Je, huu sio uvunjaji wa haki za msingi za binadamu unaofanywa na serikali ya Magufuli?

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,468
113,583
Wanabodi,

Haki ni moja ya tunu kubwa na muhimu kwa taifa lolote, nchi ukiwa na haki, inabarikiwa, nchi ikikosa haki inalaaniwa.

Vivyo hivyo kwa Watawala, tumeshuhudia watawala wakitawala kwa haki, utawala wao ukibarikiwa, na watawala wakitawala kwa hila, utawala wao ukifitinishwa. Wamekuwepo watawala wenye nguvu sana wakiwemo Mafarao, Wafalme kama kina Nabukadreza, Belshaza, Suleiman, na wengine wengi, hivi sasa hawapo kutokana na kukosena haki kwenye utawala wao.

Kuna msanii wa muziki wa kizazi kipya wa enzi hizo akijiita Balozi Dola Soul, kwenye moja ya nyimbo zake aliweka kibwagizo "wengi walikuwepo na sasa hivi wako wapi?".


Huu ni mfululizo wa makala zangu za "Kwa Maslahi ya Taifa" ambazo zinaandikwa kwa mfumo wa swali au maswali ambayo yatafanya viongozi wetu kujitafakari, kwa maswali fikirishi, na wewe msomaji utapata majibu yako kwa kila mtu atakuwa na jibu lake.

Tanzania ni nchi ya kidemokrasia ya mfumo wa vyama vingi vya siasa, inayofuata katiba na utawala wa sheria!.

Ndani ya katiba ya JMT kuna vifungu rasmi vya haki za msingi za binaadamu!. Moja ya haki hizo ni kipengele hiki

Uhuru wa mtu
kwenda atakako
Sheria ya 1984
Na.15 ib.6
17
(1) Kila raia wa Jamhuri ya Muungano anayo haki ya kwenda kokote katika Jamhuri ya Muungano na kuishi katika sehemu yoyote, kutoka nje ya nchi na kuingia, na pia haki ya
kutoshurutishwa kuhama au kufukuzwa kutoka katika Jamhuri ya Muungano.
(2) Kitendochochote cha halali au sheria yoyote yenye madhumuni ya
(a) kupunguza uhuru wa mtu kwenda atakako na kumweka chini ya ulinzi au kifungoni; au
(b) kuweka mipaka kwa matumizi ya uhuru wa mtu kwenda anakotaka ili kutekeleza hukumu au amri ya mahakama;
au
(ii) kumlazimisha mtu kutimiza kwanza wajibu wowote anaotakiwa na sheria nyingine kuutimiza; au
(iii) kulinda manufaa ya umma kwa jumla au
kuhifadhi maslahi fulani mahususi au
maslahi ya sehemu fulani ya umma,
kitendo hicho hakitahesabiwa au sheria hiyo
haitahesabiwa kuwa ni haramu au ni kinyume cha ibara hii
Kama jambo hili ni kweli limefanyika,Kigogo wa BoT azuiwa Airport kutokana na kukosa vibali vya kusafiri nje ya nchi then
Haiwezekani mtu ambaye yuko huru, tena yuko likizo, ameamua kwenda kujipumzikia zake nchi za wenzetu, azuiliwe!. Huu ni ukiukwaji wa haki msingi za binaadamu.

Nafahamu kuna wafanyakazi wa serikali, na baadhi ya idara nyeti, au hata madakitari, jeshi, polisi na zimamoto, hata wakiwa likizo, wanawajibika kumtaarifu mwajiri wao, likizo yake atakuwa wapi, ili in case of anything, aweze kuwa reached out!, lakini kitendo cha maofisa uhamiaji, kumzuia mtu mwingine yoyote wa serikali, asisafiri nje ya nchi kwa safari binafsi, huu ni ukiukwaji wa haki za msingi za binaadamu zilizo ainishwa kwenye katiba yetu.

Pamoja na nia nzuri, na nia njema ya Rais wetu, Dr. John Pombe Magufuli, kudhibiti safari za nje ya nchi zisizo za lazima na ambazo hazina tija kwa taifa, utekelezaji wa amri hiyo, ni lazima uzingatie haki za msingi za binaadamu zilizotolewa na katiba yetu na kufuatwa kwa taratibu, sheria na kanuni, na sio kutekelezwa tuu kama zimamoto, na kukiuka haki za msingi za binadamu!.

