Je kuna maprofesa na madokta (PhD) jeshini??

Duh, basi wako kimya sana, hawajioneshi!
 
Habari.
Nilitaka kujua maana sijawahi waona wala kusikia hawa 'wasomi' ktk nyanja ya jeshi eidha jwtz au polisi au jeshi lolote!
Wa kutosha sana tu (hasa JWTZ). Kamishna general wa magereza mwenyewe ana PhD (Dr. Malewa). Juzi tu pale rais anatoa kamisheni Arusha umesikia zile takwimu pale kulikuwa na Masters za kutosha sana tu.
 
Acha uongo....magereza mwanamke?You are not serious, uhamiaji ndo ke
 
Mkuu yote umetiririka vyema, ila hili la mkuu wa jeshi la magereza kusema ni mwanamke ni uongo wa mchana kweupe.
Sema kama ulikuwa ukimaanisha mkuu wa jeshi la uhamiaji hapo sawa.
 
Habari.
Nilitaka kujua maana sijawahi waona wala kusikia hawa 'wasomi' ktk nyanja ya jeshi eidha jwtz au polisi au jeshi lolote!

prof major general Dr yodan mtalima kohi alikaa COSTECH kama mkurungezi kwa miaka 13 ,ila Bwana mkubwa wa awamu ya nne alitengua uteuzi wake na kurudishwa Jeshini ,inasemekana utendaji mbovu wa walio chini yake na alishindwa kuiindeleza sayansi nchi kwa miaka yote hiyo aliyokuwa mtendaji mkuu wa chombo cha wanasayansi TZ ,Tetesi zingine kuwa bwana mkubwa alichukia aliposikia watendaji wa chini yake walikuwa wanatumia magari kwenye ishu za ujangili,mara jengo la serikali watumishi waliochini yake wakapaka rangi za matangazo ya kampuni fulani ya simu nk........ miaka ya mwisho ya utumishi wake alitumika vizuri kama mtabibu lugalo na kufanya vizuri sana kwenye fani yake.Pia inasemekana ni mtaalam pekee wa medical law TZ
 
Mkuu yote umetiririka vyema, ila hili la mkuu wa jeshi la magereza kusema ni mwanamke ni uongo wa mchana kweupe.
Sema kama ulikuwa ukimaanisha mkuu wa jeshi la uhamiaji hapo sawa.
Hakuna jeshi la uhamiaji, ile ni idara ya uhamiaji.

Kwanza nchi hii tuna jeshi moja tu JWTZ hivyo vingine ni vikosi tu.
 
Sio magereza mkuu... ni uhamiaji!!!
 
Wa kutosha sana tu (hasa JWTZ). Kamishna general wa magereza mwenyewe ana PhD (Dr. Malewa). Juzi tu pale rais anatoa kamisheni Arusha umesikia sole takwimu pale kulikuwa na Masters za kutosha sana tu.

Umeuliizwa PhD we unaleta habari za Masters
 
Hakuna jeshi la uhamiaji, ile ni idara ya uhamiaji.

Kwanza nchi hii tuna jeshi moja tu JWTZ hivyo vingine ni vikosi tu.
Kwa mujibu wa katiba yako au ya jamhuri ya muungano wa Tanzania
 
Kwa vile uprofesa hupatikana kwa kupanda cheo mtu mwenye PhD, uwezekano pekee ni mtu ambaye tayari ni profesa kutoka taasisi ya elimu ya juu kuingia jeshini akiwa tayari ni Profesa.
Si rahisi kihivyo lakini. PhD mtu akiwahi sana Itakuwa chini ya miaka 30. Kunaweza kuwa na exceptions chache. Kutoka PhD hadi Profesa kawaida ni miaka 9. Sasa mtu huyo kuingia jeshini atakuwa na miaka 40 tena yule aliwahi kabisa.
Hapo ndiyo Kuna kimbembe!
 
Yupo mmoja ni 2/c wa komandi ya Anga, jina kapuni. Mzee yule alianza kwa kuwa daktari (MD), then alivyoingia jeshi akachaguliwa akasomee uinjinia wa ndege (aeronautics engineering, ambapo ana masters kwenye upande huo!). Mpaka sasa jamaa ni brigedia jenerali (kama sijakosea).
Alafu mzee yule ukimuona wala huwezi mdhania..! Very social!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…