tumrudishe tulikomtoa kuliko kuendelea kukaa nae akija kushindwa masomo tusijelaumiwa kuwa tumemuachia bila kumfuatilia na kumjali
 
Mtoto miaka 10 alitakiwa awe darasa la 4 Au 5 , yeye yuko la kwanza darasani ndo mkubwa kuliko wote maradufu lakini maendeleo yamekuwa Sawa na sifuri
 
St. Plasdus Mvimwa Primary School. Ipo Sumbawanga vijijini kama unaweza jitoe ufahamu tu
 
Umepigwa Mara Ngapi Mpaka Ulivyokuwa Na Akili Njema ?
Heritage Iko Poa

Sent from my VFD 301 using JamiiForums mobile app

Bila Shaka Mara nyingi aisee?! Tena Mimi hadi Niko sekondari mama alikuwa na kanuni zake zake hizo ukienda kinyume nazo ni adhabu! Mathalani hata Kama ulikuwa kanisani ukachelewa kurudi ni adhabu tu alikuwa anataka kila ukifika saa 12 jioni uwe nyumbani with no any excuse unless uwe shuleni labda!

Kwa mkuu Kama nimekuelewa vyema unamaana niendelee kumbutua hadi atakapojitambua? Ila unajua kumpiga Mtu kunachosha hata Wewe unaepiga unakuta nafsi inakuwaje sijui!
 
Au nimpeleke kituo cha polisi sijui wakaongee nae niliwaza hivyo Kwa uzuri tu
 
Au nimpeleke kituo cha polisi sijui wakaongee nae niliwaza hivyo Kwa uzuri tu
Kuna jela sijui ni shule ya watoto watukutu, ilikuwepo dar karibu na regency hospital sina uhakika kama bado ipo. Mpeleke huko
 
mmmh! jamani!! huyo hata boarding hatakaa watamfukuza hawawezi kuvumilia mtoto wa hivyo.
Mtafutieni za day muwe mnamdhibiti wenyewe, huko asije hata akaanza "mchezo mchafu"
 
Back
Top Bottom