JAYRUTTY aonyesha IRIZAR la Simba

JAYRUTTY aonyesha IRIZAR la Simba

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
4,415
Reaction score
14,587
Mkurugenzi wa Kampuni ya JAYRUTTY akiwa amepiga picha na basi litakalotumiwa na kampuni hiyo katika uuzaji wa jezi za Simba pamoja na promosheni mbalimbali zinazohusiana na Klabu ya Simba. Tukio hilo limefanyika nchini China, ambapo maandalizi yote yamekamilika, na basi hilo linatarajiwa kuingia majini kuanza safari ya kuelekea Dar es Salaam.


1768387245651.png
Wakati huo huo, kwa mujibu wa taarifa kutoka kwenye vyanzo vyakuaminika, basi la Simba aina ya IRIZAR pia tayari limeshanunuliwa na linatoka nchini Hispania, kama ilivyoahidiwa. Hata hivyo, kutokana na changamoto za njia ya maji kutoka Ulaya, njia ya usafirishaji imebadilishwa. Kutokana na mabadiliko hayo, basi la Simba IRIZAR linatarajiwa kuwasili Dar es Salaam mwezi Februari mwaka huu.

Zaidi
 
Mkurugenzi wa Kampuni ya JAYRUTTY akiwa amepiga picha na Busambalo litatumika na Kampuni hiyo kuuzia Jezi za Simba na promosheni mbalimbali za Kampuni hiyo zinazohusu Simba, hapo ni nchini China ambapo kila kitu kipo tayari na Bus litaingia Majini kuanza safari ya kuja Dar Es Salaam.

Wakati huo huo kwa mujibu wa taarifa kutoka kwenye Vyanzo vyangu ni kuwa IRIZAR la Simba pia limeshanunuliwa na linatokea nchini Hispania kama alivyoahidi ila kutokana na changamoto za njia ya Maji kutokea Ulaya route imebadilishwa hivyo Bus la Simba Irizar linatarajiwa kufika Dar Es Salaam mnamo mwezi Februari mwaka huu.
Hiyo picha I wapi?
 
Isije tu ikawa ni muendelezo ule ule wa maigizo kwa mashabiki na wanachama wa hiyo timu! Hata kwenye ule uchaguzi wa kipindi kile, Manzoki alikuja kutoka China!
 
Kilio kipo pale pale, kitachobadilika sasa ni michozi kuililia ndani ya "Irizar ya mchongo" badala ya Yutong
 
Back
Top Bottom