Je, mmegundua mchezo "strategist" wa CCM na serikali walioucheza?

mcfm40

JF-Expert Member
Nov 2, 2010
4,452
3,151
Ni hivi. Katika mkutano wa bunge la February, 2017, wabunge walitoka wakiwa kitu kimoja, wote CCM na Ukawa, kiasi cha hata kuachiana muda wa kuchangia hoja bungeni.

Kuna mambo yaliyotokea hasa la Makonda ambayo yalifanya bunge zima kuongea kwa sauti moja dhidi ya serikali.

Ilionekana kwamba kama bunge hili la bajeti lingeanza na moto ule ule basi serikali ya Magu ingekuwa katika wakati mgumu sana. Wabunge wote CCM na upinzani walipanga kuichachafya hii serikali kweli kweli.

Ili kipunguza huo umoja ulioanza kujijenga baina ya wabunge katika kuikosoa serikali, ndipo mastrategist wa CCM na serikali wakahakikisha wanafufua bifu kati ya Wabunge wa Cccm na vyama vya upinzani. Lengo ni kuhakikisha wabunge wa ccm watasimama kuitetea serikali dhidi ya hoja za upinzani. Na lengo pia ni kuwakumbusha wabunge wa ccm kuwa mpinzani na adui yao ni Ukawa hasa chadema na sio serikali. Na hivyo hawapaswi kuungana na upinzani dhidi ya serikali. Hili linaonekana kufanikiwa ukiangalia jinsi kikao cha jana kilivyokwenda na jinsi wabunge wa Ccm walivyowafanyia undava wabunge wa chadema.

Kwa hiyo tutegemee mivutano baina ya ccm na upinzani ikitawala katika bunge hili la bajeti huku hoja zenye mwelekeo wa kuwaunganisha wabunge dhidi ya serikali zikipewa nafasi ndogo kabisa!

In fact, hata kuteuliwa kwa Kitila huko serikalini ni katika harakati za kupunguza mashambulizi yaliyokuwa dhahiri yanakwenda kuitikisa serikali. Watu kama kina Zitto weshalainika tayari.

Nina hakika si wabunge wa chadema wala ccm waligundua kuwa wanakuwa manipulated kwa malengo maalum.

Maelekezo waliyopewa wabunge wa Ccm kuwakataa wabunge wa EALA wa chadema lilikuwa na lengo tu la kuamsha bifu na hasira baina ya upinzani na wabunge wa Ccm ili isitokee tena wazungumze lugha moja dhidi ya serikali!

Hivyo tutegemee "business as usual" katika bunge hili la bajeti! Ndiooo... kwa kila pendekezo la serikali!

Ni hayo tu! Hii nchi ngumu sana!
 
Mkuu ebu edit kidogo UZI wako

Lakini una hoja za MSINGI ndio maana tunasema kuitoa CCM madarakani ni ngumu mno....maana kuna VICHWA VINAFIKIRI IPASAVYO KUWAPUMBAZA UPINZANI NA mwisho wa siku UPINZANI wanacheza ngoma ya CCM kiulaini bila kulazimishwaa.....wanakuja shtuka hiuo hapo 2020 WANABAKI KUCHUKUA MAKAPI YA CCM....

Badala ya wao kutumia muda huo kutangaza sera zao wao watatumia muda huo KUWASAFISHA MAKAPI na kutumia muda mwingi kujitetea ili hali CCM inatumia muda huo kuonyesha mazuri waliyo yafanya NA KUNADI SERA ZAO ipasavyo.....SASA UNAFIKIRI NI MTANZANIA GANI MPUUZI atawachagua UPINZANI??

Na sasa hivi tunataka kutengeza UGOMVI wa LISSU na EDO ili wakifika 2020 wawe tayari ni VIPANDE VIPANDE.....sisi kwa ulaini majimbo yote yetu......MPAKA AKILI ZENU ZIKAE SAWA...

Mchawi mkubwa wa UPINZANI kwa sasa ni HUYO M/KITI wenu......wala si CCM. CCM wanatumia MWANYA WA HUYO ZERO BRAIN kuwapiga ipasavyo..
 
Mkuu ebu edit kidogo UZI wako
Lakini una hoja za MSINGI ndio maana tunasema kuitoa CCM madarakani ni ngumu mno....maana kuna VICHWA VINAFIKIRI IPASAVYO KUWAPUMBAZA UPINZANI NA mwisho wa siku UPINZANI wanacheza ngoma ya CCM kiulaini bila kulazimishwaa.....wanakuja shtuka hiuo hapo 2020 WANABAKI KUCHUKUA MAKAPI YA CCM....badala ya wao kutumia muda huo kutangaza sera zao wao watatumia muda huo KUWASAFISHA MAKAPI na kutumia muda mwingi kujitetea ili hali CCM inatumia muda huo kuonyesha mazuri waliyo yafanya NA KUNADI SERA ZAO ipasavyo.....SASA UNAFIKIRI NI MTANZANIA GANI MPUUZI atawachagua UPINZANI???????
Nimejitahidi kuedit mkuu> Hizi simu kidogo zinasumbua katika uandishi!
 
