Je, Idi Amin Alikuwa anakula Wanadamu?

Je, Idi Amin Alikuwa anakula Wanadamu?

Ashampoo burning

JF-Expert Member
Joined
May 12, 2023
Posts
1,296
Reaction score
3,929
Unajua Idi Amin? Watu wake walimuita Big Daddy, lakini maadui wake walimuita mzee wa buchani – “The Butcher”. Yaani huyu jamaa alitokea kule West Nile uganda kaskazini, Uganda, kijiji chenyewe hakijulikani jina, alikulia kwenye familia maskini chokaa balaa. Baba na mama wakatengana, akabaki kulelewaa na mama yake watoto wa mjini wanasema single maza, akiwa mdogo anahangaika kama watoto wengi wa mtaa kula kwa shida saana yaani.

Sasa elimu hakuwa nayo sana, yaani mpaka kijana wa miaka 21 bado hana direction. Ndo akamua kuingia jeshini, King’s African Rifles , jeshi la kikoloni la Waingereza. Wanasema alianza kama mpishi wa makande na supu ,yaani mpishi wa jeshi 😂, lakini jamaaa akapanda cheo fasta hadi kuwa mwanajeshi kamili.private

Akatumwa Somalia 1949 kupiga waasi, akaja Kenya kudhibiti Mau Mau. Lakini issue ikawa moja – Amin hakuwa tu askari, alikuwa na ukali kupita kiasi katili haswa. Watu walikuwa wanamwogopa interrogation zake. Waingereza walitaka kumshitaki, lakini badala yake wakampa cheo kingine! 1959 akawa “Afande” – cheo cha juu kabisa kwa askari mweusi wakati ule.

piai alikuwa bonge la bodybuilder mwili nyumba kipande cha mtu na bondia pia? Akawa bingwa wa ngumi Uganda kwa miaka mingi. Kwa hiyo alikuwa na nguvu, ukali, na sasa cheo kinapanda.

Uganda ikakaribia uhuru. Apo ndipo alipokutana na Apollo Milton Obote – kiongozi wa siasa. Wakaunganisha nguvu. Obote akawa Waziri Mkuu 1962 baada ya uhuru, Amin akapewa nafasi kubwa jeshini. Lakini, Amin alikuwa mtu wa maneno machache na vitendo vibaya. Alipopewa kazi ya kukomesha wizi wa ng’ombe Kaskazini, aliua watu hovyo mpaka Waingereza wakakasirika. Obote hakumfukuza, bali akamtuma Uingereza kwenda kusomea zaidi jeshi. Jamaa akarudi akiwa amekomaa zaidi.

1964 jeshi la Uganda likawa na mgomo, nani akaletwa kutuliza? Amin! Akawekwa Deputy Commander. Lakini bado alikuwa na michezo yake ya magendo – dhahabu, kahawa, na pembe za ndovu kutoka Congo za magendo kauza sana mzee baba iddy. Na Obote mwenyewe alikuwa ndani ya mchezo huu wa kuuza magendo kutoka congo.

1966 Obote akafumua serikali, akajiweka Rais. Akawa anamtegemea Amin kwa ulinzi. Amin sasa akawa Chief of Army and Airforce ***** yaani mkuu wa majeshi. Cheo kikubwa kuliko vyote. Lakini miaka ikasogea, Obote akawa anamshuku. Hasa baada ya jaribio la kumuua 1969. Alipojaribu kumshusha cheo Amin, hakufaulu. Obote kaenda safari Singapore 1971, huku nyuma mzee Amin akapiga coup d’état kiswahili akapindua serikali fasta. Akaweka serikali yake, akajipa majina marefu kama mzaha jina refu na ukikosea kulitamka kesi:

"Rais wa milele, Field Marshal Al-Hajji Dr. Idi Amin VC, DSO, MC, Bwana wa wanyama wa nchi na samaki wa bahari, mshindi wa Waingereza barani Afrika kwa ujumla na Uganda kwa ujumla."

Mara baada ya kuingia madarakani, akawa mkali mbaya. Viongozi wote waliokuwa tishio – Askofu Mkuu, Majaji, Chansela wa Makerere, wote akawamaliza. Jeshi likajaa wapiganaji wa kabila lake na wapiganaji wa zamani wa vita. Ndani ya miezi michache, damu ilikuwa ikimwagika kila upande.
General Idi Amin_Web.jpg
 
Amin akaanzisha State Research Bureau aka wasiojulikana wa uganda – kikosi cha kutesa na kuua wapinzani. Kila aliyeonekana upande wa Obote, basi kifo. Ilifika 1972, akawafukuza Waasia wote Uganda – Wahindi na wengine. Uchumi ukaporomoka vibaya sana, mpaka leo madhara bado yapo.

