Kichankuli
JF-Expert Member
- Dec 18, 2008
- 887
- 189
Mfuko wa Bima ya Afya kwa Watumishi wa Serikali umeanzishwa kisheria ambapo kila Mtumishi hulazimika kusajiliwa na kukatwa asilimia 3 ya mshahara wake kila mwezi kuchangia bima hiyo. Leo asubuhi Mkuu wa Mfuko huo alikuwa akihojiwa na ITV, na moja wapo ya mambo aliyoyaongea ni upanuzi wa huduma zinazolipiwa na Mfuko huo kujumuisha kipimo cha CT Scanner. Katika maelezo yake alieleza kwamba pamoja na kipimoo hicho kuwa covered na Bima ya Afya, ni kweli kwamba wanachama wake wengi wanaweza kutonufaika na kipimo hicho kutokana na hospitali nyingi kutokowa na vifaa vya kuwezesha kufanya kipimo hicho.
Kwa maoni yangu naona kwamba Menejimenti ya Mfuko wa Bima ya Afya haututendei haki wanachama wake na badala yake inatubagua kutokana na maeneo ambayo tunaishi na kufanyia kazi. Naamini kwamba kwa kutumia fedha tunazokatwa Menejimenti ya Bima ya Afya wageweza kufungua maabara kwa kila mkoa na baadaye kuteremka zaidi hadi kwenye kata. Au la, wanachama tuwe tunagharamiwa fedha za nauli na kujikimu pale inapoonekana kwamba mwanachama mgonjwa anatakiwa kupimwa kipimo hicho.
Ubaguzi mwingine ambao ninauona katika Bima ya Afya ni ule wa kuwa na makundi mawili ya wanachama. Kuna wanachama ambao wanapewa vitambulisho vyenye sehemu yenye rangi ya kijani ambao hawa huruhusiwa kutibiwa hospitali yeyote. Wanachama wengine ni wale wnye vitambulisho vya rangi nyeupe ambao hawawezi kutibiwa kwenye hospitali kama Mikocheni au Aghakani (siyo zahanati za Aghakani). Nionavyo mimi hii siyo haki kwa sababu Mfuko huu ni wa lazima kisheria, vinginevyo ungefanywa wa hiari kama ule wa Mfuko wa Afya ta Jamii (CHF) na kwamba Mtumishi aambiwe kuna aina mbili za uanachama ili aweze kuchagua wapi anapopenda kuchangia kama ni VIP au Kima cha Chini. Msingi wa hoja yangu ni kwamba kwa vile hakuna utaratibu wa kukokotoa kila mwanachama ametumia gharama kiasi gani kwa mwezi au mwaka katika matibabu na kwamba kuna uwezekano wa Mtumishi Mwanachama wa ngazi ya chini kutotumia huduma ya Bima ya Afya kwa mwaka mzima au zaidi na yule wa ngazi ya juu kutumia zaidi; ni wazi kwamba kila mmoja wa wanachama anao uwezekano wa kutumia fedha za mwanachama mwenzake katika kukidhi gharama. Na hii ndiyo mantiki ya kuunda Mfuko wa Bima ya Afya ili wanachama wakusanye nguvu zao za kifedha kuweza kumkabili adui maradhi. Hakuna haja ya kuwatenga wanachama kwa makundi.
Wana JF mna maoni gani?
Kwa maoni yangu naona kwamba Menejimenti ya Mfuko wa Bima ya Afya haututendei haki wanachama wake na badala yake inatubagua kutokana na maeneo ambayo tunaishi na kufanyia kazi. Naamini kwamba kwa kutumia fedha tunazokatwa Menejimenti ya Bima ya Afya wageweza kufungua maabara kwa kila mkoa na baadaye kuteremka zaidi hadi kwenye kata. Au la, wanachama tuwe tunagharamiwa fedha za nauli na kujikimu pale inapoonekana kwamba mwanachama mgonjwa anatakiwa kupimwa kipimo hicho.
Ubaguzi mwingine ambao ninauona katika Bima ya Afya ni ule wa kuwa na makundi mawili ya wanachama. Kuna wanachama ambao wanapewa vitambulisho vyenye sehemu yenye rangi ya kijani ambao hawa huruhusiwa kutibiwa hospitali yeyote. Wanachama wengine ni wale wnye vitambulisho vya rangi nyeupe ambao hawawezi kutibiwa kwenye hospitali kama Mikocheni au Aghakani (siyo zahanati za Aghakani). Nionavyo mimi hii siyo haki kwa sababu Mfuko huu ni wa lazima kisheria, vinginevyo ungefanywa wa hiari kama ule wa Mfuko wa Afya ta Jamii (CHF) na kwamba Mtumishi aambiwe kuna aina mbili za uanachama ili aweze kuchagua wapi anapopenda kuchangia kama ni VIP au Kima cha Chini. Msingi wa hoja yangu ni kwamba kwa vile hakuna utaratibu wa kukokotoa kila mwanachama ametumia gharama kiasi gani kwa mwezi au mwaka katika matibabu na kwamba kuna uwezekano wa Mtumishi Mwanachama wa ngazi ya chini kutotumia huduma ya Bima ya Afya kwa mwaka mzima au zaidi na yule wa ngazi ya juu kutumia zaidi; ni wazi kwamba kila mmoja wa wanachama anao uwezekano wa kutumia fedha za mwanachama mwenzake katika kukidhi gharama. Na hii ndiyo mantiki ya kuunda Mfuko wa Bima ya Afya ili wanachama wakusanye nguvu zao za kifedha kuweza kumkabili adui maradhi. Hakuna haja ya kuwatenga wanachama kwa makundi.
Wana JF mna maoni gani?