Mkuu ebu edit kidogo UZI wako
Lakini una hoja za MSINGI ndio maana tunasema kuitoa CCM madarakani ni ngumu mno....maana kuna VICHWA VINAFIKIRI IPASAVYO KUWAPUMBAZA UPINZANI NA mwisho wa siku UPINZANI wanacheza ngoma ya CCM kiulaini bila kulazimishwaa.....wanakuja shtuka hiuo hapo 2020 WANABAKI KUCHUKUA MAKAPI YA CCM....badala ya wao kutumia muda huo kutangaza sera zao wao watatumia muda huo KUWASAFISHA MAKAPI na kutumia muda mwingi kujitetea ili hali CCM inatumia muda huo kuonyesha mazuri waliyo yafanya NA KUNADI SERA ZAO ipasavyo.....SASA UNAFIKIRI NI MTANZANIA GANI MPUUZI atawachagua UPINZANI???????
Na sasa hivi tunataka kutengeza UGOMVI wa LISSU na EDO ili wakifika 2020 wawe tayari ni VIPANDE VIPANDE.....sisi kwa ulaini majimbo yote yetu......

Kwani Tanzania huwa kuna Uchaguzi?
 
Tatizo la chadema mnajua kila kitu kiasi kwamba hata Mbowe akiamua kutoondoka kwenye uenyekiti hakuna wa kumpinga
Mjomba jitahidi kujikita kwenye mada husika , kila dk kumtaja mtu mmoja tu hakutakusaidia kitu .

Kwa mtu fukara na masikini kama wewe bilionea Mbowe hutamuweza , Kikwete alichemsha , Magufuli kwa kumtumia Daudi Bashite na polisi wote wa Tanzania ameshindwa vibaya sana ! Sasa mtu duni kama wewe utaishia kuchanika mbavu tu , achana na hili jabali utaumia .
 
Mkuu ebu edit kidogo UZI wako
Lakini una hoja za MSINGI ndio maana tunasema kuitoa CCM madarakani ni ngumu mno....maana kuna VICHWA VINAFIKIRI IPASAVYO KUWAPUMBAZA UPINZANI NA mwisho wa siku UPINZANI wanacheza ngoma ya CCM kiulaini bila kulazimishwaa.....wanakuja shtuka hiuo hapo 2020 WANABAKI KUCHUKUA MAKAPI YA CCM....badala ya wao kutumia muda huo kutangaza sera zao wao watatumia muda huo KUWASAFISHA MAKAPI na kutumia muda mwingi kujitetea ili hali CCM inatumia muda huo kuonyesha mazuri waliyo yafanya NA KUNADI SERA ZAO ipasavyo.....SASA UNAFIKIRI NI MTANZANIA GANI MPUUZI atawachagua UPINZANI???????
Na sasa hivi tunataka kutengeza UGOMVI wa LISSU na EDO ili wakifika 2020 wawe tayari ni VIPANDE VIPANDE.....sisi kwa ulaini majimbo yote yetu......
Hii ni kwa faida ya taifa au nani, maana nchi inazidi kuporomokea korongoni.
 
Sasa unalaumu nini? Ama unatakiwa serikali isitafute namna ya kucalm, na serikali inapokuwa fragile unafikiri nani atalaumiwa na wananchi? Serikali ama hao wahuni wachumia tumbo wanaojiita wapinzani?. Serikali inayo wajibu mkubwa wa kuhakikisha kuna amani na utulivu kwa kila kitu kwahiyo we tulia tu. Kama una familia size yako ni familia, serikali ndo nchi yenyewe
 
Tatizo la wabunge wa Ccm hawana focus. Baada ya kufanya makosa ndipo wanapo kuja kujutia. Issue kama ya uchaguzi wa wabunge wa east Afrika ni jambo la aibu sana wabunge wa Ccm wamefanya. Na kwa mtindo huu usitegemee Tanzania kuendelea
 
Magufuli alimteuwa Prof Mkumbo ili kuuwa nguvu ya JK Bungeni jana

Akili za Watanzania ni ngumu sana, wanaona bora waishi maisha magumu lakini ccm wasiitoe madarakani
 
Magufuli alimteuwa Prof Mkumbo ili kuuwa nguvu ya JK Bungeni jana

Akili za Watanzania ni ngumu sana, wanaona bora waishi maisha magumu lakini ccm wasiitoe madarakani
Wewe nae sijui umetoka shimoni......Unafahamu KITILA aliteuliwa lini?????na ni nani kakuambia MAGUFULI namuogopa KIKWETE?????
 
Nimesoma huu Uzi una maana na umeona mbali lakn em editing au touch imekua ngumu maaana kuna maneno yamepindaaa
 
Sioni ubaya ktk kuteuliwa prof Kitila Mkumbo.Yeye hakuwa mbunge hivyo hahusiani lolote na upinzani au ccm kuunga mkono hoja dhaifu za serikali. Kuisimamia serikali ni kazi ya msingi ya wabunge. Wasipofanya hivyo kwa dhati ni kosa lao.Haijalishi ni upinzani au tawala.
 
Wewe nae sijui umetoka shimoni......Unafahamu KITILA aliteuliwa lini?????na ni nani kakuambia MAGUFULI namuogopa KIKWETE?????

Shangaa na wewe! Magufuli angekuwa anamwogopa Kikwete angemteua mkewe kuwa mbunge, si angemwacha amlee Mzee mstaafu?
 
Back
Top Bottom