Je kuna masharti ya kuvaa SUTI?

Je kuna masharti ya kuvaa SUTI?

Mbwa kama inakukimbiza haitakiwi ukimbie

Na hata jua liwake vipi haitakiwi uvue koti
 
Ukivaa Suti Hutakiwi Kutembea Umbali Wa 1Km Kwa Miguu!
 
lile ni vazi laheshima jamani sio lakujivalia valia ovyo tu. nazani ayo ni sawa tu yame masharti yakwe kwamana ukiangalia kweli ni sawa suti sio vazi lakuchezea chezea tu vigezo na masharti huzingatiwa. suti iheshimike.
 
Ukivaa suti huruhusiwi kutongoza demu "bikra".
 
Hapo kwenye kutokuongea kiswahili na kulilia change wengine mbona hatutovaa suti mpaka siku ya mwisho ndio wanatununulia
 
Ukivaa suti.
Usikimbilie daladala
Usipande bodaboda
Usinywe safari beer
Usivute sigara
Ukichukua taxi uziulize bei mpaka mwisho wa safari.
Ukivaa suti kama wewe ni mzee wa kanisa usiibe sadaka wakati wa kuhesabu wala usiweke masharti kwamba lazima ununuliwe chips kukuk na soda ndio uhesabu sadaka.
Ukiwa unavaaga suti mara kwa mara usiwe na nyumba ndogo uswahilini. atakuletea shombo
 
Sharti mtu akikuomba hela lazima umpe lasi ivyo jamaa atakuzalau sana utasikia hawa wahuni tu mara ndio wanakuaga majambazi
 
Back
Top Bottom