Je Huu si ni Ubaguzi Katika Bima ya Afya?

Kichankuli

JF-Expert Member
Dec 18, 2008
887
189
Mfuko wa Bima ya Afya kwa Watumishi wa Serikali umeanzishwa kisheria ambapo kila Mtumishi hulazimika kusajiliwa na kukatwa asilimia 3 ya mshahara wake kila mwezi kuchangia bima hiyo. Leo asubuhi Mkuu wa Mfuko huo alikuwa akihojiwa na ITV, na moja wapo ya mambo aliyoyaongea ni upanuzi wa huduma zinazolipiwa na Mfuko huo kujumuisha kipimo cha CT Scanner. Katika maelezo yake alieleza kwamba pamoja na kipimoo hicho kuwa covered na Bima ya Afya, ni kweli kwamba wanachama wake wengi wanaweza kutonufaika na kipimo hicho kutokana na hospitali nyingi kutokowa na vifaa vya kuwezesha kufanya kipimo hicho.

Kwa maoni yangu naona kwamba Menejimenti ya Mfuko wa Bima ya Afya haututendei haki wanachama wake na badala yake inatubagua kutokana na maeneo ambayo tunaishi na kufanyia kazi. Naamini kwamba kwa kutumia fedha tunazokatwa Menejimenti ya Bima ya Afya wageweza kufungua maabara kwa kila mkoa na baadaye kuteremka zaidi hadi kwenye kata. Au la, wanachama tuwe tunagharamiwa fedha za nauli na kujikimu pale inapoonekana kwamba mwanachama mgonjwa anatakiwa kupimwa kipimo hicho.

Ubaguzi mwingine ambao ninauona katika Bima ya Afya ni ule wa kuwa na makundi mawili ya wanachama. Kuna wanachama ambao wanapewa vitambulisho vyenye sehemu yenye rangi ya kijani ambao hawa huruhusiwa kutibiwa hospitali yeyote. Wanachama wengine ni wale wnye vitambulisho vya rangi nyeupe ambao hawawezi kutibiwa kwenye hospitali kama Mikocheni au Aghakani (siyo zahanati za Aghakani). Nionavyo mimi hii siyo haki kwa sababu Mfuko huu ni wa lazima kisheria, vinginevyo ungefanywa wa hiari kama ule wa Mfuko wa Afya ta Jamii (CHF) na kwamba Mtumishi aambiwe kuna aina mbili za uanachama ili aweze kuchagua wapi anapopenda kuchangia kama ni VIP au Kima cha Chini. Msingi wa hoja yangu ni kwamba kwa vile hakuna utaratibu wa kukokotoa kila mwanachama ametumia gharama kiasi gani kwa mwezi au mwaka katika matibabu na kwamba kuna uwezekano wa Mtumishi Mwanachama wa ngazi ya chini kutotumia huduma ya Bima ya Afya kwa mwaka mzima au zaidi na yule wa ngazi ya juu kutumia zaidi; ni wazi kwamba kila mmoja wa wanachama anao uwezekano wa kutumia fedha za mwanachama mwenzake katika kukidhi gharama. Na hii ndiyo mantiki ya kuunda Mfuko wa Bima ya Afya ili wanachama wakusanye nguvu zao za kifedha kuweza kumkabili adui maradhi. Hakuna haja ya kuwatenga wanachama kwa makundi.

Wana JF mna maoni gani?
 
Hapa ndugu yangu kuna ufisadi wa mkubwa unaendelea chini kwa chini, karibu wanachama wote wa mfuko huu hawaridhiki na huduma zake na pia utaratibu wa makato umekaa kibabe mno. Kwanza wagonjwa wanao tumia kadi hizi hawapewi huduma inavyo stahili hasa huko vijijini kwa sababu hawachangii vituo vya afya moja kwa moja. Hata dawa hutolewa kwa shida na pengine huambiwa wafuate katika maduka yaliyoingia mkataba na mfuko huu kuhudumia wateja wake. Huko nako ni balaa tu wenye maduka haya huwa hawatoi ushirikiano kwa wagonjwa na mara nyingi huwa hawatoi dawa. Ukiwauliza kwa undani utagundua wanafanya hivyo kwa kuwa mfuko huchelewa sana kuwalipa pesa zao hivyo. Hata mikataba na maduka haya inatia shaka kwani hutolewa bila kujali hadhi au ukubwa wa duka lenyewe hivyo kuwanyima wateja wao huduma wanayo stahili.
 
Je kila mwanachama hutoa mchango sawa?

Kama mwal. wa primary anatoa mchango wa 6,000 na Daktari 30,000 je wapate matibabu yaliyo sawa? Ndo maana kuna wanaopewa kadi zenye rangi tofauti!

Does government provide support kwa wanatoa kidogo ili kupata vipimo kama CT Scan?

Ikumbukwe pia Tz hatuna Universal Health Insurance Covarage: na kama ukiwa mlala hoi ukiungua basi ni shida sana ndugu yangu!