Ila pia niliwahi kushauri humu, kama baadhi ya sheria, zinaweza kuwa ni kikwazo kwa rais wetu, kututengeneza Tanzania tunayoitaka, rais anayo mamlaka ya kisheria, kuandika waraka, 'decree' kuiweka kando katiba , hivyo kuitawala Tanzania kwa kutumia decree hivyo kuwa huru kufanya jambo lolote atakavyoona inafaa!


Mhe. Rais futilia mbali utawala wa sheria Ongoza Kwa Kutumia Decree tu!

Katiba ya nchi ndio sheria Mama, Viongozi wote wakuu wa umma, baada ya kuwachagua, tunawaapisha, wanakula kiapo cha utii wa katiba!, kwa kuapa watailinda na kuitetea katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kumuomba Mungu awasaidie.

Kama katiba inatoa haki fulani na uhuru fulani! haiwezekani, mtu aliyeapa kuilinda katiba, akaibuka kwa mamlaka aliyopewa na katiba hiyo, akauondoa uhuru fulan au haki fulani na huku Watanzania wengine wote tukimwangalia tuu, au tunamshangilia tuu!. Huku ni kwenda kinyume cha katiba, wote tukiendelea kunyamaza tuu, kunaweza kusababisha mtenda haki Mkuu, kuingilia kati kama kwenye zile tawala za nyuma, hivyo the best thing we can do, ni kwa sisi baadhi yenu kusema tuu, maana huo ndio mwisho wa uwezo wetu, kusema, au kuandika tuu na kuwaachia wenye uwezo wa kutenda watende!, na maadam wenye uwezo huo nao wameamua kunyamaza, matokeo ni Mtengaji Mkuu wa yote, ataingilia kati na atatenda!.

Japo wengi wetu, tunaishi katika lindi la umasikini, uliotopea, na sio tuu hatuna hata hiyo likizo, lakini umasikini wetu, usitufanye tuwachukie, wenzetu waliobahatika kuwa wenye heri, wenye uwezo wa kwenda kujipumzikia zao ulaya wakati wa likizo zao!.

Nashauri serikali itoe waraka wa ufafanuzi wa hili katazo la safari za nje, unless itamkwe wazi, watumishi wote wa umma, hata safari zao binafsi kujipumzikia, au kuwatembelea wapendwa wao, wapenzi wao au hata vimada wao, sasa lazima waombe kibali kwa KMK!, na jee kama hivi ndivyo katiba ilivyotamka?!, kama sio kwa mujibu wa katiba, then rais atoe waraka, Tanzania tujijue tuko kama China au Urusi, enzi zile, kuingia Beijing au Moscow, mtu hujiingilii hivi hivi!. Lazima uombe kibali.

Jee kumkumbusha rais wetu kuhakikisha watendaji wake wanazingatia katiba aliyoapa kuilinda, watimize wajibu wao kwa mujibu wa katiba, sheria, taratibu na kanuni ni kumuingilia katika utendaji wake?!

Pasco
 
Pasco, Asante sana sana kwa kuileta hii. Nimeshaandika mara kadhaa na kufanya Analysis ya siku 30 za Rais Magufuli. Amekuwa kinara wa upendeleo, kutosimamia sheria. Corporate Management kwake ni msamiati mgumu kabisa

Mtu yupo Likizo, anasafiri bila kutumia fedha za Serikali anazuiwa. Huu ni ukiukwaji wa haki za msingi kabisa za kikatiba.

Angekuwa ni mtuhumiwa sawa lakini Mahakama ndiyo inayoamua

Niliandika na kuonya haya:

- Tutapuuzwa kwa upuuzi wetu itaifa

- Rais Magufuli na Slack Management Style, Utekelezaji mbaya wa Ilani ya UKAWA
 
Mi sipo huko kwenye uvunjifu wa haki za binadamu ila nipo kwenye zuio Zima kwa ujumla, kumekuwa na watu wakishangilia 'kila' anachofanya mheshimiwa.

Sijui kama watu wanapata muda wa kuyatafakari hayo maagizo au mazuio...yapo mengi pia nadhani wanaotakiwa kuya-define wanapotosha...'niko likizo natumia hela yangu sina tuhuma yoyote kwanini nizuiwe kusafiri?' ni wrong interpretation.

