Je ni lini wa-bara wataongoza Zanzibar?

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,299
33,082
Wapendwa Wakuu

Muundo wa uongozi Tanzania unaelekea kuibua maswali mengi. Pamoja na kuwa tumo ndani ya Muungano bado Watanzania Bara hawana nafasi ya Uongozi huko Zanzibar.

Juzi tumeshuhudia Zanzibar imepata Rais na Makamu wawili wa Rais wote wazanzibar. Je kwanini Wa-bara hakuna hata mmoja huko Zanzibar?

Lakini: Wazinzabar wanatawala Bara, na kuwatungia sheria Wa bara. Tunaona makamo wa Rais Mzanzibar, wabunge wengi tu Wazanzibar; na Mawaziri kadha kutoka Zanzibar watatangazwa hivi karibuni KUJA KUWAONGOZA WA-BARA. ILIHALI HAKUNA HATA WAZIRI MMOJA WA HUKO ZANZIBAR AMBAYE ANATOKA BARA.

Je, kama Tanzania ni moja ni lini Wa-Bara watatawala Zanzibar kama wa Zanzibar wanavyotawala Bara?

Mimi Binafsi napata maswali mengi; ninapoona hakuna hata MBUNGE mmoja Msukuma huko Zanzibar

Tutarajie nini kwa mfumo huu?

Nakaribisha maoni Yenu Asanteni.
 
Wapendwa Wakuu

Muundo wa uongozi Tanzania unaelekea kuibua maswali mengi. Pamoja na kuwa tumo ndani ya Muungano bado Watanzania Bara hawana nafasi ya Uongozi huko Zanzibar.

Juzi tumeshuhudia Zanzibar imepata Rais na Makamu wawili wa Rais wote wazanzibar. Je kwanini Wa-bara hakuna hata mmoja huko Zanzibar?

Lakini: Wazinzabar wanatawala Bara, na kuwatungia sheria Wa bara. Tunaona makamo wa Rais Mzanzibar, wabunge wengi tu Wazanzibar; na Mawaziri kadha kutoka Zanzibar watatangazwa hivi karibuni KUJA KUWAONGOZA WA-BARA. ILIHALI HAKUNA HATA WAZIRI MMOJA WA HUKO ZANZIBAR AMBAYE ANATOKA BARA.

Je, kama Tanzania ni moja ni lini Wa-Bara watatawala Zanzibar kama wa Zanzibar wanavyotawala Bara?

Mimi Binafsi napata maswali mengi; ninapoona hakuna hata MBUNGE mmoja Msukuma huko Zanzibar

Tutarajie nini kwa mfumo huu?

Nakaribisha maoni Yenu Asanteni.

Maswali ni mengi, je Zanzibar wanachangia kwa uwiano uliosawa bajeti ya muungano au Tanzania bara ndio wanawabeba tu wazanzibar?. Kama ni hivyo kwa nini wawabebe wakati ni nchi inayojitawala? Ingekuwa mkoa wa Tanzania bara sawa, lakini ni nchi inayojitegemea hivyo sijui kama kuna usawa katika kuchangia bajeti ya muungano
 
Wenyewe ni wengi mno kutawala , sasa na sisi tukisema tutawale, si zitakuwa ni vurugu. Tukiona wanakosea we are ready kuwakosoa.
 
Karata zilizochezwa wakati wa kuunda "Tanzania" zilizaa utata ufuatao: Zanzibar ni nchi ndani ya muungano - Tanzania bara si nchi bali ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kama ilivyo Zanzibar . Kwa "equation" hii ni wazi wazanzibari wanaweza kuongoza bara kwani ni raia wa 'Zanzibar" na pia ni raia wa "Tanzania". Si rahisi kwa mtanzania kutoka bara kuongoza Zanzibar kwani yeye ni raia wa Tanzania lakini si raia wa Zanzibar!
 
Mathematically

Muungano =Zanzibar+Bara

but

Bara>>>>Zanzibar

therefore

Bara{zanzibar} and not Zanzibar{Bara}

For that reason Bara{zanzibar} will exist and Zanzibar{Bara} will not exist
"impossible set" or true "Null set"

However Bara kuiongoza zanzibar is logicless, kwa sababu sehemu ndogo ndio huhitajika kuiongoza sehemu iliyo kubwa and not vise versa. (i.e kikundi kidogo cha watu kitaongoza kundi kubwa na sio kundi kubwa liongoze mtu moja au kikundi kidogo cha watu)

So,
Bara will need Zanzibar na Zanzibar will not need Bara. Hence proved

Japo ni kinyume cha katiba buti kwa maslai fluani fulani ya kichama na kitaifa itaaminika iwe hivyo. But in reality Katiba lazima iheshimiwe.
 