Ikimbukwe watz wote ni binadamu na wanahitaji kuhudumiwa kama watu wengine: uwe maskini au tajiri, au uwe na kazi au mlala hoi!
 
Je kila mwanachama hutoa mchango sawa?

Kama mwal. wa primary anatoa mchango wa 6,000 na Daktari 30,000 je wapate matibabu yaliyo sawa? Ndo maana kuna wanaopewa kadi zenye rangi tofauti!

Does government provide support kwa wanatoa kidogo ili kupata vipimo kama CT Scan?

Ikumbukwe pia Tz hatuna Universal Health Insurance Covarage: na kama ukiwa mlala hoi ukiungua basi ni shida sana ndugu yangu!

Ikimbukwe watz wote ni binadamu na wanahitaji kuhudumiwa kama watu wengine: uwe maskini au tajiri, au uwe na kazi au mlala hoi!

Mkuu je katika kuugua je ugonjwa unachagua kipato chako au mchango wako katika huu mfuko??

Je kama wewe umechangia kiasi kidogo inapotokea unahitaji kipimo kikubwa kama cha CT scan husipimwe kwakuwa wewe mchango wako ni mdogo??

Je katika uanzishaji wa huu mfuku je wadau wake walitaarifiwa kwamba kutakuwa na makundi ya wafaidika na huu mpango??

Swala la pili ni kwa watoa huduma husika mahospitali,zahanati na maduka ya dawa, wao wameingia mkataba na Bima ya afya na sio wanachama wa bima ya afya, kwa hiyo basi ucheleweshaji wa malipo wanayodai sio sababu ya kuwanyanyapaa wanachama wa mfumo huu. Kwani katika mikataba yao wamekubaliana kwamba, watalipwa baada ya muda fulani na baada ya mfuko wa bima kuhakiki madai yao kama yapo sahihi au la kulingana na vigezo walivyowekeana.

Nina experience na mifumo hii ya bima ya afya nchi Tanzania kwa muda mrefu tu (manake mimi ni miongoni mwa waanzilishi wake kwenye sekta binafsi) Kinachotokea mara nyingi ni kwamba watoa huduma wengi wa Tanzania sio waaminifu. Kila wanapotoa huduma(matibabu na madawa) wa wanazidisha bei au wanakuchaji huduma ambayo hakupewa. Kwani wateja/wadau wengi huwa hawaelewi uhandishi wa kidaktari( lugha wanayoandika kwenye cheti cha mdau)


Upungufu mwingine ni mfumo wa uhakiki wa malipo ya huduma zilizotolewa kwa wadau.
 
Je kila mwanachama hutoa mchango sawa?

Kama mwal. wa primary anatoa mchango wa 6,000 na Daktari 30,000 je wapate matibabu yaliyo sawa? Ndo maana kuna wanaopewa kadi zenye rangi tofauti!

Mzalendo halisi, kinachogomba hapa ni kwamba hakuna mwanachama ambaye alishaambiwa kwamba ukitaka kuwa katika kundi la VIP unatakiwa uchangie kiasi gani. Kwa hali ilivyo hivi sasa ambapo ni asilimia ndiyo hutumika kukata mchango wa mwanachama, bado kuna kutotendewa haki miongoni mwa wanachama. Angalia hapa, Mtumishi wa kima cha chini anayelipwa mshahara wa sh. 100,000.00 kwa mwezi; 3% yake ni sh. 3,000.00, ambapo mchango wake kwa mwaka ni sh. 36,000.00. Mtumishi huyu yuko kundi moja na Afisa mwandamizi ambaye mshahara wake ni. sh. 500,000.00 na mchango wake kwa mwezi na mwaka kwenye bima ya Afya ni sh. 15,000.00 na sh. 180,000.00 kwa mtiririko huohuo. Hapa kuna tofauti ya mchango ya sh. 144,000.00. Hali hii pia utaikuta kwa kundi la wanachama wa kundi la VIP. Sasa kwa hali hii, kwanini kusiwe na kiwango kimoja tu cha mchango pamoja na haki sawa za kupatiwa huduma; au makundi hayo yawekwe wazi na mwanachama awe na uhuru wa kuchaguwa wapi anapenda kuwemo?

Lakini udhaifu mwingine wa Mfuko wa Bima ya Afya kuwa wa lazima na usio wazi ni kwamba Watumishi ambao ni Mke na Mume na wanafanya kazi serikalini, wanajikuta mmoja wao anakatwa pesa ambayo katika hali ya kawaida asingekuwa na zababu ya kukata kwani anaingia kwenye cover ya mwenzi wake.

Hali hii ndiyo inayoonyesha kuwa kuna umuhimu wa kubadili sheria iliyoanzisha Mfuko wa Bima ya Afya ili utoe haki sawa kwa wanachama wake
 
Back
Top Bottom