Wana JF hapa nimeambatanisha picha hapa chini, niliyoitoa katika gazeti la kila juma ya The East African la Aug 31-Sep 6, 2013.
Kutokana na takwimu katika gazeti hili:
1. Tanzania ina ardhi kubwa kuliko nchi zote kwa pamoja.
2. Kenya haina aridhi hata ya akiba, kiasi kwamba tayari imetumia sehemu ya misitu yake ya asili.
3. Rwanda na km za mraba zisizofikia 3,500 kati ya 26,000
4. Burundi ina akiba ya 16,000 km za mraba 16,000 kati ya 27,000.
5. Uganda ndiyo yenye akiba nzuri ya ardhi inayofikia km za mraba 78,000.
6. Burundi ina akiba kubwa ya ardhi kuliko Kenya na Rwanda.
7. Akiba ya Tanzania ni zaidi ya km za mraba 450,000! Ukijumlisha akiba ya aridhi za nchi hizo nne, utagundua kuwa haifikii hata theluthi 1 ya akiba ya ardhi ya Tanzania.
Kwa maana hiyo ni wazi kuwa kupishana kunakoendela kunachochewa na wivu, uchu wa ardhi ya Watanzania.
Kibiashara, chati inaonyesha kuwa EAC ni tegemeo la pili, ambapo Kenya ndo mnufaika mkubwa zaidi ya wenzake.
Pia Tanzania inaonyesha kuwa na maji mengi kuliko zote za EAC.
Ukiongeza mali asili za nchi hii kama vile madini, gesi, mafuta, bahari, maziwa, mipaka 8, maeneo ya kitalii n.k. utagundua kuwa Tanzania si mbia wa kutengwa kwa watawala wenye busara. Ndiyo maana mataifa makubwa hayakomi kuizuru nchi hii.
Pia tanzania ni soko muhimu kwani ina idadi kubwa ya watu kuliko nchi zote za EAC. Kenya itaathirika zaidi endapo jumuiya hii itakufa.
Sasa ni wakati kwa viongozi wetu kuwa na utashi kujenga na kuimarisha mahusiano na nchi zingine kama DRC ambayo inaweza kuleta faida pande zote mbili kwa uwiano unaoshabiiana.
Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums
Kutokana na takwimu katika gazeti hili:
1. Tanzania ina ardhi kubwa kuliko nchi zote kwa pamoja.
2. Kenya haina aridhi hata ya akiba, kiasi kwamba tayari imetumia sehemu ya misitu yake ya asili.
3. Rwanda na km za mraba zisizofikia 3,500 kati ya 26,000
4. Burundi ina akiba ya 16,000 km za mraba 16,000 kati ya 27,000.
5. Uganda ndiyo yenye akiba nzuri ya ardhi inayofikia km za mraba 78,000.
6. Burundi ina akiba kubwa ya ardhi kuliko Kenya na Rwanda.
7. Akiba ya Tanzania ni zaidi ya km za mraba 450,000! Ukijumlisha akiba ya aridhi za nchi hizo nne, utagundua kuwa haifikii hata theluthi 1 ya akiba ya ardhi ya Tanzania.
Kwa maana hiyo ni wazi kuwa kupishana kunakoendela kunachochewa na wivu, uchu wa ardhi ya Watanzania.
Kibiashara, chati inaonyesha kuwa EAC ni tegemeo la pili, ambapo Kenya ndo mnufaika mkubwa zaidi ya wenzake.
Pia Tanzania inaonyesha kuwa na maji mengi kuliko zote za EAC.
Ukiongeza mali asili za nchi hii kama vile madini, gesi, mafuta, bahari, maziwa, mipaka 8, maeneo ya kitalii n.k. utagundua kuwa Tanzania si mbia wa kutengwa kwa watawala wenye busara. Ndiyo maana mataifa makubwa hayakomi kuizuru nchi hii.
Pia tanzania ni soko muhimu kwani ina idadi kubwa ya watu kuliko nchi zote za EAC. Kenya itaathirika zaidi endapo jumuiya hii itakufa.
Sasa ni wakati kwa viongozi wetu kuwa na utashi kujenga na kuimarisha mahusiano na nchi zingine kama DRC ambayo inaweza kuleta faida pande zote mbili kwa uwiano unaoshabiiana.
Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums