Habari zenu wana JF.
Jamani, nimepanga nyumba moja hapa Dar toka January, lakini cha kusikitisha ni kwamba Bill ya maji inayokuja kwetu imekuwa majanga sasa kwa miezi mitatu. Mwezi wa kwanza bili ilikuja elfu 70, mwezi wa pili ikaja elfu 60 na mwezi huu umekuja elfu 80. Mwezi uliyopita tulienda DAWASCO kuuliza kwanini tunalipa bili kubwa hivi wakasema ni matumizi yetu.
Ila kiukweli ni kwamba, tuko wapangaji watatu tu na wote tunafunga milango asubuhi tunapoenda kazini sasa inakuwaje matumizi yanakuwa hivi. Pliz wadau naombeni msaada tufanye nini au ni kwa sababu gani bili yetu inakuwa kubwa kiasi hicho?
Je ni bili yetu au tunapewa bili ya mteja mwingine? Kumbuka pale sisi wote ni single ila moja tu ana mfanyakazi, wengine hatuna. Je tatizo ni nini? Michango yenu ndio ukombozi wetu jamani labda kuna mwingine/wengine wanapata shida kama hii ya kwetu.
NOTE: Tumeuliza mwenye nyumba kama labda alikuwa na bili nyuma akasema kuwa ali clear kabla hatujapanga kwake.
Mchango wenu tafadhali.
Jamani, nimepanga nyumba moja hapa Dar toka January, lakini cha kusikitisha ni kwamba Bill ya maji inayokuja kwetu imekuwa majanga sasa kwa miezi mitatu. Mwezi wa kwanza bili ilikuja elfu 70, mwezi wa pili ikaja elfu 60 na mwezi huu umekuja elfu 80. Mwezi uliyopita tulienda DAWASCO kuuliza kwanini tunalipa bili kubwa hivi wakasema ni matumizi yetu.
Ila kiukweli ni kwamba, tuko wapangaji watatu tu na wote tunafunga milango asubuhi tunapoenda kazini sasa inakuwaje matumizi yanakuwa hivi. Pliz wadau naombeni msaada tufanye nini au ni kwa sababu gani bili yetu inakuwa kubwa kiasi hicho?
Je ni bili yetu au tunapewa bili ya mteja mwingine? Kumbuka pale sisi wote ni single ila moja tu ana mfanyakazi, wengine hatuna. Je tatizo ni nini? Michango yenu ndio ukombozi wetu jamani labda kuna mwingine/wengine wanapata shida kama hii ya kwetu.
NOTE: Tumeuliza mwenye nyumba kama labda alikuwa na bili nyuma akasema kuwa ali clear kabla hatujapanga kwake.
Mchango wenu tafadhali.