Ila utasikia watu tumbua tumbua tumbua huku wakinyanyua hadi miguu!!siyo haki...nadhani kun sababu ya wahusika kutoa mipika ya hilo zuio!
 
unaenda kutalii nje na kuacha mlima kilimanjaro na serengeti Tanzania??..unaenda kutembelea wazungu wakati bibi yako Nantumbo hajakuona mwaka wa pili sasa?? tumalize ziara za ndani kwanza kabla hatujawaza kukwea mapipa
 
Hukatazwi kusafiri, kinachokatazwa ni kusafiri kwa gharama ya serikali na ndani ya muda wa ajira ya serikali bila kibali cha rais. Kama unataka, acha utumishi Wa umma na jigharamie mwenyewe hilo lisafari lako la ulaya
 
Pasco, Asante sana sana kwa kuileta hii.Nimeshaandika mara kadhaa na kufanya Analysis ya siku 30 za Rais Magufuli.Amekuwa kinara wa upendeleo,kutosimamia sheria.Corporate Management kwake ni msamiati mgumu kabisa

Mtu yupo Likizo,anasafiri bila kutumia fedha za Serikali anazuiwa.Huu ni ukiukwaji wa haki za msingi kabisa za kikatiba.

Angekuwa ni mtuhumiwa sawa lakini Mahakama ndiyo inayoamua

Niliandika na kuonya haya

https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...tyle-utekelezaji-mbaya-wa-ilani-ya-ukawa.html

Hivi kwa nini unapenda ligi? dont be too arrogant. kuna mambo mengine hayawezi kuwekwa wazi kila mtu, huwezi jua maagizo ya ikulu, staff wa BOT siyo BEN wala mimi. Be greatthinker.
 
Hivi kwa nini unapenda ligi? dont be too arrogant. kuna mambo mengine hayawezi kuwekwa wazi kila mtu, huwezi jua maagizo ya ikulu, staff wa BOT siyo BEN wala mimi. be greatthinker.

Nchi iliyokubali kufuata misingi ya demokrasia,Utawala bora wa Sheria ndio alama na katika hilo Uwazi na Uwajibikaji(transparency and Accountability) ndio nguzu kuu.

Hapo kwenye red Bold ni fikra za kijima(Primitiveness).
 
Ndiyo maana nimewahi kusema hapa jamnvini kuwa kwa katiba iliyopo nchi hii itaongozwa kwa presidential decrees; walio wengi na baadhi yao bila hatia wataumia. TUNAHITAJI KATIBA YA WARIOBA IRUDI KWENYE BUNGE JIPYA MAALUMU LA KATIBA vinginevyo tutaisoma namba. Tulimtaka dictator na tumempata. kazi kwetu!
 
Pasco, umesahau utekelezaji wa sera ya ujamaa vijijini? Kuna baadhi ya watendaji wa serikali wataenda mbali zaidi ya kile wanachotakiwa wafanye na hivyo kuangukia kwenye huo uvunjaji wa haki za binadamu: umesikia pia sehemu fulani watumishi waliokuwa likizo warudi kazini na kwamba likizo zao zimefutwa na kwamba pia watumishi fulani walichelewa kikao na kuswekwa ndani na DC na tena akaamuru wasipewe dhamana.

Just imagine! Kuna msemo kwamba mtu "anakupa mkono wewe unashika bega" - wapi na wapi?
 
huwezi kumpangia mtu pa kwenda. kama mtu anasafari zake aachiwe aende. kama ni mtuhumiwa ashugulikiwe.

ukiZidi utatafsiriwa labda ni wivu.

unataka aende mikumi mwenzako unataka kwenda kuangalia kangaroo Australia mikumi hawapo.kama anapesa halali sio sawa kuzuiwa. na kama anahitajika kutoa taarifa kisheria afanye hivyo Ila sio kuzuiwa kama hana tatizo.

nadhani rais anasave pesa za serikali sio mishahara ya watu na matumizi yake. kwa kwenda nje kwa mapato binafsi nchi inaongeza kipato kidogo kwa tkt. kama anaenda kuficha fweza na ikathibitika Niko pamoja na zuio hilo
 
unaenda kutalii nje na kuacha mlima kilimanjaro na serengeti Tanzania??..unaenda kutembelea wazungu wakati bibi yako Nantumbo hajakuona mwaka wa pili sasa?? tumalize ziara za ndani kwanza kabla hatujawaza kukwea mapipa

huu ndio wivu wa maendeleo kama mwenzako amekushinda kimapato ana haki ya kutumia ela yake vovote anavyoona inafaa sio aanze kufuatwa fuatwa kama kaiba!!!
 
