Je, mwaka huu 2019 hakuna Waraka wa Pasaka (Easter Note)?

Je, mwaka huu 2019 hakuna Waraka wa Pasaka (Easter Note)?

Interest

JF-Expert Member
Joined
Apr 11, 2015
Posts
3,434
Reaction score
7,091
Tumeshazoea kila ikifika msimu wa sikukuu za kidini, basi hutoka nyaraka kutoka kwa taasisi mbalimbali za kidini ambazo huwa na lengo la kuionya jamii na kushauri mambo ambayo yatadumisha amani na upendo nchini.

Naamini utamaduni huu mzuri bado unaendelea na pengine tunahitaji zaidi nyaraka hizi hasa katika kipindi hiki ambacho nchi yetu inapitia katika hali mbaya ya kiuchumi na wasiwasi mkubwa.

Mwaka jana, ulitoka waraka kutoka kwa KKKT ambao kidogo ulileta mtafaruku baina ya Serikali na taasisi hiyo ambapo ilifikia hatua Serikali kuagiza Kanisa hilo kufuta waraka wao kwa madai ya uchochezi.

Sasa, tumeingia mwaka 2019 na leo ni Sikukuu ya Pasaka.. Sijasikia waraka wowote mpaka wakati huu..

Naomba kama upo tuuwasilishe humu ili tuendelee kujitazama na kujiponya kiroho na kijamii!

Heri ya Pasaka!
 
Fuatilia maudhui ya mahubiri ya pasaka kutoka kona mbalimbali za nchi kisha unganisha utapata waraka!
 
Fuatilia maudhui ya mahubiri ya pasaka kutoka kona mbalimbali za nchi kisha unganisha utapata waraka!
Hii siyo kawaida lakini.. Huwa kuna waraka maalum unatolewa na tunatangaziwa kabisa!
 
Wadhani wao hawaogopi yalowapata akina askofu niwemugizi wa jimbo katoliki la Rulenge?? Alihojiwa uraia wake na misukosuko kibao ilifuatia apo, sasa wadhani hawaliogopi ilo???

Waache bhana wapumzike as long as sisi Watanzania hasa vijana hatuonyeshi kuchukua hatua stahiki juu ya jinsi tunavyoongozwa kwan nao wana mioyo ya nyama na c chuma ngoja tuendelee kunyooshwa mkuu wangu
 
Wadhani wao hawaogopi yalowapata akina askofu niwemugizi wa jimbo katoliki la Rulenge?? Alihojiwa uraia wake na misukosuko kibao ilifuatia apo, sasa wadhani hawaliogopi ilo???

Waache bhana wapumzike as long as sisi Watanzania hasa vijana hatuonyeshi kuchukua hatua stahiki juu ya jinsi tunavyoongozwa kwan nao wana mioyo ya nyama na c chuma ngoja tuendelee kunyooshwa mkuu wangu
Umeandika kwa hisia sana mkuu. Kwahiyo viongozi waache tu kutimiza wajibu wao kwa kuhofia watawala?

Manabii na mitume wangekuwa waoga hivi....!!
 
Tunaingia Easter muda si mrefu kwa 2020. Napo hatutakuwa na Waraka?
 
Uandike hujipendi!! ma pasta wetu, wachungaji, maaskofu wetu hadi hao wanaojiita manabii hofu tupu..ni kitete

..eti Nabii gani unaogopa mtawala? Ndiyo maana tunasema hawa ni wachungaji wa sisi kondoo wa bwana... manabii walikuwa kina Daniel, kina Yohana Mbatizaji yaani anakatwa kichwa lakini anachokiamni kinabakia palepale.

Nabii gani TRA wakitimgisha kidogo chalii ha ha ha
 
Tumeshazoea kila ikifika msimu wa sikukuu za kidini, basi hutoka nyaraka kutoka kwa taasisi mbalimbali za kidini ambazo huwa na lengo la kuionya jamii na kushauri mambo ambayo yatadumisha amani na upendo nchini.

Naamini utamaduni huu mzuri bado unaendelea na pengine tunahitaji zaidi nyaraka hizi hasa katika kipindi hiki ambacho nchi yetu inapitia katika hali mbaya ya kiuchumi na wasiwasi mkubwa.

Mwaka jana, ulitoka waraka kutoka kwa KKKT ambao kidogo ulileta mtafaruku baina ya Serikali na taasisi hiyo ambapo ilifikia hatua Serikali kuagiza Kanisa hilo kufuta waraka wao kwa madai ya uchochezi.

Sasa, tumeingia mwaka 2019 na leo ni Sikukuu ya Pasaka.. Sijasikia waraka wowote mpaka wakati huu..

Naomba kama upo tuuwasilishe humu ili tuendelee kujitazama na kujiponya kiroho na kijamii!

Heri ya Pasaka!
Waraka ume potezwa na askofu Munga.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom