Mwanamayu
JF-Expert Member
- May 7, 2010
- 11,349
- 6,476
Juzi tumesoma kwenye magazeti na kuona picha jinsi askari wa kutuliza ghasia wakihitimu mafunzo ya kupambana na ghasia. Walikuwa kwenye vifaa vipya na kuonesha kufuzu mafunzo hayo. Moja ya malengo ya JWTZ ni kutuliza ghasia nchini endapo mamlaka husika - polisi - kushindwa. Sasa nyie polisi kabla hata ya muda kufika na mafunzo yote hayo na vifaa vyote hivyo mmekwisha zidiwa? Na nyie JWTZ mmejuaje kama hawa FFU walio - pass out juzi kama wameshindwa wakati hata hizo ghasia zenyewe hazijatokea?
Je, hili ni Jeshi la Wananchi wa Tanzania au Jeshi la Watawala wa Tanzania? Mimi najua kuwa Fanya Fujo Uone (FFU) wakishindwa wanaitwa askari Magereza ambao wanamafunzo ya kujua wapi wapige ili mfanya fujo atulie na wana uwezo huo kwani uyanyamazisha majambazi huko magerezani, nao wakishindwa ndipo uitwa ninyi. Nanyi uitwa na Comander in chief ambaye ni Rais kwa kutangaza hali ya hatari na kutupangia muda wa kutembea na kazi yenu kubwa ni kuua.
Mwalimu Nyerere aliwataka mishi na wananchi ili tuwe kitu kimoja, sasa nyie mnajiona ni tofauti na wananchi!
Je, hili ni Jeshi la Wananchi wa Tanzania au Jeshi la Watawala wa Tanzania? Mimi najua kuwa Fanya Fujo Uone (FFU) wakishindwa wanaitwa askari Magereza ambao wanamafunzo ya kujua wapi wapige ili mfanya fujo atulie na wana uwezo huo kwani uyanyamazisha majambazi huko magerezani, nao wakishindwa ndipo uitwa ninyi. Nanyi uitwa na Comander in chief ambaye ni Rais kwa kutangaza hali ya hatari na kutupangia muda wa kutembea na kazi yenu kubwa ni kuua.
Mwalimu Nyerere aliwataka mishi na wananchi ili tuwe kitu kimoja, sasa nyie mnajiona ni tofauti na wananchi!