The Father of All
JF-Expert Member
- Feb 26, 2012
- 10,959
- 13,426
Dunia imeshuhudia na kushangilia 'kusainiwa' kwa mkataba wa amani almaaruf PEACE CONFERENCE 2025 kulikofanyika huko Sharm el Sheikh Misri. Japo hatuna uhakika wa kuleta majibu, maswali yanayosumbua ni kama ifuatavyo:
1) Je, Netanyahu na Trump wake wanaaminika?
2) Je, kama wataendelea na ujanja ujanja na ujambazi wao dunia itaendelea kuangalia bila kufanya lolote?
3) Je, wahuni hawa wameingia mkataba huu kuzima nguvu ya maandamano na upinzani dhidi ya mauaji ya kimbari ya Gaza au wameishiwa pumzi baada ya uchumi wa Israel kudorora na majeshi kuanza kuchoka vita?
4) Je, ni baada ya kujaribu kurejesha mateka wao na kushinda na kuamua kujitoa kimasomaso na kuepusha aibu kwa kujifanya wameshinda hivyo vita imekoma?
5) Je, itawezekana kupata suluhu wakati maigizo yote yaliwatenga wapalestina ambao ndiyo wenye ngoma yao?
Yetu macho na masikio.
Nawaza kichini chini na kupiga kelele kimya kimya Baba yenu.