Mkuu wangu NGANU, mdau wetu aliyeanzisha mada ni mshabiki wa SIMBA.
Maana kama kweli tunataka kuendeleza mpira na tunaona kwamba YANGA na SIMBA hazileti mabadiliko tufanyeje? Tuendeleze timu za mikoani ili zilete changamoto. Tayari AZAM wameleta changamoto nzuri. Mwaka jana walikuwa nambari 2 na YANGA ikawa nambari 3. Mwaka huu AZAM imekuwa nambari 2 na SIMBA imekuwa nambari 3.Nafikiri tunaelekea upande sahihi lakini huenda tukachelewa kufika. Maana hata Uingereza wanagombea kusajili wachezaji 'uwanja wa ndege' niambie mchezaji gani maarufu ambaye ametokana na akademi za michezo nchini Uingereza? SUAREZ, VAN PERSIE, CISSE, BA, CARZOLA, ARTETA, DZEKO, KUN AGUERO, DZEKO, wachezaji hao wote walisajiliwa 'uwanja wa ndege'. Ligi ya UJERUMANI: LEWANDOSKI, ROBEN, RIBERY, hao wote walisajiliwa 'uwanja wa ndege'. Ligi ya HISPANIA: CRISTIANO RONALDO, OZIL, BENZEMA, KHEDIRA, ALONZO, DI MARIA, NEYMAR, SANCHEZ, hao wote walisajiliwa 'uwanja wa ndege' Ingawa mpira ni mchezo, siku hizi mpira unalenga biashara zaidi. Ndo maana SAMATTA NA ULIMWENGU wako TP MAZEMBE, wakati MBUYU TWITE ametoka KONGO anacheza Tanzania! Naomba kuwasilisha.