Magufuli ni dictator hajui ayafanyayo yata mcost asilimia kubwa ya watanzania kwa umaskini wao wanampigia mapambia lakini atakwama maana anavunja utawala wa sheria
 
Acheni mambo ya kifala.mtu kajibana mwaka mzima Ili aende zake kuinjoy mwezi huu halafu anakatazwa. Huku tunapoelekea mh.rais unaharibu sasa au umelewa sifa nini
kwa wastani wa uchumi wa taifa letu, ni uhaini kwenda kula x-mas ulaya. Aende tu Serengeti, hakuna namna
 
Binafsi nimefanya kazi kwa muda mrefu na serikali na nafahamu vizuri sheria za kusafiri nje ya nchi. Kwanza tujue kuwa kuomba kibali cha kusafiri kwenda nje ya nchi hakijaanza leo, ni tangu enzi za Mwalimu. Kilichokuwepo ni kukosa usimamizi. Tangu miaka hiyo, unajaza fomu 2 moja inaishia wizarani au kwa mwajiri wako (mkurugenzi, Katibu Mkuu). Ya pili inakwenda Ikulu. Na unajaza tu unapokuwa kwa shughuli za kikazi.

Najua, wengi mnajua, airport kuna taratibu gani za kuasafiri. Hakuana anayeangalia kibali cha kusafiri mtu zaidi ya Visa na pengine kama kuna kitu kinaleta sintofahamu barua ya mwaliko.

Kama kunatokea kitu kama hiki hasa kwa mtumishi wa umma, kuna cha zaidi. Tujipe muda, nchi inafukuta na watu wengine wanatafuta pa kutokea. Kama hana shida kwani alijitambulisha au kuna reja ya wafanyakazi Airport. Hakuna!!!!

Hatuwezi kuja na majibu ya jumla hata aliyekataliwa tunafahamiana sana naye.
Wanabodi,

Tanzania ni nchi inayofuata katika na utawala wa sheria!.

Ndani ya katiba ya JMT kuna vifungu rasmi vya haki za msingi za binaadamu!. Moja ya haki hizo ni kipengele hiki

Kama jambo hili ni kweli limefanyika,
[h=1]Kigogo wa BoT azuiwa Airport kutokana na kukosa vibali vya kusafiri nje ya nchi[/h] then
Haiwezekani mtu ambaye yuko huru, tena yuko likizo, ameamua kwenda kujipumzikia zake nchi za wenzetu, azuiliwe!.


Pasco

Pasco, Asante sana sana kwa kuileta hii.Nimeshaandika mara kadhaa na kufanya Analysis ya siku 30 za Rais Magufuli.Amekuwa kinara wa upendeleo,kutosimamia sheria.Corporate Management kwake ni msamiati mgumu kabisa

Mtu yupo Likizo,anasafiri bila kutumia fedha za Serikali anazuiwa.Huu ni ukiukwaji wa haki za msingi kabisa za kikatiba.

Angekuwa ni mtuhumiwa sawa lakini Mahakama ndiyo inayoamua

Niliandika na kuonya haya

https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/985296-rais-magufuli-na-slack-management-style-utekelezaji-mbaya-wa-ilani-ya-ukawa.html

Na juzi nimeandika ni ujinga kushabikia hata mambo ya kipuuzi.
https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/987478-tutapuuzwa-kwa-upuuzi-wetu-kitaifa-makala.html
 
Nchi iliyokubali kufuata misingi ya demokrasia,Utawala bora wa Sheria ndio alama na katika hilo Uwazi na Uwajibikaji(transparency and Accountability) ndio nguzu kuu.

Hapo kwenye red Bold ni fikra za kijima(Primitiveness).
Pamoja sitaki kumtetea mtu hapa, ila ukweli uelezwe. Kila kitu kina sheria na taratibu zake. Mfanyakazi wa Serikali yupo kazini tangu siku anayoanza kazi hadi anapostaafu. Hivyo hata wakati wa likizo kama si likizo bila malipo anawajibika kwa mwajiri. Kumbuka fomu ya likizo lazima uiombe na useme unaenda wapi. Hili ni jambo la kawaida kwa nchi nyingi. Mfano India kama ni mfanyakazi wa serikali kama upo likizo lazima uombe kibali kwenda nje na ueleze faida za nchi ya India itakazopata kwa wewe kwenda nje. Ukirudi lazima utoe mrejesho. Kwa India ukkistaafu kama kiongozi katika serikali. Huruhusiwi kuajiriwa popote hadi baada ya miaka miwili bila kibali cha serikali.
 
Back
Top Bottom