Mathematically

Muungano =Zanzibar+Bara

but

Bara>>>>Zanzibar

therefore

Bara{zanzibar} and not Zanzibar{Bara}

For that reason Bara{zanzibar} will exist and Zanzibar{Bara} will not exist
"impossible set" or true "Null set"

However Bara kuiongoza zanzibar is logicless, kwa sababu sehemu ndogo ndio huhitajika kuiongoza sehemu iliyo kubwa and not vise versa. (i.e kikundi kidogo cha watu kitaongoza kundi kubwa na sio kundi kubwa liongoze mtu moja au kikundi kidogo cha watu)

So,
Bara will need Zanzibar na Zanzibar will not need Bara. Hence proved

Japo ni kinyume cha katiba buti kwa maslai fluani fulani ya kichama na kitaifa itaaminika iwe hivyo. But in reality Katika lazima iheshimiwe.

Kwa majibu yako ni kuwa sisi Wabara hatuwezi kuwaongoza Wazanzibar?
 
Karata zilizochezwa wakati wa kuunda "Tanzania" zilizaa utata ufuatao: Zanzibar ni nchi ndani ya muungano - Tanzania bara si nchi bali ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kama ilivyo Zanzibar . Kwa "equation" hii ni wazi wazanzibari wanaweza kuongoza bara kwani ni raia wa 'Zanzibar" na pia ni raia wa "Tanzania". Si rahisi kwa mtanzania kutoka bara kuongoza Zanzibar kwani yeye ni raia wa Tanzania lakini si raia wa Zanzibar!

Kama ni hivyo kwa nini kila leo Wazanzibari hawaachi kulalamika kuwa wanatawaliwa na Watanganyika ? Hivi sasa wana Raisi wao, Makamu Raisi wawili wao na huku Tanganyika wanaye Makamu wa Raisi. Kwa mahesabu rahisi ni kuwa kati ya viongozi wakuu (maraisi) wanne ndani ya Jamhuri ya Tanzania, watatu wanatoka Zanzibar ! Hii ina maana kwamba kila wakaazi 250,000 huko Zanzibar wanamtoa Raisi wakati huku Tanganyika ni Raisi moja kwa wakazi 40,000,000 ! Talk of the absurdity of it all !!
 
Kwa majibu yako ni kuwa sisi Wabara hatuwezi kuwaongoza Wazanzibar?

Sina uhakika ila labda uhakika tutaupata katika historia ya uongozi wa Zanzibar kama waliwahi kuwepo wabara. May be wakati wa Nyerere otherwise sidhani kama ipo au itakuwepo tena.
 
Wa Bara hawataongoza Zanzibar kwani hiyo ni nchi inayojitegema kwa kuwa na raisi wake, na hamna nchi kama Tanzania Bara "Tanganyika" ilikwenda na maji na kumezwa na Tanzania wakati wa muungano hivyo sidhani kama itakuwa rahisi kwa Mbara kushika hatamu Zanzibar.
 
Karata zilizochezwa wakati wa kuunda "Tanzania" zilizaa utata ufuatao: Zanzibar ni nchi ndani ya muungano - Tanzania bara si nchi bali ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kama ilivyo Zanzibar . Kwa "equation" hii ni wazi wazanzibari wanaweza kuongoza bara kwani ni raia wa 'Zanzibar" na pia ni raia wa "Tanzania". Si rahisi kwa mtanzania kutoka bara kuongoza Zanzibar kwani yeye ni raia wa Tanzania lakini si raia wa Zanzibar!

Unapotaja Tanzania ni ' Tanganyika na Zanzibar''. Kama ungetumia maneno hayo hoja yako ingeskosa mashiko. Zanzibar ni sehemu ya JMT vinginevyo Zanzibar ni Zanzibar na Tanganyika ni Tanganyika. Unaposema Tanzania tayari umeshaua Tanganyika na Zanzibar. Hakuna nchi inayoitwa Tanzania bila Zanzibar au Tanganyika. Kwahiyo raia wa Tanzania ni wale wa Tanganyika na Zanzibar. Kama Zanzibar ni nchi, Tanganyika imefia wapi? na kama hakuna Tanganyika,Tanzania inatoka wapi?
 
Ahsante mtoa hoja!! Wabara kutawala Zanzibar ni mpaka pale tutakapofumbua hili fumbo" Chao ni chao kwa nini?Na chetu ni chao kwa nini? Lakini chao si chetu kwa nini??
 
