banned do
JF-Expert Member
- Apr 27, 2017
- 574
- 507
Habari zenu wana jamvi?Ni zaidi ya mara moja nimekuwa nikinunua umeme kupitia M-Pesa na Tigo Pesa kisha sipokei ujumbe wenye Token na kunionesha kuwa nimenunua umeme.Baada ya kupiga simu huduma kwa wateja watoa huduma hutaja namba za token kisha kutaka nizinukuu kisha kuingiza kwenye mita ya Luku.Nilijaribu kufuatilia nikagundua si mimi peke yangu tu bali kuna jirani zangu pia.Je katika hili kuna makato yoyote ya kodi yanayokatwa na TRA?Na je huu si mtindo mpya wa ukwepaji kodi?Wenye uelewa katika jambo hili tusaidiane.