Kuna jambo linahitaji kutazamwa kwa jicho la tatu. Mara kwa mara tumekuwa tukisikia baadhi ya viongozi wakisisitiza kuwa Watanzania waliopo nje ya nchi au wanaokosoa mwenendo wa serikali wanatumika na “mabeberu.” Kauli hizi zimekuwa zikitumika kama njia ya kuzima hoja badala ya kujibu hoja zenyewe.
Lakini tukijiuliza kwa undani: Je, kila anayekosoa ni adui wa taifa? Au ni raia anayejali mustakabali wa nchi yake?
Vilevile, viongozi hawa hawa wanapozungumza juu ya “kutunza amani” kwa kuwatisha wananchi kwamba machafuko yakitokea hawatakuwa na pa kukimbilia, ni muhimu kujiuliza ukweli uliopo nyuma ya pazia. Wananchi wa kawaida hawana njia mbadala lakini je, viongozi wenyewe hawana access ya kusafiri muda wowote? Wengine wana pasipoti za nchi nyingine, mali nje ya nchi, na fedha kwenye mabenki ya kimataifa.
Mfano wa wazi ni Andry Rajoelina ambaye alishawahi kuhusishwa na uwekezaji na maisha ya nje ya nchi wakati wa uongozi wake. Hili linaonyesha kuwa hali hii si ya Tanzania pekee.
Swali la msingi linabaki: Je, ni haki kwa viongozi kuwaambia wananchi wabaki watulivu kwa gharama yoyote, huku wao wakiwa na “plan B” za maisha nje ya nchi?
Nchi haiwezi kujengwa kwa hofu, bali kwa uwazi, uwajibikaji, na kuheshimu maoni tofauti. Kukosoa si uhaini ni sehemu ya demokrasia.
Wananchi wanapaswa kupewa nafasi ya kuuliza, kujadili, na kushiriki kikamilifu bila kuwekewa lebo au vitisho. Amani ya kweli inatokana na haki, si ukimya wa kulazimishwa
Lakini tukijiuliza kwa undani: Je, kila anayekosoa ni adui wa taifa? Au ni raia anayejali mustakabali wa nchi yake?
Vilevile, viongozi hawa hawa wanapozungumza juu ya “kutunza amani” kwa kuwatisha wananchi kwamba machafuko yakitokea hawatakuwa na pa kukimbilia, ni muhimu kujiuliza ukweli uliopo nyuma ya pazia. Wananchi wa kawaida hawana njia mbadala lakini je, viongozi wenyewe hawana access ya kusafiri muda wowote? Wengine wana pasipoti za nchi nyingine, mali nje ya nchi, na fedha kwenye mabenki ya kimataifa.
Mfano wa wazi ni Andry Rajoelina ambaye alishawahi kuhusishwa na uwekezaji na maisha ya nje ya nchi wakati wa uongozi wake. Hili linaonyesha kuwa hali hii si ya Tanzania pekee.
Swali la msingi linabaki: Je, ni haki kwa viongozi kuwaambia wananchi wabaki watulivu kwa gharama yoyote, huku wao wakiwa na “plan B” za maisha nje ya nchi?
Nchi haiwezi kujengwa kwa hofu, bali kwa uwazi, uwajibikaji, na kuheshimu maoni tofauti. Kukosoa si uhaini ni sehemu ya demokrasia.
Wananchi wanapaswa kupewa nafasi ya kuuliza, kujadili, na kushiriki kikamilifu bila kuwekewa lebo au vitisho. Amani ya kweli inatokana na haki, si ukimya wa kulazimishwa