jogi
JF-Expert Member
- Sep 25, 2010
- 25,558
- 25,323
Katika moja ya hotuba zake Mwalimu Julius Kambarage Nyerere alipata kusema "......katika utawa wangu yapo mambo mazuri tulifanya, lakini pia yapo mambo ya hovyo hovyo tulifanya! Ndiyo tulifanya!!! Sisi ni binadam tulifanya! "
Mwalimu alisema katika hotuba ile kuwa alitarajia kuwa tawala baada yake zingeyachukua yoote mazuri yaliyofanywa na utawala wake na kuyaendeleza huku yale ya hovyo hovyo yakitupiliwa mbali.
Akistaajabia kuzikwa kwa azimio la arusha akasema anashangaa kuona mambo mazuri waliyoyafanya ndio yanaachwa na yale ya hovyo hovyo ndio tunayaendeleza.
Tayari mziki wa Dar mpaka Dom unarindima.
Je, Mwalimu alitumia vigezo vipi kulinganisha jambo la hovyo na jambo zuri?
Kwa muktadha huo, tumejithibitishiaje kuwa tunaendeleza jambo zuri la Mwalimu Nyerere la kuhamia Dodoma (ambalo halikutekelezwa kwa kwenye zama za Mwalimu, Mwinyi, Mkapa na Kikwete)
Au tunaendeleza jambo la hovyo na tunashindwa kumwambia Amiri jeshi mkuu wetu?
Mwalimu alisema katika hotuba ile kuwa alitarajia kuwa tawala baada yake zingeyachukua yoote mazuri yaliyofanywa na utawala wake na kuyaendeleza huku yale ya hovyo hovyo yakitupiliwa mbali.
Akistaajabia kuzikwa kwa azimio la arusha akasema anashangaa kuona mambo mazuri waliyoyafanya ndio yanaachwa na yale ya hovyo hovyo ndio tunayaendeleza.
Tayari mziki wa Dar mpaka Dom unarindima.
Je, Mwalimu alitumia vigezo vipi kulinganisha jambo la hovyo na jambo zuri?
Kwa muktadha huo, tumejithibitishiaje kuwa tunaendeleza jambo zuri la Mwalimu Nyerere la kuhamia Dodoma (ambalo halikutekelezwa kwa kwenye zama za Mwalimu, Mwinyi, Mkapa na Kikwete)
Au tunaendeleza jambo la hovyo na tunashindwa kumwambia Amiri jeshi mkuu wetu?