Nadhani it is a question of minority and majority. Zanzibar ni kanchi kadogo sana ikilinganishwa na Tanganyika (Tanzania Bara). Hata idadi ya watu zanzibar haizidi idadi ya watu kwa jiji la DSM. Kutokana na ukweli huo, wazanzibari wanajisikia wamemezwa zaidi kwenye muungano kuliko tunavyojisikia sisi waTZ bara. Sasa, inapotokea mTZ bara anaenda kuongoza zanzibar hali ya kujisikia kumezwa ndiyo inakuwa kubwa zaidi. Hivyo, ndivyo ninavyofikiri kwamba wazee wetu waasisi wa muungano walitaka waepushe manung'uniko miongoni mwa wazanzibari ya kujisikia wamemezwa. Kumbuka hata wazo la kuungana lilitolewa na Nyerere. Hivyo, Mwl. alikwepa kuonekana ana agenda ya kuimeza zanzibar.

Pamoja na hayo, kama kutakuwa na 'national dialogue' ya kuwa na katiba mpya, itakuwa ni muhimu pia suala la muungano likajumuishwa ili kuweka fursa ya wananchi ambao ndiyo wadau wakuu wa muungano kutoa mawazo yao ya namna ya kuuboresha.
 
Kama ni hivyo kwa nini kila leo Wazanzibari hawaachi kulalamika kuwa wanatawaliwa na Watanganyika ? Hivi sasa wana Raisi wao, Makamu Raisi wawili wao na huku Tanganyika wanaye Makamu wa Raisi. Kwa mahesabu rahisi ni kuwa kati ya viongozi wakuu (maraisi) wanne ndani ya Jamhuri ya Tanzania, watatu wanatoka Zanzibar ! Hii ina maana kwamba kila wakaazi 250,000 huko Zanzibar wanamtoa Raisi wakati huku Tanganyika ni Raisi moja kwa wakazi 40,000,000 ! Talk of the absurdity of it all !!
Hivi kweli eeh!, unajua linawezekana hili ni taifa la viongozi. Inawezekana wenzetu wamebarikiwa kutawala, kati ya viongozi wakuu 5 wa nchi yetu 3 wanatoka Z'bar na 2 ndio bara. Z'bar inawatu wasiozidi 1mil na bara si chini 40mil du!, halafu majaji wakuu wote Z'bar. Hawa jamaa wana kipaji cha uongozi.
 
Sasa mnasema mnaibeba Znz, na ni mzigo, kwanini hamuitui?

Ukweli ni kwanza hata waznz pia hawawataki, sasa cha kujiuliza ni nani ana-provide 'gundi' ya huu Muungano? CCM na now CUF..sasa hao ndio wakuulizwa.
 
Tatizo ni katiba ambayo hairuhusu asiye mkazi/ mzanzibari kugombea nafasi yoyote huko Zanzibar. Ndo maana wanasema kuwa ni nchi inayojitegemea lakini ukisema Tanganyika ni nchi vilvile unaweza kunyongwa kwani utaitwa mhaini. Mkuu haya ni mapungufu kama yalivyo mengine ndani ya katiba zetu. Niulize kwanini Tanganyika tusiwe na serikali yetu badala ya kutumia ila ya muungano?
 
Sasa mnasema mnaibeba Znz, na ni mzigo, kwanini hamuitui?

Ukweli ni kwanza hata waznz pia hawawataki, sasa cha kujiuliza ni nani ana-provide 'gundi' ya huu Muungano? CCM na now CUF..sasa hao ndio wakuulizwa.

Kila siku huwa nasema, Wazanzibar ondokeni bara muone kama mtu atawafuata. Nusu yenu mnaishi na kufanya kazi bara, wabara walioko znz si zaidi ya 5,0000. Kwahiyo, ni simple kama hamtaki muungano, fungeni maduka, acheni ajira za bara, rudisheni mashamba na majengo, enendeni kwa amani mkaijenge nchi yenu. period!
 
Binafsi nafikiri kuwa, endapo tunahitaji kuleta uwiano sawa, ni vema kuangalia mambo makuu matatu yafuatayo
  • Pato la taifa: Je shughuli za bara na Zenji zinachangiaje kwa pamoja kwenye pato la taifa. Na mgawanyo wa rasilimali na nafasi za uongozi ziendane na kigezo hicho kwanza
  • Idadi ya watu: Idadi ya watu iwe sehemu muhimu katika kuleta mgawanyo huu, lakini pia (LABDA) tunaweza kuongeza kiwango cha umaskini ili kuleta uwiano wa maendeleo kwa Tanzania
  • Maeneo kimkakati! Hili ni suala nyeti, lakini ni vema kujua - na kwa pamoja kukubaliana kwa kiwango gani Zenji ina-ihitaji bara na vivyo hivyo bara kwa Zenji. Suala la kujiuliza hapa ni je Zenji ni strategic area - eneo mkakati kwa bara? Hapa ndo itabidi kubainisha maslahi ya kila eneo
Kisha tusema kwa mfumo huu, tunahitaji wabara wakatawale Zenji! Bila shaka ni vema hiyo inafikiriwa endapo tunahitaji umoja huo, ambao kwa sasa binafsi naona unaelekea kuzikwa
 
Back
Top Bottom