Java & Android Programming Training

Mtangoo

JF-Expert Member
Joined
Oct 25, 2012
Posts
6,165
Reaction score
5,621
Tunapenda kuwatangazia wale wanaopenda Kujifunza Kuandika Code kwa Java na Kuweza kutengeneza mobile application kuwa Tutakuwa na Kozi Mbili moja ikianzia October 25 na nyingine Itaanza Disemba Mosi.

Taarifa zote za msingi zipo katika kiambatanisho cha PDF. Kwa maswali yote niulize nami nitajitahidi kuyajibu yote.

Shukrani sana Tuonane Tar 25!

NB:
Kwa wanaoshindwa kufungua file la PDF click na uchague Open badala ya save. Na kama ulishalihifadhi mahala, kwenye browser yake nenda kwenye menu ya File --> Open halafu ulifungue ulipoliweka.

Kama una PDF Reader kama Adobe Reader au Foxit au nyingine basi double click hilo faili litafunguka. List ya PDF readers ipo hapa kwa uchache:

The 6 Best PDF Readers for Windows
 

Attachments

Swali: Mimi Sijui mambo ya IT wala programming. Je kozi hii itanifaa

Jibu: Kozi hii ni kwa watu ambao hawajawahi kuwa na ujuzi wowote wa Programming wala "IT". Mahitaji ya lazima ni kujua Kiingereza kiasi cha kuelewana na mwalimu na pili uwe unajua kutumia Kompyuta kwa matumizi ya kawaida. Zaidi ya hapo hakuna kingine kinachohitajika!
 
Nini matarajio yangu Baada ya kumaliza mafunzo haya?
Baada ya kumaliza tunatarajia:
1. Utakuwa na Ufahamu mzuri wa Java. Hii itakusaidia kuifahamu vizuri na hivyo kuitumia vyema. Ni kama fundi anayejua Toolbox nzima huwezi ukamkuta anaingiza nati kwa kutumia nyundo. Anajua pale ni mahali pa bisibisi na sio nyundo. Ila fundi anayejua nyundo tu atalazimisha hata sehemu ya kuchomelea ipigwe nyundo.

Kwa hiyo tunatarajia ukimaliza uwe na uwezo wa kutengeneza program za viwango vya juu za Java. Na hii si maalum kwa Android bali ni program zote za Java iwe ni Java EE au Java na Swing

2. Tunatarajia uwe na uwezo wa kuandika Android app from scratch. Tumeona Watanzania wengi wakiungaunga kwa kunakili code Stackoverflow au ku customize code za Watu github na penginepo. Hapa tutakufundisha jinsi ya kuandika programu yako tangu chini mpaka juu na jinsi ya kutumia maktaba (library) zilizoandikwa na wengine katika kurahisisha maisha. Ukiangalia kwenye Lesson ya mwisho tutajifunza kuandika application ambayo ni real world na sio ka mfano ka Hello World. Ni kozi ya kupata ujuzi kamili na sio stori.

3. Tutakufundisha kanuni za Kujaribu (Test Driven Development) ambayo pamoja na mengine mengi inafanya program zako ziwe na ubora wa hali ya juu unapopeleka kwa mteja kwani unakuwa umeshaijaribu kila kona!

Kwa ufupi ni kuwa utakuwa na uwezo mkubwa wa kuwa professional. Lakini bado baada ya Training utahitaji kuvifanyia mazoezi na kufanya kazi kwa muda ili vikae vizuri kichwani na mkononi.

Karibu sana!
 
Mkuu huwa mnatoa na course nyingine. (C,C++,python)?
Yes. Ila huwa tunakwenda serially na pia huwa tunaangalia interest ya watu katika Kozi husika. Katika Pool ya Languages, pamoja na Java tuna Python, C/C++, Swift, PHP na Elixir. Pia tunafundisha Shorter Courses kama Git SCM, SQL and DBMS, Secure Rest APIs na nyingine nyingi. Unaweza kuni PM email yako na kozi ambazo uko interested ili uweze kuwa alerted ratiba ikiwa tayari hata kabla haijaenda public
 
Nime update maelezo kwa wale waliopata shida kufungua PDF
 
Naomba kufahamu kama hutojali.

Wewe mwenyewe umeshafanya na kushiriki project zipi zilizofanikiwa na zinatumika?
Siwezi kusema kwa sababu ni project za kampuni na tuna mikataba ya kutunza faragha, ila kifupi ni kuwa project mojawapo ya hivi karibuni itatumika nchi kama Tatu za East Africa. Sitatoa details kwa sababu tajwa!

Lakini pia hizi training hazijaanza jana wala juzi ni Tangu 2013. Kuna waliopitia wengine ni wana JF wakiamua kusema utawasikia. Lakini pia kwa sababu tajwa sitawasema!

Kuongezea unaweza kupitia baadhi ya profiles zangu (sio zote)
 
Vigezo gani vinatumika? ikiwemo lugha ya ufundishaji ni ipi?? elimu nayo??
Vigezo kwa Foundation of Java ni kujua Kiingereza basic kiasi cha kuweza kuwasiliana na mwalimu, na pia ujue kutumia kompyuta. Hauhitaji kuwa unajua kitu chochote kuhusu programming. Ukiwa una idea ya programming hakuna tatizo but sio requirement.

Kwa kozi ya Android ni lazima uwe umepitia Foundation of Java kwa sababu tunajenga juu ya msingi huo.

Elimu ya mtu hatuulizi wala haituhusu kwa kuwa hii ni kozi ya kujifunza utaalam na sio shule kwa maana iliyozoeleka (Professiona course not Academic course). Ukiwa na degree haujui kabisa lugha ya kiingereza hautajiunga ila ukiwa darasa la nne na unaweza kuwasiliana unakaribishwa.

Lugha ya kiswahili inaruhusiwa pia hasa kwa maswali au kujieleza, ila Lugha official ni kiingereza kwa kuwa kunaweza kuwa na watu wa nchi nyingine ambao hawajui kiswahili.

Nimejitahidi kujibu ila kama kuna sehemu haiko wazi unaweza kuuliza
 
mnapatikana Wapi maana wingine tukisikia Programing na Java Hzo, huwa nahisi kama nimeongezewa miaka ya Kuishi.

Maskini wake hata kimoja Sina ujuzi nacho
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…