Je, kweli CHADEMA ni mpango wa Mungu?

Je, kweli CHADEMA ni mpango wa Mungu?

Maseto

JF-Expert Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
944
Reaction score
546
Kwa siku za karibuni, Nimekuwa nikifuatilia kwa umakin sana maneno yanayozungumzwa na viongozi wa Chadema kwenye mikutano na kugundua kuwa wamekuwa wakimtaja Mungu mara kwa mara.

Wanaonekana kutuaminisha kuwa kila wanachofanya wanatumia nguvu za mungu.

Mungu hatumiwi kwa namna hiyo. MUNGU ANA MAHALI PAKE PA KUMTAJA TAJA.

Itafika wakati mtu akiruhusu kuwa tegemiz sana kwa Mungu hukosa uwezo wa kujituma ktk kufanikisha jambo eti Mungu hajamjalia.

Mungu husingiziwa kwa kila dosari au mafanikio.

Nashauri ktk majukwaa Mungu asitajwe kihivyo na chadema. Tuige mfano wa MWALIMU NYERERE alikuwa mhudhuriaji sana ibada lakini ktk majukwaa ya kisiasa hakumtaja Mungu.
 
Unamjua "Mungu" wanaomtaja chadema ? unafahamu kuna "Mungu" wengi?
 
Ukiacha kumshirikisha Mungu katika kila jambo utangoja sana.! Fuatilia hotuba za Rais Obama utaelewa kitu ninacho maanisha.. GOD BLESS CHADEMA, GOD BLESS TANZANIA
 
Kwani kuna tatizo gani? au wewe feemason? Mungu atatajwa kwa kuwa yeye ni kimbilio msaada na tumaini letu!
 
Hakuna Mungu wengi, kuna mungu wengi, tofautisha kati ya mungu na Mungu wewe! CDM wanamtaja Mungu
 
Wanataka wananchi wawaonee huruma...hizi njaa ni mbaya sana!
 
Wanataka wananchi wawaonee huruma...hizi njaa ni mbaya sana!

Mtabakia hivyohivyo huku Chadema inasonga mbele nyie mtabaki na matusiyenu na waganga wakienyeji wakina Long water
 
Mungu akitajwa unakereka sana ee?
 
Wanataka wananchi wawaonee huruma...hizi njaa ni mbaya sana!

kuelewa nako linatakiwa liwe ni somo jipya, me nadhani labda wanataka MUNGU awaonee huruma, kitu ambacho si kibaya hata kidogo, kwani hata na Wamarekani ambao ni mfano wa waliofanikiwa wameandika kabisa kwenye nembo ya taifa lao kuwa "IN GOD WE TRUST", pia katika wimbo wetu wa taifa tunasema "MUNGU IBARIKI AFRIKA...., MUNGU IBARIKI TANZANIA...", hivyo kama ni huruma ya MUNGU, wacha waitafute tu.
 
Wanataka wananchi wawaonee huruma...hizi njaa ni mbaya sana!

Unataka kumhodhi Mungu. Wacha roho mbaya, Kila mtu ana haki ya kuabudu na kutaja anachoamini. Mbona nyie mna Maji marefu na kamati za ufundi. Hata kuonewa huruma ni uungwana. Unataka wawachukie kama nyie.
 
Mungu ni kichaka cha wazembe na wanaotaka ku manipulate wenzao.
 
Yote yamedhihirika kilichobaki ni CDM kutembea na Kwaya kwenye majukwaa tu! Wacheze ndomboro ya Yesu na disco la Yesu! Wasio na macho waanze kuazima maana mambo yapo karibu!
 
kumbe hujajua kwanini cc chadema tunamwomba Mungu,this is becoz chama che2 ni cha kanisa, na ndiyo maana kwenye mikutano ye2 ha2kosi maaskofu wawili wa3.
 
Back
Top Bottom