Hhahahaa uwi dunia in mambo jamani acheni tu
Basi buana juzi Kati natoka dar-dom kwenye siti nimekaa na mtu mzima Sana, no stori Hadi tunafika,mbele Kuna kijana wa makamo ambaye kwenye kiti hatulii Ni Kama anatamani Mzee akaye mbele yeye arudi nyuma tukae wote (wabadilishane),Kila baada ya dakika mbili ananiangalia.
Muda mwingine ikabidi anisemeshe kabisa ,Mambo vipi Safi ,tumefika msamvu tunashuka akasema vipi Safari yani kwa vyovyote anatamani kuongea na Mimi ila nafasi ikakosekana.
Tumefika Dom tunashuka akahakikisha anakaa nyuma yangu wakati wa kushuka akanisalimia vipi waelekea wapi nikamwambia ahha nashukuru nimepata mwenyeji ,unaondoka kwa usafiri gani nikasema boda boda ,tuchukue tax au bajaji usijali nitalipia naenda maeneo hayo hayo unayoenda,ok,sawa nikajibu
Akaita usafiri hao ,njiani naitwa Henry waitwa Nani ,naitwa lady of destiny unafanya kazi wapi nikamtajia ,aah buana nimeamishiwa dodoma uwe mwenyeji wangu daah maisha sijui yatakuwaje basi ghafla nikamwambia Mimi nimefika ok ,basi naomba mawasiliano Mana ofisi uliyopo ndo na Mimi nimehamia,japo nilikuja kujua yupo sehemu nyingine nyeti sana
Ok ok bye bye
Kesho badae simu za kutosha ananiuliza unaish wapi,kazi,na maisha yangu kwa ujumla ,nimekupenda na Nini na Nini hivyo
Sasa nikamuuliza familia iko wapi kasema dar ok nikajua huyu tayari Ni mume wa mtu ,ok njoo tuende lunch,njoo sijui tuende wapi,naomba one night nipo tayari kukupa chochote,hutajutia maamuzi yako ,
Yani ningekuwa mhuni ningemmaliza ,anapiga simu mara zaidi ya 20 per day,usipopokea unaenza kuta mced Cal hata 15 akianza kukutumia sms ukiandika moja kashaandika tano,njoo hapa hotelin nimekumis Yani maneno mengi , ikabidi nimwambie nina familia na Mr kafuma sms zake akapowa kidogo,
Tukaenda hivyo Nikaona hakati tamaa ,ghafla nikamtext sorry naomba uniazime elfu 50 nimepata dharura (sikuwa na shida )ila nilitaka tu kumkimbiza Mana nilishachoka na Sina tabia ya kutembea na watu wenye familia zao
Hadi Leo hiyo sms haijajibiwa ,sijajua kama alikufa au yupo hai