Mataifa ya Ulaya na Marekani wakawa wanamsema vibaya hadharani, lakini chini kwa chini bado walikuwa wana fanya nae biashara. Hypocrisy/unafiki ya dunia wa wazungu.

1976, ndege ya Kifaransa ikatekewa Entebbe na Wapalestina pamoja na wanaharakati wa Ujerumani. Amin akawa anashirikiana nao. Lakini Israeli wakaja wakafanya Operation Entebbe, wakawaokoa mateka. Amin akachanganyikiwa – akawaua wafanyakazi wa uwanja wa ndege, Wakenya aliowashuku, na hata mzee Mwingereza aliyekuwa hospitali.

Kufikia hapo, jina lake likawa rasmi: “The Butcher of Uganda.”au mzee wa buchani kwa kiswahili Wanasema aliuwa zaidi ya watu 300,000 wakati wa utawala wake – raia, viongozi, yeyote aliyemkosoa kidogo.

Lakini nguvu zikaanza kushuka. Watu wakakimbilia Tanzania, na Julius Nyerere akasema enough is enough. Amin akavamia Tanzania 1978 akitaka Kagera. Jamaa akashindwa vibaya sana. Nyerere akaungana na waasi wa Uganda, wakapiga mpaka Kampala. Amin akakimbia kama mwizi kibaka wa mbagala akiwa anafukuzwa na watu.

Alikimbilia Libya kwa Gaddafi, kisha akamalizia maisha yake Saudi Arabia, mpaka kifo chake 2003. Hakuwahi kushtakiwa wala kulipa kwa damu zote alizomwaga.


Swali moja lilikuwa linawatesa watu wa Uganda pamoja na dunia:
“Je, Idi Amin alikuwa anakula watu kweli?”

Yaani hili swali na kama movie ya kutisha nsyukaa hivi. Watu wengi uganda hasa wafanyakazi wa ikulu walikuwa wana hii story ya iddy amin kula watu.

Wakati anakunywa whisky na kutafuna mbuzi choma, maneno yakaanza: “Labda si mbuzi choma tu, labda ni nyama ya binadamu…” 😳hahaha maana kila mtu wa ikulu alikuwa na hiyo story .

Tuhuma zikazidi – walisema Amin alikuwa anakula maadui zake, wengine wakadai alikuwa na friji limejaa viungo vya watu. Kuna siku alimwambia mwandishi, “nyama ya binadamu ina chumvi nyingi sana” – statement iliyopelekea uvumi kuwa kweli jamaa alikuwa kanibali.


Si hivyo tu, inasemekana alikuwa akihifadhi vichwa vya maadui zake kama alama ya ushindi. Watu wakazidi kuamini kwamba Big Daddy alikuwa sio tu dikteta, bali pia mnyama aliyekuwa anakula wanadamu.

Kuna jamaa mmoja anaitwa Henry Kyemba – alikuwa mtu mkubwa serikalini enzi za Idi Amin, Waziri wa Afya kabisa. Yaani alikuwa karibu na Big Daddy kila siku, anashuhudia mambo moja kwa moja. Ya mzee iddi amin

Ndani ya hicho kitabu, akafichua uvumi uliokuwa ukizunguka kama moto wa porini: kwamba Amin hakuwa tu dikteta, bali pia alikuwa akihusishwa na ukanibalisti ulaji wa nyama za watu . Jamaa akasema kulikuwa nLakini mambo yalipozidi kuwa machungu – mauaji, mateso, na hofu kila kona – Kyemba akakimbia nchi, akatoroka kaacha vyeo vyote nae aliacha vyeo kama yule mcuba wetu wa tanzania hahah natania tu. Alipofika uhamishoni, akaandika kitabu mwaka 1977 kinaitwa “State of Blood”.

kwamba Big Daddy alikuwa anahifadhi vichwa vya maadui zake kwenye friji, na hata kuongelea nyama ya binadamu.
 
Wengi wanadai huo ulikuwa ni uzushi tu.

Wengine wanadai ni kweli alifanya hivyo kama sehemu ya desturi ya kabila lake; ukiua mtu, ili mzimu wake usikusumbue, inabidi ule sehemu ya mwili wake.

Kwa mfano, mimi nimekuwa kwenye Jamii ambayo ukiua nyoka, ulipaswa kumshika huyo nyoka mkiani au sehemu yoyote ya mwili wake ili usije ukamuota kwenye ndoto, ukaweweseka.
 
Back
Top Bottom